Serikali ifanye haya kukabiliana na tatizo la ajira kwa vijana

mserekale

Member
Jul 4, 2019
79
103
Kutokana na wimbi la ukosefu wa ajira kwa vijana ni vyema serikali ikafanya mikakati ya makusudi kukabiliana na hili tatizo.

Haya ni mawazo yangu binafsi kuhusu nini kifanyike;

1. Kudhibiti bidhaa za nje(massive importation of goods).Bidhaa za nje kwa kiasi fulani zinachangia kuua soko la ndani hivyo kuwakosesha vijana wetu ajira na fursa za kujiingizia kipato.

Katika hili serikali ni vyema ikaweka mikakati madhubuti ya kudhibiti bidhaa zinazotoka nje ya nchi ambazo zinawezekana kutengenezwa hapa nchini kwetu kwa mfano bidhaa za samani(furnitures) kama vile makabati, viti vya kukalia, masofa n.k
Kwa kufanya hivyo itasaidia kuinua soko la ndani na vijana wetu watahamasika kujiajiri kwenye shughuli hizo za mikono.

2. Kuongeza fursa na nafasi za ajira serikalini. Kuna haja ya serikali kuwaajiri vijana ili walitumikie Taifa katika sekta ambazo zina upungufu wa watumishi ambao unaweza kuchangiwa na masuala ya kustaafu, vifo, kufukuzwa kazi ama upungufu wa wataalamu katika sekta husika.

3. Vijana wapewe elimu ya kilimo, biashara na ujasiriamali. Kuna haja ya serikali kuanzisha masomo ya kilimo, ujasiriamali na biashara mashuleni kama masomo ya ziada ili elimu watakayoipata kwenye masomo hayo iwasaidie kujiajiri nje na taaluma walizosomea.

4. Serikali ifanye jitihada ya kuwekeza katika viwanda vya kusindika mazao na matunda ili vijana wajiajiri kwenye sekta ya kilimo.

5. Serikali ifanye jitihada za kutafuta masoko ya wakulima ili vijana watakaojiajiri kwenye kilimo wapate sehemu ya kuuza mazao yao.

Kama kutakuwa na mawazo mengine tofauti na haya naomba tuyashirikishe katika uzi huu lengo likiwa ni kuisaidia serikali kukabiliana na changamoto ya ajira kwa vijana.

Asanteni na karibuni kwa mawazo zaidi juu ya nini kifanyike.
 
Tupo busy kujenga stg, flyover ubungo, na kununua ndege,

Kuhusu ajira sio kipaombele changu mimi, labda ntawafikilia hapo mwakani nikiingia tena ikulu,
 
Tupo busy kujenga stg, flyover ubungo, na kununua ndege,

Kuhusu ajira sio kipaombele changu mimi, labda ntawafikilia hapo mwakani nikiingia tena ikulu,
Hayo yote yafanyike lakini pia serikali itambue kuna maelfu ya vijana wanasota mtaani kwa kukosa ajira. Ni vema serikali ikalitizama hili suala kwa jicho la karibu
 
Hayo yote yafanyike lakini pia serikali itambue kuna maelfu ya vijana wanasota mtaani kwa kukosa ajira. Ni vema serikali ikalitizama hili suala kwa jicho la karibu
Ongezea hii.vijana wanaotaka kuanzishaa biashara baada ya kuhitimu wasidaiwe kodi na vingine vingine kwa mda wa miaka 2 au mitatu mpaka watapoimarika kibiasha ra na kuweza kujimudu pia kuajir wenzao
 
Ongezea hii.vijana wanaotaka kuanzishaa biashara baada ya kuhitimu wasidaiwe kodi na vingine vingine kwa mda wa miaka 2 au mitatu mpaka watapoimarika kibiasha ra na kuweza kujimudu pia kuajir wenzao
Hili ni bonge la wazo.
Serikali itengeneze "tax holiday" ya miaka hata 3 kwa wahitimu wa vyuo vikuu wanaotaka kuanzisha na kuendesha biashara nchini.
Pia wapewe mikopo isiyo na riba.
 
Hakuna kipindi ambcho future za watu wengi zmeharibika kama kipindi hiki

Alomaliza chuo ukimuuliza malengo yake...hajui

Alonunua kiwanja ukimuuliza lini atajenga hajui

Aloajiriwa ukimuuliza mustakabali wa maisha yake...hajuii

Na wale wapenzi ambao walikuwa wanawasubiria wapenzi wamalize chuo...wpate ajira....maisha ya ndoa yaanze...ndo wameshaachana coz mwanamke hawez kukaa na mtu ambye hajui future yake

Sasa hivi kila kichwa kitajenga future yake...
 
