fimboyaasali
JF-Expert Member
- Jan 14, 2011
- 8,409
- 7,962
Unajua hayo ni mawazo ya kijinga kabisa,kumbuka wlimu ni haki ya binadamu huwezi kumnyima kwa ajiki ya mimbaSERIKALI IACHE MZAHA; KURUHUSU WATOTO WALIOPEWA MIMBA KURUDI SHULENI KUSOMA NI ANGUKO LA TAIFA LA KESHO.
Anaandika Robert Heriel.
Naiomba serikali, viongozi wakubwa msikie Jambo hili, tena msifanye mzaha. Huruma huruma za ajabu ajabu katika baadhi ya ishu ni hatari Kwa ustawi wa taifa.
Nafahamu wapo watu wenye roho laini, wenye huruma, lakini siku zote huruma ikizidi huleta Matatizo.
Kuruhusu watoto wakike waliopata mimba kuendelea na shule kimantiki ni Kuruhusu watoto wakike wapewe MIMBA. Yaani mi Kuruhusu mimba mashuleni Kwa lugha ya kawaida.
Nyakati za Magufuli, moja ya mambo niliungana naye ni pamoja na hili. Hatuwezi kuwa wapole na wenye huruma katika masuala haya ya Msingi.
Nani asiyejua nchi yetu ni masikini, Nani asiyejua familia zetu nyingi ni familia zilizozidiwa na ufukara. Kuzaa kunahitaji maandalizi, kuzaa kunahitaji mipango, kunahitaji wazazi wawili wenye akili iliyokomaa. Kuruhusu watoto waliopewa ujauzito waendelee na shule ni kuongeza matatizo ya kimaadili na kiuchumi.
Niliwahi kuandika kuwa serikali Kwa sehemu kubwa inachangia kumomonyoko Kwa maadili ya jamii.
Unamsomesha aliyepata mimba shuleni na wakati huo huo unamfunga miaka 30 aliyembebesha mimba huyo binti, hiyo ni Akili kweli, embu tutafakari. Kama tumeamua kuwapa watu adhabu acheni wapewe adhabu.
Huyu apoteze haki ya kusoma Kwa kukubali kudanganywa akapewa mimba, huyu mwingine afungwe Kwa kushindwa kujizuia hisia zake na kumpa mimba mtoto wa kike.
Mtoto yeyote aliyebalehe mwenye uwezo wa kubeba mimba ni Mkubwa, na anavigezo vyote vya kuitwa mama ndio maana akabeba mimba.
Kuhusu suala la akili ni ishu nyingine kabisa Kwa maana wapo watu wazima kiumri lakini hawana akili za kikubwa, na wapo watu wenye umri Kati ya 15-18 ambao wanaakili za kikubwa. Hivyo logically hatuwezi kusema Umri ni Akili au akili ni Umri ikiwa wapo wenye umri mkubwa wanazidiwa akili na wenye umri mdogo.
Kuruhusu wanafunzi waliopewa mimba wasome ni kuidhinisha zinaa ndani ya nchi. Ni kuitangazia dunia kuwa nchi yetu inaruhusu zinaa. Hapatakuwa na hofu yoyote Kwa mabinti kushiriki tendo la ndoa.
Serikali na watu wote tutambue kuwa moja ya mambo yanayowatisha mabinti wa kike wasifanye zinaa ni Kama ifuatavyo;
1. Kasumba ya kuumia wakati WA kutolewa Bikra.( Hii ni Kwa ambao hawajawahi kufanya kabisa).
2. Aibu ya maumbile. Wasichana kuogopa kuonekana nyuchi na maungo Yao ya Siri kwani wanahofia Kuambiwa wanamaumbile mabaya.
3. Kupata MIMBA
Mabinti wengi huogopa zaidi mimba kuliko magonjwa ya zinaa.
4. Kupata magonjwa ya zinaa Kama UKIMWI
Japo hii sio Sana lakini ni moja ya sababu kuu nne zinazowafanya mabinti waogope kuingia kwenye tendo la ndoa.
