Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Kati ya vitu ambavyo mtu unajifunza baada ya kujaribu ni hili la gharama la kuchapisha vitabu Tanzania. Kwa muda mrefu nimekuwa nikitatizika sana na changamoto ya watoto wetu kujisomea na waandishi wengi kujiingiza kwenye uandishi wa vitabu. Wakati niko katika hatua za mwisho za kuchapisha kitabu cha "Majeruhi wa Mapenzi" nimepewa quotes za kuchapisha kitabu hiki Tanzania ambapo nimekuta kuwa VAT ni asilimia 18!
Mara moja nikaona mojawapo ya matatizo makubwa.
a. Nikiamua kuchapa vitabu mia tano tu kila kitabu (chenye kurasa 288) kina gharimu 39,500 najiuliza nitauza kitabu hicho kimoja kwa shilingi ngapi ili kurudisha japo gharama za kuchapishia?
b. Unapoweka gharama ya kodi kubwa kama hii ni watu wangapi wanaoweza kuchapisha vitabu Tanzania? Kwanini isiwekwe kwenye viwango vya chini na ikiwezekana 0% (zero rating protection0 kwenye vitabu vya lugha ya Kiswahili na vya masomo?
c. Hivi hatuoni kwa kufanya gharama ya kuchapisha vitabu kuwa kubwa sana tunachochea ujinga kwani ama vitabu vinakuwa ni vya bei ya juu sana au watu wengi ambao wanataka kuchapisha vitabu wanajikuta wanakwama. Kwa mfano, invoice mojawapo ya makampuni ninayozungumza nayo nyumbani kwa vitabu 5000 ni shilingi milioni 39. Matokeo yake wengi wanaochapisha vitabu Tanzania inabidi yawe ni mashirika au taasisi ambazo zinapata ufadhili fulani au watu ambao wana uwezo mkubwa wa kifedha?
d. Je, watawala wetu hawaoni umuhimu wa kupunguza au kuondoa kabisa VAT kwenye vitabu na badala yake waache kodi ilipwe wakati wa manunuzi kama (Sales Tax) ya kawaida badala ya kumpitishia mtunzi mzigo wa kodi?
Ombi langu:
Serikali ifute VAT kwenye vitabu visivyozidi kurasa 300 na kwa vile vinavyozidi basi VAT iwe kwa kiasi cha chini kinachowezekana. Ikumbukwe wachapishaji tayari wamelipa kodi kadhaa katika kuagiza malighafi mbalimbali na bado kuna gharama nyingine zinazoingia. Lengo ni kufanya vitabu vichapwe kwa urahisi na inaweza kuchochea ushindani mkubwa hata kwenye nchi za jirani ambako nako gharama ya kuchapisha vitabu ni kubwa au wameamua kuweka VAT (Kenya mwaka jana walitaka kuweka VAT ya 18% kwenye vitabu vya kiada).
Mara moja nikaona mojawapo ya matatizo makubwa.
a. Nikiamua kuchapa vitabu mia tano tu kila kitabu (chenye kurasa 288) kina gharimu 39,500 najiuliza nitauza kitabu hicho kimoja kwa shilingi ngapi ili kurudisha japo gharama za kuchapishia?
b. Unapoweka gharama ya kodi kubwa kama hii ni watu wangapi wanaoweza kuchapisha vitabu Tanzania? Kwanini isiwekwe kwenye viwango vya chini na ikiwezekana 0% (zero rating protection0 kwenye vitabu vya lugha ya Kiswahili na vya masomo?
c. Hivi hatuoni kwa kufanya gharama ya kuchapisha vitabu kuwa kubwa sana tunachochea ujinga kwani ama vitabu vinakuwa ni vya bei ya juu sana au watu wengi ambao wanataka kuchapisha vitabu wanajikuta wanakwama. Kwa mfano, invoice mojawapo ya makampuni ninayozungumza nayo nyumbani kwa vitabu 5000 ni shilingi milioni 39. Matokeo yake wengi wanaochapisha vitabu Tanzania inabidi yawe ni mashirika au taasisi ambazo zinapata ufadhili fulani au watu ambao wana uwezo mkubwa wa kifedha?
d. Je, watawala wetu hawaoni umuhimu wa kupunguza au kuondoa kabisa VAT kwenye vitabu na badala yake waache kodi ilipwe wakati wa manunuzi kama (Sales Tax) ya kawaida badala ya kumpitishia mtunzi mzigo wa kodi?
Ombi langu:
Serikali ifute VAT kwenye vitabu visivyozidi kurasa 300 na kwa vile vinavyozidi basi VAT iwe kwa kiasi cha chini kinachowezekana. Ikumbukwe wachapishaji tayari wamelipa kodi kadhaa katika kuagiza malighafi mbalimbali na bado kuna gharama nyingine zinazoingia. Lengo ni kufanya vitabu vichapwe kwa urahisi na inaweza kuchochea ushindani mkubwa hata kwenye nchi za jirani ambako nako gharama ya kuchapisha vitabu ni kubwa au wameamua kuweka VAT (Kenya mwaka jana walitaka kuweka VAT ya 18% kwenye vitabu vya kiada).