Serikali ianze mpango wa Mgao wa Chakula na ianze na Dar?

Kuna mambo manne nayaona. Kwanza ni kweli kabisa kuna mbadiliko ya hali ya dunia na ukame unakuwa ni janga. Bahati nzuri katika nchi yetu tuna mito mikubwa ambayo inaathirika kutokana na tributaries kukauka lakini haikauki kabisa. Kwa wenzetu wenye irrigation scheme huweka reservoir kukabiliana na hali kama hiyo, sisi hatujafikiria hilo kama waziri mkuu Pinda alivyokiri mbele ya ugeni wa India. Si sahihi kufikiri mkulima au wakulima wanauwezo wa kujenga reservoir hasa wa kilimo chetu cha mkono.

Pili, ni kweli pia wananchi wanatakiwa wabuni mbinu za umwagiliaji. Mimi nimezaliwa katika maeneo ambayo kilimo cha umwagiliaji kilianza miaka 150 iliyopita na kina jina la asili,mifereji hiyo ipo na mingine imwekewa miiko(kulinda). Utashangaa siku hizi watu wamebomoa mifereji hiyo na eneo letu linaathirika kama maeneo mengine.
Yapo maeneo yasiyohitaji pump bali utaratibu wa mifereji kwani maji yaliyopo yanatiririka. Ukienda maeneo hayo utamaduni umetoweka, vijana wenye nguvu wametimkia mjini na wazee waliopo wanaishi ili siku ipite. Kilimo cha namna hii hakiwezi kukabiliana na njaa.

Tatu, serikali ina mkono pia kwasababu mkulima wa nyanya pale kipera na mlali morogoro anauza tenga lake kwa sh 2500. Sasa huyu mtu mpaka akusanye 300,000 za kununua pump sijui maisha yanamsubiri huku kukiwa na mlo, ada n.k. Endapo angepata bei nzuri nina hakika angeongeza uzalishaji na kwa njia hiyo uzalishaji wa mazao muhimu kama yanafaka ungezalisha ziada na kukidhi mahitaji ya nchi. Kuna atakayesema aende bank, lakini je kuna bank itampa mtu mkopo asiye na hata akaunti? Serikali inatakiwa ijenge mazingira ya kumwezesha mkulima kwa bei na upatikanaji wa mitaji. Ulaya na marekani wanafanya hivyo ndio maana mkulima ana insurance, nikimaanisha serikali zao hazikuwaacha tu bali ziawajengea mazingira mazuri. Ireland ilipiga marufuku uingizaji wa mayai ili kumjengea mkulima mazingira mazuri ya bei.

Nne, mwaka jana december kuna mbunge amelalamika kuwa watu wa sumbawanga waruhusiwe kuuza mazao nje. Ni sawa kwasababu wanamahijtaji kama watu wengine. Kama serikali ingenunua chakula kile na kukihifadhi badala ya kuachia kiende nje, huenda leo tungekuwa na ziada ya kuuza kwa bei nzuri Kenya na Somalia. Sioni mantiki ya kuacha chakula kiuzwe nje halafu tuagize kwa pesa za kigeni. Sijui kama SGR yetu ina ukubwa wa kiasi gani kitaifa lakini upo umuhimu wa kuangalia suala la hifadhi. Wakati wa miaka ya 1980.... tuliwahi kuletewa mchele kutoka Japan na Korea. Ulikuwa sio mzuri na maelezo yalikuwa ni chakula cha msaada kwani wanasafisha maghala na mchele huo ulikuwa wa miaka 10.
Sisi tunashindwaje kuhifadhi chakula hata kama hali ya hewa ni nzuri miaka 2 tu?

Taarifa za mashirika ya kimataifa zinaonyesha kuna balaa la njaa East Africa hasa Kenya na Somalia. Historia inaonyesha kuwa kunapokuwa na matatizo kama hayo kwa jirani zetu sisi huwa ni waathirika kutokana na mahitaji yanayochochewa na bei. Kwa vile tuna upungufu katika mikoa mingi ukichanganya na ukosefu kwa majirani sina uhakika tupo salama.
Kama alivosema mmoja wetu, je 'stress test' inatupa jibu gani? Tutakapobaini kuna tatizo na kuanza kusubiri meli zitoke Japan au Korea, tunaweza kupoteza watu. Na historia ni shahidi wa kweli kuwa hatujaweza kuwa tayari kukabiliana na majanga.
Kenya na Uganda mambo si mazuri, tuna uhakika tupo salama!!!! endapo tupo salama tumshukuru mwenyezi, vinginevyo tunapaswa kujiandaa.
 
