Serikali iingilie kati ukataji wa miti hii ya Matunda

Chizi Maarifa

JF-Expert Member
Jul 29, 2013
10,274
23,050
Miaka ya hivi karibuni kumetokea upungufu mkubwa wa maembe dodo katika soko la Dar es Salaam na pengine sehemu nyingine.

Maembe haya matamu yasiyo na mfanowe kiasi cha kutungiwa wimbo wa "embe dodo,embe dodo limelala mchangani" yamekuwa adimu baada ya kutokea mbegu nyingine ambayo imekuwa ikitoa embe ambazo kwa nje zinafanana na dodo lakini kwa ladha na harufu ni tofauti sana.

Nliamua kufanya utafiti kisa cha kupotea kwa maembe dodo asili na badala yake kuwa na embe hizi zisizo na taste wala harufu tamu. Wengi wanasema kumekuwa na tabia ya kukata miti ya maembe dodo na kuchoma mkaa au kukata mbao.

Jambo hili limekuwa likinihuzunisha sana kila unapofika msimu wa maembe sababu najua sitopata kwa urahisi embe dodo asili.

WITO KWA SERIKALI
Miti hii ya Maembe Dodo ilindwe na igeuzwe kuwa ni moja ya Nyara za Serikali kama ilivyo miti ya Mikoko n.k

Isiruhusiwe kuchomwa mkaa wala kukatwa mbao. Maembe pia ikiwezekana yawe ni tunda la Taifa. Embe dodo ni moja ya the best maembe ambayo nimewahi kula duniani.

Tunapopoteza hazina hii kwa kuleta maembe ya kisasa au ambayo yamekuwa grafted.kiuhalisia tunawatendea makosa sana hata wazazi wetu na wakale.maana haya matunda yamekuwa yakipewa sifa nyingi sana.
 
hahahahaha mkuu achana na maembe dodo tuko busy na uchaguzi wa uganda
 
Hatimaye kapatikana mtu wa kuisemea. Kiukweli hali ni mbaya. Mfano wilaya ya ifakara na Ulanga ukataji wa miti ya miembe na kusafirisha magogo yake kwenda Dar es Salaam imekuwa sasa ni jambo la kawaida. Ni muhimu serikali kuingilia kati maana miti ya maembe inaweza kutumika kama food security hasa pale watu wanapokosa kabisa chakula hasa kwa maeneo ya vijijini.

Miembe ilindwe
 
Upande wa pili wa shilingi umeuona? Kwa nini watu wanachongea aseti miembe,kwa nini haikukatwa nyuma na inakatwa sasa? Unajua kuwa serikali imezuia miti ya asili isikatwe kwa ajili ya mbao? Kila zuio huwa Lina madhara. Kwa upande mwingine Kukatwa kwa miembe dodo ni fursa kwa wajasilia Mali wapande mashamba ya kutosha ya miembe maana huko mbeleni itakuwa dili.
Huwa nashangaa kupita vijijini na kutoona mashamba ya miembe bali miti ya miembe iliopandwa mbali mbali.Kama kweli unaipenda TZ Nenda kapande miembe dodo ya asili ila utavuna baada ya miaka 10, wenye ukwasi wa hela wanapanda miembe ya kisasa.
 
Miaka ya hivi karibuni kumetokea upungufu mkubwa wa maembe dodo katika soko la Dar es Salaam na pengine sehemu nyingine.

Maembe haya matamu yasiyo na mfanowe kiasi cha kutungiwa wimbo wa "embe dodo,embe dodo limelala mchangani" yamekuwa adimu baada ya kutokea mbegu nyingine ambayo imekuwa ikitoa embe ambazo kwa nje zinafanana na dodo lakini kwa ladha na harufu ni tofauti sana.

Nliamua kufanya utafiti kisa cha kupotea kwa maembe dodo asili na badala yake kuwa na embe hizi zisizo na taste wala harufu tamu. Wengi wanasema kumekuwa na tabia ya kukata miti ya maembe dodo na kuchoma mkaa au kukata mbao.

Jambo hili limekuwa likinihuzunisha sana kila unapofika msimu wa maembe sababu najua sitopata kwa urahisi embe dodo asili.

WITO KWA SERIKALI
Miti hii ya Maembe Dodo ilindwe na igeuzwe kuwa ni moja ya Nyara za Serikali kama ilivyo miti ya Mikoko n.k

Isiruhusiwe kuchomwa mkaa wala kukatwa mbao. Maembe pia ikiwezekana yawe ni tunda la Taifa. Embe dodo ni moja ya the best maembe ambayo nimewahi kula duniani.

Tunapopoteza hazina hii kwa kuleta maembe ya kisasa au ambayo yamekuwa grafted.kiuhalisia tunawatendea makosa sana hata wazazi wetu na wakale.maana haya matunda yamekuwa yakipewa sifa nyingi sana.
Mzee, nunua shamba panda miembe ili baadae upige hela.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom