Serikali ifuatilie utendaji wa uongozi wa Chuo cha Kilimo cha Sokoine (SUA)

Hot bird

Member
Jan 18, 2021
56
100
Wakuu habari zenu hapa ndani?

Nimeandika uzi huu kwa ajili ya kusaidia maendeleo ya taifa na ustawi wa jamii kwa ujumla, hii ni kutokana na ukweli kuwa taasisi nyingi za serikali zinaendeshwa kwa utendaji mbovu, sasa leo naandika machache kuhusu chuo cha kilimo cha sokoine (SUA), kilichopo Morogoro.

1. Ndio chuo chenye umaskini wa hali ya juu, yaani ni kawaida kabisa kukuta wahadhiri wake wakilalamika kukosa pesa za kuendelezwa sababu tu chuo hakina pesa wakati huohuo vyuo vingine mambo yanaenda vizuri tu.

2. Miundombinu ya chuo hasa kufundishia ni mibovu na imechoka sana (nitaambatanisha picha ya wanafunzi wakisomea nje ilhali lecturer yuko ndani).

3. Chuo kina wakufunzi WENGI ambao wamesoma hapohapo na hata mkiitwa interview wengi watachukua wanafunzi waliosoma hapohapo,hii imesababisha hali ya kutohoji utendaji wa viongozi wa chuo.

4. Magari ya chuo yana hali mbaya,na uongozi haujali wala haufatulii hili (kiambatanisho kipo).

5. Kuna rushwa kubwa ya ngono chuoni, hasa kwa wahadhiri na wale watu wa hostel, wanataka sana rushwa kwa wanafunzi hasa wa kike.

6. Barabara za chuo hazikidhi vigezo vya chuo kikuu, tena hapa uongozi umejinasibu kuwa umetengeneza barabara ila ni kwa kiwango duni sana pesa itakua imeliwa.

7. Vitendea kazi (mfano projector) vya kufundishia havipo kwa baadhi ya vitivo na kwa wenye navyo basi vipo vichache sana.

Naandika uzi huu kuomba serikali ifatilie utendaji kazi wa chuo hiki, yawezekana kabisa VC wa chuo anafanya kazi nzuri sana ila kuna utaratibu mbovu wa watu wa chini yake.


 
wanasuaso hao.. round cafeteria, multipurpose hall, new lecture theatre, uwanja wa nyumbani freedom square kwa wale wakusapua kama mm. prof Maganga wa Department ya Forestry yupo?
 
Wakuu habari zenu hapa ndani?

Nimeandika uzi huu kwa ajili ya kusaidia maendeleo ya taifa na ustawi wa jamii kwa ujumla, hii ni kutokana na ukweli kuwa taasisi nyingi za serikali zinaendeshwa kwa utendaji mbovu, sasa leo naandika machache kuhusu chuo cha kilimo cha sokoine (SUA), kilichopo Morogoro.

1. Ndio chuo chenye umaskini wa hali ya juu, yaani ni kawaida kabisa kukuta wahadhiri wake wakilalamika kukosa pesa za kuendelezwa sababu tu chuo hakina pesa wakati huohuo vyuo vingine mambo yanaenda vizuri tu.

2. Miundombinu ya chuo hasa kufundishia ni mibovu na imechoka sana (nitaambatanisha picha ya wanafunzi wakisomea nje ilhali lecturer yuko ndani).

3. Chuo kina wakufunzi WENGI ambao wamesoma hapohapo na hata mkiitwa interview wengi watachukua wanafunzi waliosoma hapohapo,hii imesababisha hali ya kutohoji utendaji wa viongozi wa chuo.

4. Magari ya chuo yana hali mbaya,na uongozi haujali wala haufatulii hili (kiambatanisho kipo).

5. Kuna rushwa kubwa ya ngono chuoni, hasa kwa wahadhiri na wale watu wa hostel, wanataka sana rushwa kwa wanafunzi hasa wa kike.