Maendeleo huletwa na watu na sio serikali. Kazi ya serikali ni kusupport mazingira ya opportunities na kukusanya kodi yake. Nina shamba eka 80 kulee bonde la mto Kilombero na nina hekta 20 outside Atlanta Georgia (Powder Springs) na nalima peanuts. I divide my time both in Kilombero and Atlanta. Kuna state na federal subsidies za kwenye farming sector if you qualify, lakini haimaanishi kila mtu akae amsubiri Obama atatue matatizo yetu.
Limited government is a way of life esp. here in the US, government has to stay out of our way. Ask yourself what you can do for your country, and not what your country can do for you.
Acheni kuitegemea serikali kwa kila kitu. Kwa hiyo ningekaa bila kununua pump ya umwagiliaji kisa nangoja serikali iniletee? Again, I stand by my statement, Tanzania hakuna njaa, njaa ni ya kujitakia. Ipo mito, maziwa na ardhi tele tena yenye rutuba sana. Lakini most of it wanakaa fisi na ngedere.
Hiyo kauli ya JK may be ina ukweli. Wabongo wengi tumekuwa wavivu na ujamaa umetuharibu akili zetu hadi tumekuwa wazembe na hatuko creative. Kila kitu eti serikali ama serikali tufanyie. Yes, kuna vitu vya kufanywa na serikali but at the same time we have to play our part.
Ujamaa umetufanya tumekuwa wajinga


Ndugu yangu ni lazima niwe na wasiwasi kidogo na capacity yako katika kuangalia mambo haya; inawezekana wewe unayaangalia zaidi katika kiwango cha mfuasi badala ya kuangalia katika kiwango cha muongozaji.

Kuna mambo ambayo serikali haitakiwi iingilie maisha ya raia wake, na kuna mambo ambayo ni wajibu wa serikali kuhakikisha kuwa shughuli za raia zinakwenda sawa bila mgogoro. Shughuli za kilimo katika kila nchi iliyoendelea hapa duniani hutegemea sana serikali. Ndiyo maana nchi za Amerika ya Kusini huko zimekuwa zinalalamika sana kwenye WTO kuhusu Marekani kuwasaidia wakulima wake. Wewe kama mkulima wa hapo GA unatakiwa ujue subsidies za serikali; na kama huzijui hizo subsidies basi sijui namna ya kukueleza.

Je umeshawahi kuuliza jukumu la FEMA ni nini kama siyo kutoa misaada kwa raia kutokana na majanga ya asili?. Kwa Tanzania ukosefu wa mvua ni janga la asili ambalo serikali ina wajibu wa kuwasaidia raia. Shortcut ya kushindwa kufikiri na kudhani kuwa serikali inatakiwa isifanye lolote bali ichukue kodi na kutumbue bure bila kuwasaidiwa wananchi wake isipokuwa ya serikali kijamaa tu, ni upotofu mkubwa sana ambao tunahitaji kuufuta hasa kwa vile tumeiga mambo mengi bila kuangalia mipaka yake.

Kwa vile nitakuwa hapo Atlanta kwenye conference ya MBA wiki tatu zijazo, nitakuja hapo Powder Springs niangalie shamba lako ili tujadiliane zaidi. Nimewahi kuishi hapo Atlanta kwa muda mrefu sana nikifanya kazi pale Applied Systema Intelligence Inc kule Roswell; siyo mbali sana na hapo Powder Springs.
 
Sijui unamaanisha chama gani maana mimi si mwanachama wa CCM na wala sijawahi kuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa. Tunachokubaliana wote hapa ni kwamba tatizo la upungufu wa chakula ni la kweli na lina ukubwa wake. Serikali imekiri hilo, sanjari na kueleza mikakati ya namna ya kukabiliana na tatizo hilo, mojawapo ikiwa ni kuachia shehena kutoka SGR kwenda kwenye maeneo yenye matatizo. lakini ni lazima tukubali pia kwamba tukiachia watu waendelee na kasi hii ya kuhamisha chakula, watu hawa watamaliza hata akiba zao na baadae kulalamika na kuomba msaada. Sasa suala la serikali kununua ziada yote nalo ni gumu kwa sababu za kibajeti na za kimahitaji. Hata hivyo, wakati tunakubali kwamba hali hii ni mbaya, tusiwe na negativity iliyopitiliza kiasi cha kutoa insinuations za kwamba kutakuwa na mgawo wa chakula na pale utakapotokea basi serikali haitatenda haki!

We bana nakuona wewe kama mtu anayeshiba...suala la njaa ni kubwa mno hapa TZ....leo ni July nilikuwa koani Mara katika baadhi ya sehemu gunia la mahindi la kilo 100 linauzwa hadi shillingi 80,000, hivi ikifika Novemba hadi January hali itakuwaje? Serikali imepeleka chakula sasa wananunua gunia hilo kwa sh 40-50,000 lakini itakuwa hali ya wiki mbili hadi mwezi na mahindi yatauzwa kwa zaidi ya laki
 
Ndugu yangu ni lazima niwe na wasiwasi kidogo na capacity yako katika kuangalia mambo haya; inawezekana wewe unayaangalia zaidi katika kiwango cha mfuasi badala ya kuangalia katika kiwango cha muongozaji.

