Serikali ifute na iadhibu vikali "house-girling"

GODZILLA

JF-Expert Member
Dec 26, 2014
5,902
10,502
Nimetembea humo majumbani unakuta katoto ka kike kana miaka tisa eti kanaitwa "house girl".

Katoto kadogo kanatumikishwa kazi nzito kuanzia alfajiri mpaka saa sita usiku. Eti "ameajiriwa".

Natambua, serikali imepitisha sheria mbalimbali za kuzuia kazi za watoto, kama vile sheria za kazi, sheria za shule na mikataba mbalimbali ya kimataifa!

Lakini sheria hizi sio rafiki na hazijatibu kabisa tatizo la watoto wadogo kutumikishwa majumbani.

Sheria zinazungumza kuhusu kuzuiwa kufanyishwa kazi nzito nzito za migodini nakadhalika. Lakini hazijasema ni namna gani watoto wadogo wa kike wanaweza kutwezwa majumbani kupitia hichi kinachoitwa "house girl".

Ni sheria legevu mno na hazitiliwi maanani.

Wakati mwingine najiuliza kama kuna vyombo vinavyosimamia kwa dhati hizi sheria za kuwalinda watoto! Pamoja na ulegevu wake, lakini huenda zingeweza kudhibiti huu udhalilishaji kwa kiwango fulani.

Hawa watoto wanalawitiwa na kunajisiwa, licha ya madhara mengine mengi ya kisaikolojia, traumatization, kukosa fursa ya elimu, kuadhibiwa vikali, kunyanyaswa, kufanywa watumwa na hata kuuwawa.

Kazi za majumbani zifanywe strictly na mtu mwenye umri wa zaidi ya miaka kumi na nane na hata juu zaidi ya hapo. Hii iwe criminalized kwa kiwango cha adhabu kali.

Futa kabisa hizi 'housegirl'. Wanatumia watoto wa watu vibaya mno na kwa namna ya kudhalilisha kulikopindukia.
 
Tatizo kubwa hapa ni ajira kwa watoto!! Serikali na wadau (ngo's) wajitahidi kudhibiti hili.

Pia hili kundi la wafanyakazi wa majumbani ni vyema sasa litupiwe jicho ikiwezekana wawekewe na viwango vya mshahara (sio tamko tu ila hata kisheria ikiwezekana) ili wasinyonywe kupindukia na waajiri wao.
 
Kwani wanalazimishwa kuajiriwa? Mbona mnakuwa wa ajabu aisee..

yote haya yanasababishwa na upumbafu wa serikali hao watoto walitakiwa wawe mashuleni education system ya hii nchi ni ya kuzimu purely
 
Wote mnaoshabikia hili ni aidha wanafiki au bado mnakula ugali majumbani kwa wazazi wenu hata mashemeji! Hamjawa na familia yaani baba, mama na watoto. Housegirl kwa mama mwenye mtoto na hapo hapo anatafuta riziki hakwepeki. Binti mdogo kama housegirl ana faida na hasara zake both sides. Tuache kuvimbiwa na kuanza kugeneralise. Kuna mahousegirls wameweza hata kuwa watu wa maana kupitia stage hii
 
Ungesema serikali iwatafutie shule na kazi ningekuelewa, lakini nakuona unabwabwaja tuu humui hawa watoto hutumwa na wazazi wao kutoka kijijini? Na wengine hata pesa wanachukua wao
Hajui alichoandika. Halafu anadhani woote wananyanyaswa.
Mi nilienda kufanya video shooting ya Kitchen Party ya House girl mmoja kule makongo juu ambae alikaa kwa Boss mpaka akachumbiwa.

Alipewa zawadi kama gas cookers plate 4 kubwa washing mashine dinner setsvitanda na mavitu kibao ma bonge la sherehe la msosi kujichotea.
Alikuwa ni dada mgogo wa Dodoma.

Wazazi wake walikuwa na hali sio nzuri kiuchumi, walikuja wao na zawadi ya karanga tu na walianza kutoa machozi wakati binti yao anakabidhiwa zile zawadi.
Yule Mama alimpenda sana yule house girl.
 
Wote mnaoshabikia hili ni aidha wanafiki au bado mnakula ugali majumbani kwa wazazi wenu hata mashemeji! Hamjawa na familia yaani baba, mama na watoto. Housegirl kwa mama mwenye mtoto na hapo hapo anatafuta riziki hakwepeki. Binti mdogo kama housegirl ana faida na hasara zake both sides. Tuache kuvimbiwa na kuanza kugeneralise. Kuna mahousegirls wameweza hata kuwa watu wa maana kupitia stage hii
Kama unahitaji msaidizi tafuta mwenye umri unaostahili!
 
yote haya yanasababishwa na upumbafu wa serikali hao watoto walitakiwa wawe mashuleni education system ya hii nchi ni ya kuzimu purely
Upumbafu ni wenu ninyi mnaowachukua watoto wadogo wakawe watumwa wa kufua nepi badala ya kuwaacha wasome na wakue.
 
Lililoleta hii mada litakuwa li mazwazwa, mtoto wa miaka 9 umamfahamu wewe au hata hujazaa? Huyo aliyeajiri mtoto wa miaka 9 halafu anamwamsha saa 9 usiku atakuwa na akili tumamu huyo? Nasema.hii mada ni uongo wa mchana kweupe!
 
Lililoleta hii mada litakuwa li mazwazwa, mtoto wa miaka 9 umamfahamu wewe au hata hujazaa? Huyo aliyeajiri mtoto wa miaka 9 halafu anamwamsha saa 9 usiku atakuwa na akili tumamu huyo? Nasema.hii mada ni uongo wa mchana kweupe!
Acha kujifanya unaishi Tanzania ambayo siyo hii tunayoishi wengine, na kama hujawahi muona housegirl mwenye miaka tisa labda huko kwenu Samvulachole
 
tumezoea kuona mada za kuwatolea povu waarabu kuwa wanawadhalilisha wa africa wanaokwenda kufanya kazi za ndani.

Lakini kiuhalisia ni afadhali ya hko arabuni kuliko bongo, Yani mtoto wa miaka 12 - 15 mzigo anaobebeshwa sio mchezo kabisa. na wengi unakuta hata huo mshahara hawapewi, Na ni hali ya kawaida tu ndani ya mazingira ya jamii zetu.

Yote haya yanatokana na Umaskini tulioletewa na CCM.
 
Back
Top Bottom