6. Barabara za chuo hazikidhi vigezo vya chuo kikuu, tena hapa uongozi umejinasibu kuwa umetengeneza barabara ila ni kwa kiwango duni sana pesa itakua imeliwa.

7. Vitendea kazi (mfano projector) vya kufundishia havipo kwa baadhi ya vitivo na kwa wenye navyo basi vipo vichache sana.

Naandika uzi huu kuomba serikali ifatilie utendaji kazi wa chuo hiki, yawezekana kabisa VC wa chuo anafanya kazi nzuri sana ila kuna utaratibu mbovu wa watu wa chini yake.

View attachment 1688968
Wanafunzi wako nje wakisikiliza kipindi kinachoendelea ndani ya darasa kutokana na wingi wa wanafunzi.

View attachment 1688969
Funguka mkuu vizuri, kuna viongozi wapo humu watafuatilia
 
Dah. Hivi mimi najiuliza chuo kuchukua wanafunzi wengi kuliko capacity yake ni order kutoka serikalini au TCU ndio inaamua au vp? Anayefahamu kuhusu hili anijuze, kwa sababu siku hizi hapo SUA kuna utitiri wa wanafunzi ukilinganisha na mazingira halisi.
 
Hapo wanafunzi wanaosomea nje ni kama kule Mazimbu campus....
 
IMG-2021.jpg
huyo mwamba kulia hapo ,mbona kama hafatilii hata hicho kipindi chenyewe ....🤣
 
Dah. Hivi mimi najiuliza chuo kuchukua wanafunzi wengi kuliko capacity yake ni order kutoka serikalini au TCU ndio inaamua au vp? Anayefahamu kuhusu hili anijuze, kwa sababu siku hizi hapo SUA kuna utitiri wa wanafunzi ukilinganisha na mazingira halisi.
Mashule yanayozalisha wanafunzi ni mengi pia ndio maana sasa hivi wanafunzi ni wengi.
 
Si bora hata hiyo SUA umesema inawalimu, nenda DIT utabloo utasema sio bongo....part timers ndo wamejazana na kulipwa kwao hadi ngumi zipigwe. Mkuu wa chuo yupo,katibu mkuu yupo,waziri yupo na miaka inakatika tu.
 
Niliwahi kusema huko nyuma ya kwamba course kama Rural Development si kozi za hadhi ya kufundishwa SUA, kama vipi chuo kiitwe Sokoine University tu, neno Agriculture liondolewe maana haiwezekani kozi ambazo zinaweza kufundishwa hata udom na Jordan, KIU n.k zifundishwe SUA
 
No 3.nakuunga mkono asilimia 100% ni ngumu kumpinga mwalimu wako uliyekuwa unampigia magoti asikukakamate ( wakufunzi ni miungu watu) wamepewa mamlaka makubwa sanaaaa .pia ajira zake kila mmoja ana aliyembebe ( trust me ) bila wakukujua sua kazi hutoboi

Ushauri

1.Ajira ziletwe utumishi wao wapelekewe wafanyakazi ,mambo ya kujazana wakufunzi kipindi cha usaili ndo chanzo cha hayo ya kujuana

2.Ajira ziwe kwa kila MTU ,sio mpaka aliyesoma sua ( trust me kama hujasoma sua una asilimiaa 2% ya kutoboa usaili kama waliosoma sua wapo humu)

3. Interview ziwe open kama zinafanyika sua wawepo waangalizi wengine hata kwa kujiinga kupitia Skype au zoom ndo watapatika waliofaulu kwa uwezo wao

Pongezi : ukigraduate sua kwa kweli huwez penya kiujanja ujanja miaka yote hata kama kuna kubebwa lazima na we uwe unabebeka

Sent from my TECNO CF7 using JamiiForums mobile app
 
Daaah, mkuu umesema vema na yote Ni kweliii, hostel mbovu kabisaa, huko mazimbu ndo aibu kabisaaa, hostel Hadi madarasa, barabara mbovu hasa kipindi Cha masika,
Hostel za kihonda nazo changamoto!!
SUA inahitaji maboresho makubwa Sana Tena Sana
 
Back
Top Bottom