Kuna mambo ambayo serikali haitakiwi iingilie maisha ya raia wake, na kuna mambo ambayo ni wajibu wa serikali kuhakikisha kuwa shughuli za raia zinakwenda sawa bila mgogoro. Shughuli za kilimo katika kila nchi iliyoendelea hapa duniani hutegemea sana serikali. Ndiyo maana nchi za Amerika ya Kusini huko zimekuwa zinalalamika sana kwenye WTO kuhusu Marekani kuwasaidia wakulima wake. Wewe kama mkulima wa hapo GA unatakiwa ujue subsidies za serikali; na kama huzijui hizo subsidies basi sijui namna ya kukueleza.

Je umeshawahi kuuliza jukumu la FEMA ni nini kama siyo kutoa misaada kwa raia kutokana na majanga ya asili?. Kwa Tanzania ukosefu wa mvua ni janga la asili ambalo serikali ina wajibu wa kuwasaidia raia. Shortcut ya kushindwa kufikiri na kudhani kuwa serikali inatakiwa isifanye lolote bali ichukue kodi na kutumbue bure bila kuwasaidiwa wananchi wake isipokuwa ya serikali kijamaa tu, ni upotofu mkubwa sana ambao tunahitaji kuufuta hasa kwa vile tumeiga mambo mengi bila kuangalia mipaka yake.

Kwa vile nitakuwa hapo Atlanta kwenye conference ya MBA wiki tatu zijazo, nitakuja hapo Powder Springs niangalie shamba lako ili tujadiliane zaidi. Nimewahi kuishi hapo Atlanta kwa muda mrefu sana nikifanya kazi pale Applied Systema Intelligence Inc kule Roswell; siyo mbali sana na hapo Powder Springs.

Brother, you really sound like a communist/socialist while Sherrif sounds like a capitalist.
 
Brother, you really sound like a communist/socialist while Sherrif sounds like a capitalist.
Nah Raj,Sherrif fails to understand that US government is 30% of the total GDP while Tanzania govt is merely 14% of the total GDP.It.s the size of the government that shows how socialist it is,they have socialized medical care for the elderly and the needy and we don't,socialized secondary education and we dont.....socialized food assistance for the needy(food stamps) we don't.....I can go on and on.
What we fail to understand is,the government itself is a corporation and every citizen has equal shares/stocks,and the wealth of that corporation is vested in our natural resources including the people.There's nothing wrong if the government owns 50% of the total gdp(like Norway) but to people like sherrif that will be too socaialist......
 
Nah Raj,Sherrif fails to understand that US government is 30% of the total GDP while Tanzania govt is merely 14% of the total GDP.It.s the size of the government that shows how socialist it is,they have socialized medical care for the elderly and the needy and we don't,socialized secondary education and we dont.....socialized food assistance for the needy(food stamps) we don't.....I can go on and on.
What we fail to understand is,the government itself is a corporation and every citizen has equal shares/stocks,and the wealth of that corporation is vested in our natural resources including the people.There's nothing wrong if the government owns 50% of the total gdp(like Norway) but to people like sherrif that will be too socaialist......

Kobello, do you think the government of Tanzania should start serving food for wananchi?
 
Kobello, do you think the government of Tanzania should start serving food for wananchi?
Serving?....no.
According to reliefweb,400 tonnes of cereals pass through our borders daily,we had a lil over 1.1mil tonnes of food surplus last year,the SGR stands at about 200,000 tonnes of grains and the estimated shortage for 2011/12 is merely 500,000 tonnes.We have the third largest livestock herd in Africa after Sudan and Ethiopia...a better policy won't hurt!..don't you think so?
 
Sunday, July 3 2011 at 11:53

Tanzania is staring at a food crisis in the coming months as it emerges that tonnes of food are being smuggled out to drought-stricken countries in the region despite falling harvests.

Police estimate that more than 400 tonnes of maize are being trucked out of the country every day through Kilimanjaro region to Kenya, Sudan, Somalia and Ethiopia.

The Deputy Minister for Agriculture, Food Security and Co-operatives, Christopher Chiza, told The East African from Dodoma last week that hoarding and smuggling of food crops by opportunistic traders are to blame for the current high prices and shortages in the local market.

Mr Chiza said the traders are taking advantage of drought in some areas and higher prices in neighbouring countries to hoard the commodities.

"They speculate that food prices will rise even higher if the dry spell persists," he said, adding that the country has abundant food stocks due to previous bumper harvests.

To address the problem, the government plans to offload a portion of the food grains currently held by the National Food Reserve Authority, to areas facing food deficits.

The government said food demand stands at about 11.1 millions tonnes a year, whereas food harvests as of February this year stood at 12.2 million tonnes, translating to a surplus of 1.1 million tonnes.

Cereals accounted for about seven million tonnes while other crops accounted for 4.9 million metric tonnes.

Tarime and Rorya Special Police Zone Commander Constantine Massawe, speaking from Tarime last week, said they have already impounded eight trucks loaded with 56 tonnes of cereals headed for Kenya, Somalia and Sudan at Sirari border post. Mr Massawe said the trucks were seized after a tip-off by villagers.

Active cross-border trade with neighbouring countries like Burundi, Democratic Republic of Congo, Rwanda and Kenya could also cause food shortages in the region.

The government has already imposed an export ban in an effort to reduce outflows and is offloading food from the government reserves to regulate the prices. But so far, these efforts have not yielded the anticipated results.

Consumers in Kenya, Somalia and Sudan - who are facing acute food shortages - pay up to $52 (Tshs 80,000) for a 90-kg bag of maize, against $32 (Tsh50,000) that the bag fetches in Tanzania.

International humanitarians agencies say three years of below-average rainfall have led to a deterioration of pasture and particularly affected pastoralist communities in northern regions such as Arusha, Ngorongoro and Kilimanjaro.

Josette Sheeran, executive director of the World Food Programme, said the food crisis in East Africa has left an estimated 14 million people struggling to survive due to widespread poor and erratic rainfall, combined with rising food prices in Ethiopia, Kenya, Somalia and Uganda.

Ms Sheeran said hunger is looming across the Horn of Africa, threatening the lives of millions of people already facing rising food prices and internal conflict.

With the failure of the April-June long rains in some areas and below-average rainfall in others, the number of people in need of assistance is expected to rise in the coming weeks.

"It is essential that we move quickly to break the destructive cycle of drought and hunger that forces farmers to sell their produce as part of their survival strategy," Ms Sheeran said.

In Kenya, the number of people in need of food assistance is expected to rise from the current 2.4 million.

The scale of the increase, however, depends on an assessment in July.

The United Nations Office for the Co-ordination of Humanitarian Affairs said the price of grain in drought-affected areas of Kenya is 30 to 80 per cent above the five-year average, while in Ethiopia the consumer price index for food increased by almost 41 per cent last month.

Further food price hikes are expected in Ethiopia, Kenya, Uganda and Somalia, but could ease after the next harvests later this year.

Several regions in Tanzania are also facing hunger and the authorities have called for good use of the available food resources.

Agriculture and Food Security Minister Jumanne Maghembe said in Dodoma last week that about 12 of the 21 regions of the country were facing food shortage.

They are Mwanza, Shinyanga, Mara, Tanga, Kilimanjaro, Arusha and Manyara, he said.

Prof Maghembe said regions with an average mark in terms of harvests include Tabora, Dodoma, Singida, Coastal and Kagera - excluding Muleba District, where the condition is critical.

Dodoma has requested 29,222 tonnes from the Prime Minister's Office (Emergency Unit) for distribution to areas facing acute food shortage.

Chamwino District has requested 7,756 tonnes of grains for 130,200 people - including the old, orphans, widows and the disabled.

Kongwa needs 7,146 tonnes for 122,154 people; Bahi 5,715 tonnes for 97, 692 people; Kondoa 5,005 tonnes for 86,830 people; Dodoma Urban 4,226 tonnes for 72,239 people and Mpwapwa 4,008 tonnes for 69,513 people.

A Rural Vulnerability Assessment conducted in June projected that 1,253,500 people in Tanzania would face food insecurity.

Report by Mike Mande, Adam Ihucha and Leonard Magomba
 
No what's the Need of EA Community if all members depends of smuggled food from Tanzania?
 
It is a toxic combination that has stalked the continent of Africa for generations.
When a man does his worst and nature does what it does, the result is human
suffering on an unimaginable scale.
When terrible droughts are accompanied by civil war it compounds the misery for millions
of people. That is exactly what is happening in EA. Somalia is one of the worst-hit areas,
where there has been virtually no real rain for about two years.
And in this lawless, anarchic, Godforsaken, failed state there is little help for the victims. It is too dengarous
and difficult for aid agencies to operate on meaningful basis. Instead, thousands of families are forced to
walk hundreds of miles to camp in Kenya, where doctors fight to save children who arrive ill with malnutrition.
My point here is not only is Somalia failing its people it could even happen in Tanzania. Today Somalia is a haven
for Islamic terrorism which threatening the West and it is also from Somalia that the Pirate gangs ply the high sea
in our coast area, hijacking, kidnapping and killing. It is disaster zone, not a country, and once again its poor,
vulnerable and neglected people are having to pay a terrible price.
 
Tatizo la chakula Tanzania ni kama tatizo la Umeme, hatuoni ingawa macho tunayo hakuna sera ya chakula na hakuna hata anayejuwa kwanini Nyerere alijenga hayo Magara ya SGR=NFRA kwa sasa.