Sio serikali ya CCM labda ibadilike. Mtaji wa CCM na serikali ni maskini na watu wasiojielewa. Ikifanya haya uliyoyataja ina maana itakuwa inajikaanga ili iondoke kwenye kutawala nchi. Hakuna serikali ulimwenguni inayopenda wenye akili kama za kwako.
 
Ongezea hii.vijana wanaotaka kuanzishaa biashara baada ya kuhitimu wasidaiwe kodi na vingine vingine kwa mda wa miaka 2 au mitatu mpaka watapoimarika kibiasha ra na kuweza kujimudu pia kuajir wenzao
Nadhani hapa umemaanisha "mtaji" ila ponit yako imeeleweka. Asante sana kwa mchango mzuri

Tuendelee kuwaomba wahusika wayafanyie kazi mawazo yote yatakayotolewa hapa.
 
Ajira sio tatizo tatizo vijana wanasoma ilimladi tu wana degree hawasomi kulingana na soko linataka nini
UKo sawa kabisa ....
Niliwahi kuandika hapa JF kwamba kwa Tanzania ajira ndo hakuna lakini kazi ziko nyingi sana. Binafsi hata muda wangu hautoshi kwa kazi zangu lakini ukimwambia mtu aje tusaidiane kufanya hizo kazi ... swali la kwanza ni MSHAHARA UTANILIPA KIASI GANI ...
Hapo ndo utachoka ....
Niliwahi pia kutoa mawazo ya biashara ... lakini cha kushangaza ni watu watano tu (tena wawili toka Zanzibar) ndo walifanyia kazi baadhi ya mawazo hayo.
Majuzi tulikuwa na program ya kuondoa umaskini wa kipato kwenye ngazi ya kaya ... vijana hawafundishiki ... hawaeleweki ... wao wanafikiri kwamba unapowaanzishia program tayari wewe umeishalipwa na donor kwa ajili ya kuanzisha program hiyo.... ULEMAVU WA FIKRA.
 
Kwa kuongezea tu hata ndoa nyingi kwa sasa zimesimama. Wengi wamewekeana ahadi za kuoana mara baada ya kupata ajira lakini mambo yako tofauti kidogo na matarajio yao na hiki ndicho chanzo cha mahusiano mengi kuvunjika.
Hakuna kipindi ambcho future za watu wengi zmeharibika kama kipindi hiki

Alomaliza chuo ukimuuliza malengo yake...hajui

Alonunua kiwanja ukimuuliza lini atajenga hajui

Aloajiriwa ukimuuliza mustakabali wa maisha yake...hajuii

Na wale wapenzi ambao walikuwa wanawasubiria wapenzi wamalize chuo...wpate ajira....maisha ya ndoa yaanze...ndo wameshaachana coz mwanamke hawez kukaa na mtu ambye hajui future yake

Sasa hivi kila kichwa kitajenga future yake...
 
Halmashauri karibia zote zinamapungufu ya watumishi, kazi zimekwama sana sehemu nyingi ila watu hawasemi.Nina rafiki yangu aliajiriwa kama Social welfare officer wilaya fulani ila ni mwaka sasa anakaimu kama Hr
 
Sio serikali ya CCM labda ibadilike. Mtaji wa CCM na serikali ni maskini na watu wasiojielewa. Ikifanya haya uliyoyataja ina maana itakuwa inajikaanga ili iondoke kwenye kutawala nchi. Hakuna serikali ulimwenguni inayopenda wenye akili kama za kwako.
Mi nafikiri ikifanya hivyo ndipo itakuwa imejiwekea mazingira mazuri ya kubaki madarakani tofauti na ilivyo sasa..
 
Mi nafikiri ikifanya hivyo ndipo itakuwa imejiwekea mazingira mazuri ya kubaki madarakani tofauti na ilivyo sasa..
Mtu mwenye kujua kesho yake akili yake inafunguka ... akili ikifunguka hawezi kuendelea kunyenyekea kwa tabaka la wanyanyasaji.
 
Halmashauri karibia zote zinamapungufu ya watumishi, kazi zimekwama sana sehemu nyingi ila watu hawasemi.Nina rafiki yangu aliajiriwa kama Social welfare officer wilaya fulani ila ni mwaka sasa anakaimu kama Hr
Upungufu wa watumishi upo karibia kila sekta as you have said ukienda mashuleni utakuta kuna upungufu wa walimu, ukienda kwenye hospitali zetu na vituo vya afya utakuta kuna upungufu wa madaktari, wauguzi, watabibu n.k na sekta zingine hivyo hivyo

Kwa hiyo ndiyo maana katika hoja yangu ya pili nimesema kuna haja ya serikali kuongeza fursa za ajira serikalini ili kukabiliana na huo upungufu wa watumishi. Hii pia itasaidia kupunguza idadi kubwa ya vijana walioko mtaani kwa ukosefu wa ajira.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom