Serikali ifikirie kwa kina kuwa na "Shirika la Maji la Taifa" na pia kuanzisha "Rural Water Access Agency" ya maji vijijini kama umeme wa REA

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Watu wanasema unapokuwa na njia ambayo kwa miaka mingi haizai matunda na bado unaing'ang'ania badala ya kutafuta njia mbadala ya kutatua tatizo, wewe una tatizo la akili.

Suala la upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi, mijini na vijijini, limekuwa jambo ambalo limeumiza kichwa serikali kwa miaka mingi sana. Kuna wakati huduma hii ilikuwa chini ya mamlaka ya serikali mija kwa moja - Idara ya Maji chini wa Wizara. Hili halikufaniliwa.

Utaratibu wa huduma za maji uliopo sasa ndio unachanganya kuliko hata huko nyumba. Tunashindwa kuelewa nani hasa ndio mwenye mamlaka kaitika suala la maji. Unakuta Wiara ipo, na serikali za miji zipo, na mwisho wa siku haieleweki nani ana mamlaka zaidi ya mwenzake.

Kuna Board za maji zimeanzishwa lakini ni kama hazina meno, zipo zipo tu!

Sasa wakati umefika tutafute namna mpya ya kushughulika na suala la maji nchini. Tunapaswa kufikira kwa makini uwepo wa Shirika la Maji la Taifa, ambalo majukumu yake yatakuwa kama lilivyo TANESCO, na pia kuwa na Rural Water Access Agency, ambayo majukumu yake yatakuwa kama ilivyo REA. Shirika hili linaweza kuwa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu kulipa uzito au Wizara ya Maji ikibidi

Kwa upande wa Shrika la Maji, hili litapaswa kujiendesha kibiashara. kwa ngazi ya Taifa, Mkoa na Wilaya. Ruzuku toka serikalini inaweza kuwapo mwanzoni lakini baada ya muda fulani tutatarajie lijiendeshe kwa faida.

Ni kweli huko nyuma tulikuwa na NUWA (National Urban Water Authority) , na lengo lilikuwa zuri bali lilikumbwa na mihemuko ya kisiasa enzi za ubinafsishaji likatenguliwa. Tuanzishe kitu bora zaidi.

Rural Water Access Agency, kama ilivyo REA, itapewa ruzuku toka serikalini, na pia kutakuwa na levy (tozo) toka kwenye bili za maji za Shirika la Maji la Taifa kwa ajili ya kuendeleza upatikanaji wa maji vijijini.

Ningependa sana Kitila Mkumbo watafakari kwa makini pendekezo hili na kulifikisha kwa Magufuli ili lifanyiwe utekelezaji.
 
... Siku hizi almost kila wilaya ina mamlaka ya maji. Hizo bado hazitoshi kianzishwe tena chombo kingine?
Hapana Mkuu. Ni kwamba siku hizi suala la maji liko kwa kiasi fulani liko halmashauri za miji, lakini kumbuka halmashauri za miji haziko chini ya wizara ya maji, ziko chini ya Tamisemi na bado maji ni jukumu la Waizara ya maji. Ndio maana nikasema hii inaleta mkanganyiko tu. Suala ni kuondoa maji halmashauri za miji na Wizara ya maji na kuanzisha shirika linalojitegemea chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu kama mashirika mengine ya umma.
 
Hapana Mkuu. Ni kwamba siku hizi suala la maji liko kwa kiasi fulani liko halmashauri za miji, lakini kumbuka halmashauri za miji haziko chini ya wizara ya maji, ziko chini ya Tamisemi na bado maji ni jukumu la Waizara ya maji. Ndio maana nikasema hii inaleta mkanganyiko tu. Suala ni kuondoa maji halmashauri za miji na Wizara ya maji na kuanzisha shirika linalojitegemea chini ya Ofisi wa Waziri Mkuu kama mashirika mengine ya umma.
Nimekusoma mkuu
 
Safi sana mkuu this is one of the best idea
Shukurani Mkuu. Saidia kufikisha mapendekezo kwa wanaohusika

Na actually, hii approach imetumika kwa mafanikio kwa TANROADS na TARURA kwa huduma za barabara, TANESCO na REA kwa huduma za umeme. Ona kwamba suala la tozo (levyy) kwa TANROADS na REA limesaidia sana. Levy ya TANROADS iko kwenye mafuta na levy ya REA iko kwenye bill ya umeme.

Kwa hiyo tunakuwa na something similar kwa ajili ya huduma za maji.