Tungelikuwa na sera ya chakula haya yasingelikuwepo, na wala umaskini husingekuwepo maana umaskini unahusiano mkubwa na njaa, mwenye njaa hawezi kusuka mikakati ya maana kwa ajili kujenga uchumi ataishia kufikiria mlo wa siku hiyo, sasa akifikiria mbali atafikiria mlo wa kesho; tumefanya a lot of wrong investments huku kilimo kikiachwa bila investment ya aina yoyote hile, mara ya mwisho hii nchni kufanya investments kwenye kilimo ilikuwa wakati wa Nyerere, baada ya hapo tuliamini kwenye kuvutia watu wanje waje nchni ndio kuwekeza na tulisahau kilimo moja kwa moja.

Serikali ilipaswa kuwa na sera ya chakula, ambayo inatambuwa aina kuu za vyakula vya Mtanzania ambavyo kwanza vingepata subsidise ya serikali na pia bei yake ingepangwa na serikali kuwa bei ya chini kabisa ambayo kila mtu anaweza kuimudu, vyakula hivyo vilipaswa kupewa kipambewe na kujulikana na kila mtu na kila wakati idadi yake ilipaswa kujulikana ni kiasi gani na vinalimwa na kutunzwa wapi kila mkulima anayelima hivyo vyakula alipaswa kuwa kwenye registry maalum na kujulikana, pili tumeegemea kujenga barabara za kuwasaidia Warundi, Wakongo na Zambia kupitisha magari yao na malori yao huku hatuna internal network yetu inayopita na kukusanya vyakula na mazao yote ya mkulima kwenda kwenye soko, uchumi utakuwa vipi na ajira zitaongezeka vipi? Kama tunge invest kwenye Internal Agricultural Network yetu badala ya barabara hizi zilizojengwa kwa sifa ambazo hazina faida yoyote kiuchumi tunge kuwa mbali sana, ndio maana Mawaziri wanakwambia unaweza kusafiri na tax kutoka Mtwara hadi Mwanza hii inaonyesha ambavyo hiyo ni Network ya hasara na hisiyo na faida yoyote kwa kujenga nchni yetu na kuweka usalama wa chakula nchni, siku zote huwezi kuwasikia wakikwambia jinsi gani hiyo network inaweza kukusanya malighafi za mkulima watakwambi unaweza kusafiri na tax kutoka Mtwara hadi Mwanza? starehe ya ajabu sana hiyo.

Hakuna nchni iliyowai kuendelea bila mipango, sisi hatuna mipango yoyote, hizo SGR zilijengwa na Mwalimu kimkakati lakini hawa jamaa hawajui na ndio maana wameshindwa kuzitumia, 2005/2006 serikali ilikuwa inazitumia kwa ajili ya kuweka vyakula vya misaada kwa ajili ya kugawia watu, na sasa ndivyo wanavyofanya; kama tungekuwa na watu wenye akili timamu SGR zingetumika kama zonal food security markets, ambapo serikali ingelikuwa inanunua vyakula vya mkulima kwa bei ya juu na kutunza, kwahiyo kila mkulima angeliwa anakimbiza chakula chake kuuza SGR, na tungefanya invest ya barabara kimkakati kutoka kwenye mashamba na vijiji vinavyozalisha kuelekea kwenye SGR ya karibu, ila wameachia wakina MO wanasomba vyakula kila kona kwa bei chee ya kulalia wakulima kitu kinachoperekea wakulima wa mipakani kuuza vyakula nje ya nchni na pale wapokatazwa inakuwa ni kuwaonea kwasababu hakuna bei ndani ya nchni.

Sehemu kubwa ya Mazao ya Rukwa yauzwa Kongo na Zambia na wale Tarime wanauza Kenya. MO anakusanya hasa hapa Central zone kwa bei nafuu ya kulalia wakulima anatunza alafu wakati wa njaa anauzia serikali kwa bei juu, na pale hasipo wauzia wanapeana vibali vya uongo kuwa ameagazi chakula nje kumbe ni hivi vya ndani alivyotunza ili apate nafasi ya nafuu ya kodi na kupata Dollar kwa njia za uongo.
 
....Tunajua pia kwamba SGR ina chakula cha kutosha na sasa kinatolewa kupunguza nakisi katika maeneo ambayo hayakuwa na mavuno mazuri. ...

Unaposema kuwa SGR inachakula cha kutosha, na wakati huo huo Serikali inazuia wananchi wasiuze chakula nje ya nchi kwa sababu kunaupungufu wa chakula mie sikuelewi!!!
Serikali inunue chakula hicho kwa wakulima katika marketi price na iweke kwenye Maghala yake (SGR's) ila inapoendelea kuwabana wananchi wasiuze na wabaki na chakula kikiliwa na DUMUZI ili hali wao wanashida na pesa kwa ajili ya kupeleka watoto wao shule na fedha kwa ajili ya matibabu.
Hali inayotokea sasa hivi kwa Serikali kuzuia wananchi wasiuze Chakula nje ya nchi ni uonevu mkubwa na kutia shaka ya kuwa Serikali haina fedha za kununua chakula hicho kwenye maghala yake!. Tusiwe viziwi na watu wasiosikia la mkuu, tusome alama za nyakati, na turuhusu soko huru lifanye kazi, kama tunashindwa sie kununua.

