ksny
JF-Expert Member
- Mar 30, 2016
- 1,692
- 1,657
ote ni mashuhuda wa mambo ya hovyo yanayofanywa na baadhi ya Watanzania wenzetu waliojipa hadhi ya Ukimbizi hewa ughaibuni.Wote ni mashuhuda wa mambo ya hovyo yanayofanywa na baadhi ya Watanzania wenzetu waliojipa hadhi ya Ukimbizi hewa ughaibuni.
Kiuhalisia hawa siyo wakimbizi bali ni wahalifu walioamua kukimbia mkono wa Sheria kama walivyo wahalifu wengine.
Wahalifu hawa wakiongozwa na Vinara Wakuu Ansbert Ngurumo, Tundu Lissu ,& Godbless Lema wameichafua nchi yetu kupitia mitandao ya Kijamii, kufanya ziara kwa Nchi Wahisani, kutembelea ofisi za Mashirika au Taasisi kubwa za Kimataifa n.k
Huko kote wanapeleka taarifa za uongo, uzushi & kupotosha kuhusu yale yanayofanywa na Serikali ya Tanzania
Wahalifu hawa waliokosa Uzalendo na kuongozwa na maslahi binafsi wamefikia hatua ya kumtukana, kumkashifu na kumbeza Rais wetu mpendwa Mhesh Dkt John Pombe Magufuli.
Niombe Serikali ya Tanzania ianzishe mchakato wa kupata hati maalumu (International arrest warrant) kwa kushirikiana na Polisi wa Kimataifa - Interpol ili wahalifu hawa wakamatwe, kurejeshwa nchini na kushtakiwa mujibu wa sheria.
Waziri wa Mambo ya Nje & Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba Kabudi, imetosha!
Hkuna sababu ya kukaa kimya huku taswira ya nchi yetu na Rais mpendwa ikichafuliwa machoni pa Jumuiya ya Kimataifa.
Viva Tanzania
Viva Rais Dkt John Magufuli
Kiuhalisia hawa siyo wakimbizi bali ni wahalifu walioamua kukimbia mkono wa Sheria kama walivyo wahalifu wengine.
Wahalifu hawa wakiongozwa na Vinara Wakuu Ansbert Ngurumo, Tundu Lissu ,& Godbless Lema wameichafua nchi yetu kupitia mitandao ya Kijamii, kufanya ziara kwa Nchi Wahisani, kutembelea ofisi za Mashirika au Taasisi kubwa za Kimataifa n.k
Huko kote wanapeleka taarifa za uongo, uzushi & kupotosha kuhusu yale yanayofanywa na Serikali ya Tanzania
Wahalifu hawa waliokosa Uzalendo na kuongozwa na maslahi binafsi wamefikia hatua ya kumtukana, kumkashifu na kumbeza Rais wetu mpendwa Mhesh Dkt John Pombe Magufuli.
Niombe Serikali ya Tanzania ianzishe mchakato wa kupata hati maalumu (International arrest warrant) kwa kushirikiana na Polisi wa Kimataifa - Interpol ili wahalifu hawa wakamatwe, kurejeshwa nchini na kushtakiwa mujibu wa sheria.
Waziri wa Mambo ya Nje & Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba Kabudi, imetosha!
Hkuna sababu ya kukaa kimya huku taswira ya nchi yetu na Rais mpendwa ikichafuliwa machoni pa Jumuiya ya Kimataifa.
Viva Tanzania
Viva Rais Dkt John Magufuli
Mimi ninafikiri itafika mahali tuache kuwa wafuasi vipofu na wasiokuwa na uwezo wa kufikiri na kuchambua. Tanzania ni kubwa kuliko Lisu na hao waliyo tajwa. Tanzania ni kubwa kuliko Magufuli. Lakini kitendo cha kutaka kumkamata kila mbaye hakubaliani na wengi, au hakubaliani na Magufuli tutajaza magereza yetu. Kama mtu anaeneza uongo huko nje, kwa nini tuhangaike naye. Nchi haiwezi kuchafuliwa na watu watatu/wachacha kwa uongo usio wa msingi. Wengi tunajuwa hao waliyotajwa siyo wakimbizi wa siasa bali ni wakosa ajira za kisiasa.
Mimi sioni sababu ya kuwakamata. Kila mtu ana uhuru wa kujiita mimbizi, na kama atapewa ukimbizi wa siasa basi muiache akae huko alikochagua. Mimi nimewa kuitwa kutafsiri kwenye maombi ya mkimbizi wa siasa msichana wa Kisukuma. Yeye anadai aliikimbia TZ kwa kulazimishwa kukeketwa na wazazi wake. Huyu alipewa ukimbizi. Kazi yangu ilikuwa kutafsiri/ukalimani. Nilitafsiri nikamaliza na kulipwa. Ila kweli sababu aliyotoa kuomba ukimbizi ilikuwa ya uongo kwa sababu Wasukuma hawakeketi.
Kwa hiyo hao waliyokimbia, ni lazima wajitahidi kuipaka matope TZ ili waweze kukubaliwa kupata ukimbizi na hatimaye wa nchi husika. Watu kama ho huitwa wakimbizi wa kuchumi na siyo kisiasa. Ndiyo maana wakisha pata ukimbiza huomba uraia na kuendelea kuishi huko. Mimi sipingani nao kuhusu kuomba ukimbizi maana sasa kilichobaki ni hicho. CHADEMA haina uwezo wa kuwalipa. Kazi hawana au hawataki kutafuta. Itakuwa rahisi kukimbilia nje na kuanza kuishi maisha ya "saidia masikini", lakini nje hiyo sharti iwe Ulaya, Marekani, Canada, Australia, New Zealand au Scandinavia. Kwa nini siyo Rwanda, Burundi, au Congo. Mbona wakimbizi wa siasa toka hizo nchi wamejaa kwetu. mbona hata Kenya kinakuwa kituo cha kupitia tu.