Japo nina reservation sana na TANROADS wanavyotumia levy ya road mainatance, lengo ni zuri sana, tatizo kidogo hapo kwenye uongozi. I seriously think Mfugale anatakiwa apumzike sasa, Magufuli asiweke mbele urafiki dhidi ya maslahi ya taifa
 
Huu wingi agencies and authorities hautusaidii kabisa. Juzi tu hapo serikali imefuta mamlaka kadhaa za maji na kuunganisha na zingine. Tuna mataasisi mengi sana yasiyofanya chochote zaidi ya kula kodi za wanyonge. Tatizo ni mipango na mikakati mizuri hata ukiwa na mamlaka ngapi kama hakuna watu wenye maono na akili nzuri utaishia kulipa watu mabilioni kila mwezi huku wapo maofisini wanachati kila siku.
 
Huu wingi agencies and authorities hautusaidii kabisa. Juzi tu hapo serikali imefuta mamlaka kadhaa za maji na kuunganisha na zingine. Tuna mataasisi mengi sana yasiyofanya chochote zaidi ya kula kodi za wanyonge. Tatizo ni mipango na mikakati mizuri hata ukiwa na mamlaka ngapi kama hakuna watu wenye maono na akili nzuri utaishia kulipa watu mabilioni kila mwezi huku wapo maofisini wanachati kila siku.
Heee! Wingi wa taasisi kwani zinafanya kazi moja? Ukiwa na taaisis na zote zinashughulika na jambo lile lile hapo utasema wingi wa taasisi hautusaidii. La sivyo inakuwa ni argument haina mshiko na kama wamefuta taaisi kwa kuwa ni nyingi lakini zinashughulika na mambo tofauti basi hawana akili.

Ni sawa na kusema kwa nini tuna shirika la reli, na la umeme, na la ndege, na la simu, na la mafuta, kwa hiyo yamekuwa mengi futa mengine au yapunguzwe. Ni mwendawazimu tu ndio anaweza kutoa argument kama hiyo
 
Hii ipo japo sio kwa jina ukilopendekeza wewe, iliyopo inaitwa RUWASA (Rural water supply and sanitation agency ).
Fuatilia vizuri hasa kwa halmashauri za vijijini.
Hee Mkuu, kama wapo basi hawafanyi kazi yao sawasawa! Sijawahi hata kuwasikia.
 
Mkuu wazo lako ni zuri lakini ni wazi kwamba hizi idara,mamlaka,bodi,wakala na zile ministerial departments kwa Tanzania nyingi zinafanya kazi zile zile za mamlaka ya serikali za mitaa.
Hoja kubwa ni kutengeneza kile ambacho kinaitwa "legal and reguratory framework" kufanya kila idara au bodi au wakala kuwa kuwajibika ipasavyo.
Mfano kulikuwa hakuna haja kubwa ya kuwa na TANROADS na TARURA ni kujiongezea admninistrative expenses ambazo hazina maana.
Nchi hii haiwezi kuja kutoka kwenye nakisi au deficit ya kibajeti. Maana hatuna regulatory framework nzuri ndio maana kurahisisha majukumu tunaunda idara kila uchao bila kujua tunaongeza expenses
 
RUWASA ipo ndo kwanza imeanzishwa hata mwaka haijamaliza... Fuatilia kwa ukaribu tamko la Rais la tarehe 10.5.2018 kuhusiana na sekta ya ardhi na sekta ya maji.

The Government is ahead of you
 
Mkuu wazo lako ni zuri lakini ni wazi kwamba hizi idara,mamlaka,bodi,wakala na zile ministerial departments kwa Tanzania nyingi zinafanya kazi zile zile za mamlaka ya serikali za mitaa.
Hoja kubwa ni kutengeneza kile ambacho kinaitwa "legal and reguratory framework" kufanya kila idara au bodi au wakala kuwa kuwajibika ipasavyo.
Mfano kulikuwa hakuna haja kubwa ya kuwa na TANROADS na TARURA ni kujiongezea admninistrative expenses ambazo hazina maana.
Nchi hii haiwezi kuja kutoka kwenye nakisi au deficit ya kibajeti. Maana hatuna regulatory framework nzuri ndio maana kurahisisha majukumu tunaunda idara kila uchao bila kujua tunaongeza expenses
Sawa kabisa kuu. Kuna wakati pia nilijiuliza sana kwa nini TARULA haikufanywa idara ndani ya TANROADS ili kupunguza gharama za uendeshaji? Nakuelewa vizuri kabisa.
 
Back
Top Bottom