Suruhisho la hili si kuzuia wananchi wasiuze Chakula nje ya nchi, ila ni kuhimiza na kuwajengea uwezo wananchi na makampuni ya ndani au nje yawekeze kwenye kilimo cha vyakula na si kuhimiza kilimo cha BIOFUEL au kutoa ardhi kwa ajili ya kilimo cha BIOFUEL, hii haina manufaa kwetu inamanufaa kwao hao wanaojiita matajiri wa Dunia hii.
 
Ulitakiwa ujue kuwa Tanzania ni nchi iliyojengwa kwa msingi wa kutegemea huruma ya mungu kuleta mvua. Mgao wa umeme leo unaupta kutokana na kukosekana kwa mvua ya kutosha. Kilimo cha Tanzania pia kinategemea mvua. Sasa kama hakuna mvua, na nchi yetu haina utaratibu wa kutunza nafaka, huwezi kumalumu mkulima huko kijijini kuwa kwa nini hakutunza nafaka za mwaka jana ili zimsaidie mwaka huu. Madai ya mito na maziwa kuwapo nisimplistic sana kwa sababu mtu wa Dodoma hawezi kulima kwa kutegema maji ya mto au ziwa lolote. Hakuna infrasrutcture yoyote ya irrigation. Na kwa taarifa yako, hata kwenye nchi zinazotumia irrigation, bado huwa wakulima wanalalamika iwapo kutakuwa na kiangazi kikubwa sana kwa sababu maji yote wanayomwagilia mashambani yatakuwa yanayeyushwa na jua.


Katika dunia ya kisasa, majanga ya kiasili yanasimamiwa na serikali, na ukosefu wa mvua ni mojawapo ya majanga ya kiasili ikiwa ni pamoja na vumbunga na kunyesha kwa mvua nyingi za kusababisha mafuriko.

La kushangaza, utaiona serikali yako inatoa pesa za kufidia wafanyabisahara eti "bail out" kutokana na mtikisiko wa mfumo wa fedha duniani, lakini serikali hiyo hiyo haina akiba ya kukabililina na mtikisiko wa asili, kama ukosefu wa mvua na mafuriko.

Umenena. Inatia aibu na simanzi kwa kweli kwa jinsi Serikali isivyokubali kuwekeza kwa kiwango kikubwa na cha kutia moyo katika miundombinu ya kilimo cha umwagiliaji na Matrekta pamoja na majembe ya kulimia kwa kutumia Wanyama-kazi. Kwa kutumia hiyo bailout ya zaidi ya shilingi bilioni 1,700 tungeweza kama taifa kununua matrekta zaidi ya 48,571 kwa fedha taslimu. kama tungetumia njia ya kulipa kwa awamu ya asilimia 20 kila mwaka tungepata zaidi ya matrekta 242,871 yakiwa na vifaa vyote. Hebu fikirieni impact kwenye uchumi ingekuwaji. Ni wakati wa Mwalimu ndipo nchi yetu iliweza kuwa na matrekata mengi kwa ajili ya kilimo. yalifikia zaidi ya 17,000 miaka ya sabini. Kwa sasa idadi ya matrekta yote nchini ni kama 9860. 1860 ni mapya na asilimia 85 ya yaliyobaki umri wake ni zaidi ya miaka 10. Hayo 1860 ambayo ni mapya yamepatikana kwa njia ya mkopo toka Serikali ya India. Pia kwa fedha hizo (shilingi bilioni 1,700 za bailout kwa kulipa kwa fedha taslimu tungeweza kununua magari makubwa zaidi ya 6,800 kwa ajili ya kuchimba visima kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji na matumizi katika kaya zetu.

-----------------------------HIYO NDIYO TANZANIA NA UONGOZI WAKE--------------------------------------
 
Tatizo la chakula Tanzania ni kama tatizo la Umeme, hatuoni ingawa macho tunayo hakuna sera ya chakula na hakuna hata anayejuwa kwanini Nyerere alijenga hayo Magara ya SGR=NFRA kwa sasa.

Tungelikuwa na sera ya chakula haya yasingelikuwepo, na wala umaskini husingekuwepo maana umaskini unahusiano mkubwa na njaa, mwenye njaa hawezi kusuka mikakati ya maana kwa ajili kujenga uchumi ataishia kufikiria mlo wa siku hiyo, sasa akifikiria mbali atafikiria mlo wa kesho; tumefanya a lot of wrong investments huku kilimo kikiachwa bila investment ya aina yoyote hile, mara ya mwisho hii nchni kufanya investments kwenye kilimo ilikuwa wakati wa Nyerere, baada ya hapo tuliamini kwenye kuvutia watu wanje waje nchni ndio kuwekeza na tulisahau kilimo moja kwa moja.

