Kijakazi
JF-Expert Member
- Jun 26, 2007
- 6,407
- 8,900
Kutokana na Imani potofu tulizonazo juu ya ndege huyu Mzuri aina ya Bundi, ningeomba Serikali iamrishe Shule zote za Msingi ikiwezekana kunzia cheke chea wafuge huyu ndege aina ya Bundi, na watoto wafundishwe ya kwamba ni ndege mzuri na wa kawaida kama ndege mwingine wowote yule, watoto waruhusiwe kumshika na kumchezea kwa kufanya hivi nina imani kabisa hawa watoto wakikuwa wakubwa watakuwa hawana imani za kishirikina kama sisi tulivyo na labda pia itapunguza vifo vya watu wasio na hatia wanaouliwa kwa shutuma za kishirikina!