Tango73
JF-Expert Member
- Dec 14, 2008
- 2,128
- 1,225
Baada ya kufa kwa ukomunisti duniani, China inawatupa kwa nguvu wanavijiji wake{proleretariants) barani Africa. Hawa wachina ni wale jamii ya watu waliojulikana kama proleretariants au walala hoi wasio na elimu na uwezo wa kumiliki mali. Wengi wao elimu yao wameishia darasa la nne. Watu hawa hivi sasa ni mzigo mkubwa sana kwa serikali ya China hivi sasa ndio maana inawatupa kijanja katika nchi za Africa.
Zambia wamelalamika nusura ya kuandamana kwa sababu wachina hawa wanafanya kazi za raia wao masikini kama vile kuuza maandazi, korosho na ubwabwa mitaani. Serikali isipowaangalia wachina hawa itakuja kujutia miaka ya 2090 maana watafikia uwezo wa kumiliki ardhi na raia wetu kubakia wapagazi wao.
Zambia wamelalamika nusura ya kuandamana kwa sababu wachina hawa wanafanya kazi za raia wao masikini kama vile kuuza maandazi, korosho na ubwabwa mitaani. Serikali isipowaangalia wachina hawa itakuja kujutia miaka ya 2090 maana watafikia uwezo wa kumiliki ardhi na raia wetu kubakia wapagazi wao.
Kuna kipindi nilikuwa China kikazi, nikabahatika kumuuliza Balozi wetu wa Tanzania huko, kwa wakati huo kwa nini wanatoa viza kwa wachina kuja Tanzania kama ubuyu?.
Yule balozi alinijibu kwamba ukiwaminya kuja nchini basi na serikali yao inabania viza za Wafanyabiashara wetu kwenda huko, akanipa mfano Waziri Nyalandu wakati huo alipoendesha zoezi la kuwafagia Wachina Kariakoo, China ilirespond kwa kuminya idadi ya viza za wafanyabiashara wetu!.
Balozi akaniambia kuwa, tatizo pia liko kwa taasisi nyingine za serikali ambazo kwa rushwa zinatoa vibali mbalimbali na nyaraka muhimu.
Na Wachina ni wajanja, wakifika wanatafuta vibali na documents zote zinazohitajika hata kwa Rushwa, kiasi kwamba ukitaka kumrudisha wanalalamika kwamba wameonewa na hivyo kuibua mgogoro wa kidiplomasia!
Hata hivyo nilimtahadharisha balozi kwamba, Iwapo mtaendelea kutoa viza kama njugu, na iwapo serikali Itaendelea kuwa corrupt katika taasisi za vibali, basi tutajikuta nchi hii baada ya miaka 50 kuna demographics tofauti kabisa na tulivyo sasa, Wachina watakuja, watazaa na Watanzania, Watoto wao watakuwa watanzania, watamiliki ardhi, wataingia bungeni na huwezi jua loyalty yao itakuwaje?
China inajaribu kutumia muscle yake ya kiuchumi kutapanya watu wake, kama leo unavyoona Singapore kuna Chinese ethnic people kibao, Malaysia na nchi nyingi za Asia, hawa huwa bado wanaitizama China kama motherland.
Ukitaka kufahamu akili ya China, kuna kisa cha kweli ambapo wakati Marekani inafanya mazungumzo ya kurejesha mahusiano ya Kidiplimasia na Marekani, Mao ZeDong ( Mao Tse Tung) alipendekeza kwa Raisi Nixon, China ipeleke mamia ya mabinti marekani kama gesture ya urafiki mpya, lakini Nixon alikataa hili wazo kistaarabu. Ni dhahiri Mao hapa alikuwa anapiga mahesabu ya mbali.
Kiufupi ni hivi:
Serikali itoe viza chache kwa wachina wasio wawekezaji kuja nchini, pili ihakikishe Ina Computerize mifumo ya Kutrack Wageni,
Tatu ihakikishe Mgeni hatoi pesa benki, Hapati huduma ya malazi gesti au hotelini mpaka atoe Passport yenye viza halali.
Nne ni lazima serikali iandae operations za kuwakumbusha ( japo kiakili) kwamba wageni bado ni wageni wasijisahau, Operations hizo ni kama kuwauliza waonyeshe passport zao, kama ziko poa basi ok, lakini kama haziko vizuri wawe deported.
Kule Guangzhu kwenye waafrika wengi, shurti mgeni atembee na Pasipoti, na hupati huduma yoyote mpaka uwe nayo, na wakati wowote polisi anaweza kukuuliza umuonyeshe passport yako!
Tusikubali umasikini wetu ukatupeleka kuuza identity ya Nchi, mchina ukimuachia utajikuta miaka 100 ijayo wako asilimia 40 ya population nzima, Wenzetu wako strategic!