Serikali ilipaswa kuwa na sera ya chakula, ambayo inatambuwa aina kuu za vyakula vya Mtanzania ambavyo kwanza vingepata subsidise ya serikali na pia bei yake ingepangwa na serikali kuwa bei ya chini kabisa ambayo kila mtu anaweza kuimudu, vyakula hivyo vilipaswa kupewa kipambewe na kujulikana na kila mtu na kila wakati idadi yake ilipaswa kujulikana ni kiasi gani na vinalimwa na kutunzwa wapi kila mkulima anayelima hivyo vyakula alipaswa kuwa kwenye registry maalum na kujulikana, pili tumeegemea kujenga barabara za kuwasaidia Warundi, Wakongo na Zambia kupitisha magari yao na malori yao huku hatuna internal network yetu inayopita na kukusanya vyakula na mazao yote ya mkulima kwenda kwenye soko, uchumi utakuwa vipi na ajira zitaongezeka vipi? Kama tunge invest kwenye Internal Agricultural Network yetu badala ya barabara hizi zilizojengwa kwa sifa ambazo hazina faida yoyote kiuchumi tunge kuwa mbali sana, ndio maana Mawaziri wanakwambia unaweza kusafiri na tax kutoka Mtwara hadi Mwanza hii inaonyesha ambavyo hiyo ni Network ya hasara na hisiyo na faida yoyote kwa kujenga nchni yetu na kuweka usalama wa chakula nchni, siku zote huwezi kuwasikia wakikwambia jinsi gani hiyo network inaweza kukusanya malighafi za mkulima watakwambi unaweza kusafiri na tax kutoka Mtwara hadi Mwanza? starehe ya ajabu sana hiyo.

Hakuna nchni iliyowai kuendelea bila mipango, sisi hatuna mipango yoyote, hizo SGR zilijengwa na Mwalimu kimkakati lakini hawa jamaa hawajui na ndio maana wameshindwa kuzitumia, 2005/2006 serikali ilikuwa inazitumia kwa ajili ya kuweka vyakula vya misaada kwa ajili ya kugawia watu, na sasa ndivyo wanavyofanya; kama tungekuwa na watu wenye akili timamu SGR zingetumika kama zonal food security markets, ambapo serikali ingelikuwa inanunua vyakula vya mkulima kwa bei ya juu na kutunza, kwahiyo kila mkulima angeliwa anakimbiza chakula chake kuuza SGR, na tungefanya invest ya barabara kimkakati kutoka kwenye mashamba na vijiji vinavyozalisha kuelekea kwenye SGR ya karibu, ila wameachia wakina MO wanasomba vyakula kila kona kwa bei chee ya kulalia wakulima kitu kinachoperekea wakulima wa mipakani kuuza vyakula nje ya nchni na pale wapokatazwa inakuwa ni kuwaonea kwasababu hakuna bei ndani ya nchni.

Sehemu kubwa ya Mazao ya Rukwa yauzwa Kongo na Zambia na wale Tarime wanauza Kenya. MO anakusanya hasa hapa Central zone kwa bei nafuu ya kulalia wakulima anatunza alafu wakati wa njaa anauzia serikali kwa bei juu, na pale hasipo wauzia wanapeana vibali vya uongo kuwa ameagazi chakula nje kumbe ni hivi vya ndani alivyotunza ili apate nafasi ya nafuu ya kodi na kupata Dollar kwa njia za uongo.

kAMA HAWATAKUSIKIA NA KUKUELEWA LITAKUWA JAMBO LA KUSHANGAZA SANA.
 
nah raj,sherrif fails to understand that us government is 30% of the total gdp while tanzania govt is merely 14% of the total gdp.it.s the size of the government that shows how socialist it is,they have socialized medical care for the elderly and the needy and we don't,socialized secondary education and we dont.....socialized food assistance for the needy(food stamps) we don't.....i can go on and on.
What we fail to understand is,the government itself is a corporation and every citizen has equal shares/stocks,and the wealth of that corporation is vested in our natural resources including the people.there's nothing wrong if the government owns 50% of the total gdp(like norway) but to people like sherrif that will be too socaialist......

i salute you
 
Mzee Mwanakijiji;2200859]Robo tatu ya Tanzania inakabiliwa na upungufu mkubwa wa chakula. Kuna watu wanakabiliwa na njaa katika nusu ya wilaya zote nchini na hali haionekani kutengemaa sasa hivi. Serikali inajitahidi kuhamisha nafaka kutoka sehemu mbalimbali zenye chakula kupeleka kwenye sehemu zenye upungufu wa chakula. Kwenye soko la dunia nchi nyingi zaidi zinazidi kugombea chakula kidogo kilichopo na kama kawaida mataifa makubwa yatakuwa na uwezo wa kupata vyakula vingi kuliko nchi maskini.Kwa vile chakula ni limited resources ni wazi kuwa itahitajika uamuzi wa makusudi wa kuanza kufikiria jinsi ya kuration chakula aidha kwa mikoa, wilaya na hata kwa kaya.Nimekuwa nikifuatilia suala hili kwa miaka mitatu na naweza kusema kwa uhakika mkubwa tu, hakuna kitu kinachoweza kusababisha migongano ya kisiasa na kijamii kama hili suala la chakula. nawaza tu
Mbopo;2201131]Suala lako ni hypothetical na unajiuliza kama kweli ulifanya uchunguzi huo kweli au ulitaka tu kutimiza wajibu wako wa kila siku wa kumsifia Mwalimu na wakati huo huo kuendeleza programu yako ya chuku dhidi ya mtawala wa leo. Hali unayozungumzia wewe si ya Tanzania (labda kwa sababu mwenzetu uko nje) ya leo. Sasa kujaribu kuonyesha kwamba 70% ya watanzania wanakabiliwa na njaa ni upotoshaji wa hali ya juu na hata inakinzana na maelezo yako mwenyewe kwa kusema kwamba nusu ya wilaya zote zinakabiliwa na njaa. That is not 70%
Chapakazi;2201552]hehehehe! Habari uliyoandika na iliyoandikwa kwenye magazeti ni tofauti kabisa!! Sijui data zako umezitoa wapi...
Mzee Mwanakijiji;2204466]Nyie subirini tu.. watu watasema ooh mnaombea mambo mabaya yatokee n.k ili mpate cha kusema; kweli kabisa watu wakianza kupata shida kweli ya chakula hatutaki watu kuanza kusema "hatukujua", "hali ya chakula duniani iko nje ya uwezo wetu"
FaizaFoxy;2204560] Easy to terrorize an entire country with few sentences of hungerThis now is the dirtiest trick ever from failures
Tuwe waangalifu na chakula chetu
Mwandishi Wetu
27 Jul 2011
WAZIRI wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Profesa Jumanne Maghembe amesema ya kuwa tathmini ya awali ya upatikanaji wa chakula nchini imeonyesha kuna upungufu katika wilaya 56 na hali hiyo imesababisha bei ya nafaka kupanda bei.
Kwa mujibu wa Profesa Maghembe, wilaya hizo ni Bariadi, Kishapu, Meatu, Maswa, Kahama, Shinyanga Mjini, Vijijini, Bukombe, Karatu, Monduli, Meru, Ngorongoro, Longido, Arusha Mjini na Arusha Vijijini, Magu, Kwimba, Misungwi, Ilemela, Nyagana, Ukerewe, Mwanga, Moshi, Siha na Bombo Nyingine ni Same, Mbulu Simanjiro, Babati, Kiteto, Bunda, Rorya, Musoma mjini na Musoma Vijijini. Pia, Nzega, Igunga, Tabora, Uyui, Temeke, Ilala, Kinondoni, Manyoni, Iramba, Singida, Mafia, Rufiji, Dodoma, Bahi, Iringa Vijijini, Iringa Mjini, Muleba, Chato, Chunya, Mbarali, Masasi na Mkinga.

Wilaya hizi ni nyingi mno na ni kielelezo tosha ni kwa nini bei ya vyakula iko juu akribu nchi nzima, hali inayofanya maisha ya Mtanzania wa kawaida kuwa ngumu kwani chakula, tofauti na bidhaa nyingine, ni kitu cha lazima kwa kila binadamu. Limekuwa jambo jema kwamba waziri ametoboa ukweli wa mambo kwani ilianza kujengeka dhana kwamba tuko salama kwa upande wa chakula kasi cha ‘ziada' kutoroshwa nje na hasa aktika nchi jirani ya Kenya kwa magendo.

Kana kwamba hiyo haitoshi, majuzi tu tulishuhudia wakuu wa wilaya za Kenya zinazopakana na Tanzania upande wa kaskazini mashariki wakikutana na wenzao wa wa wilaya hizo kuomba rasmi kununua chakula, bila shaka baada ya kuamini kwamba hali yetu ya chakula ni nzuri. Wakuu wa wilaya za mikoa ya Arusha na Kilimanjaro hawakuwakatalia wenzao kununua chakula kutoka kwao ila waliwaambia kwamba watapeleka ombi lao serikali kuu ili liweze kufikiriwa. Hayakuwa majibu mabaya, lakini, dhana iliyojengeka ni kwamba chakula cha kuwauzia wakenya hao kipo.
Lakini sasa tunapata picha nyingine kwamba hatuna sababu yoyote ya kuuza chakula chetu nje kwani wenyewe hakitutoshelezi. Tunatarajia kuvuna tani 6,786,600 wakati mahataji ni tani 7,200,340, hivyo kuwa na upungufu wa tani 413,740 kitaifa.

Ni matumaini yetu kwamba sasa, baada ya kuifahamu hali halisi ilivyo, chakula tulichonacho tutakitumia si vizuri tu bali hata kwa uangalifu yasitukute ya mwaka 1974, tulipolazimika kula hadi unga wa njano kutoka Marekani baada ya kukumbwa na baa la njaa.
 
Back
Top Bottom