5. Maadili ya Dini na wazazi
Wapo watoto waliolelewa wakaleleka. Hawa huogopa kujiingiza kwenye tendo la ndoa mapema Kwa sababu ya Mafunzo waliyopewa. Hawa ni wachache.
Sababu namba tatu ambayo ni kupata mimba ni sababu nyeti mno ambayo mabinti huogopa kufanya ngono hovyo hovyo. Hii ni kutokana na kuwa mimba huwafanya wafukuzwe shule, lakini la pili mimba ni aibu kwao wenyewe na wazazi wao. Mimba huwaumbua kwa Yale waliyofanyia gizani sasa hutokea hadharani Kwa tumbo kuvimba.
Kuruhusu mimba shuleni ni Kuruhusu watoto wasio na Baba.
Kuruhusu Mimba shuleni ni Kuruhusu watoto wa mitaani kwani familia nyingi za kibongo ni Masikini.
Kuruhusu Mimba shuleni ni Kuruhusu ongezeko la single Mama hapo Baadaye ambalo kimsingi linaathari hata hivi sasa.
Kuruhusu Mimba shuleni ni Kuruhusu taifa kuelemewa na Kundi tegemezi ambalo halilisaidii TAIFA.
Kuruhusu Mimba shuleni kutaathiri maadili ya watoto kwenye malezi kwani wamama wazazi watakuwa shuleni wakisoma wakati Mtoto akiachwa Kwa mfanyakazi wa ndani, sasa jiulize ni familia ngapi zinauwezo WA kuajiri mfanyakazi wa ndani.
Kuruhusu Mimba shuleni ni kuhujumu nguvu kazi ya nchi; kwani Mwanaume atafungwa, mama atarudi shule, Bibi naye Kwa vile bado ni kijana afanyaye kazi labda ni kilimo au ujasiriamali au kazi za ualimu, uhasibu n.k watabidi waache kazi zao wadili na mtoto au waajirifanyakazi WA ndani ili wamlipe Mshahara Mdogo usiozidi 50,000 ambao pia ni uhujumu uchumi.
Serikali iache zile sheria za shule Kama zilivyo.
Atakayempa mimba mwanafunzi apate miaka yake 30 jela, na mwanafunzi afukuzwe shule. Kumbuka nimesema hakuna mtoto anayebeba Mimba.
Mtu au kiumbe chochote chenye uwezo wa kubeba mimba ujue kimekomaa, imefikisha umri wa kuitwa Mkubwa.
Kwenye nature au asili, kubeba mimba au kutungisha mimba ni moja ya ishara ya ukubwa.
Serikali na wazazi tusiendekeze mambo haya. Nafahamu Sisi sote tuwazazi, wanaopata mimba ni binti zetu, dada zetu, watoto wetu n.k lakini lazima tuwe wakali katika hili.
Mtoto aambiwe angali mdogo, ukipata mimba shule unafukuzwa, nyumbani unafukuzwa, yaani mtoto akijua Jambo hilo hawezi pata mimba ninauhakika. Hofu ndiyo ilifanya kizazi kilichopita kubaki na maadili.
Familia zinazoendekeza watoto ndizo hupata madhara ya watoto kupatwa na mimba wakiwa shuleni, kuwa mashoga, kuvuta bango na kutumia madawa ya kulevya.
Nafahamu kuna Exceptional katika mambo mengi, hivyo hata katika Jambo hili wapo wanaopatwa na madhara Kwa bahati mbaya tuu Kama kubakwa Kwa lazima, kulazimishwa kunywa madawa ya kulevya, kulawitiwa n.k. lakini kundi hili wapo wachache mno,
Wengi Hufanya Kwa hiyari Yao wenyewe.
Serikali nafahamu inaweza ikawa inahitaji pesa Fulani kutoka nchi za nje, ikiwa ni hivyo nasi itumie Siasa katika Jambo hili. Kwenye media iwe mataifa wanajua kuwa tunaruhusu wanafunzi waliopewa mimba kuendelea kusoma lakini kiuhalisia hakuna kitu Kama hicho.
Kalagabaho!
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa OSTERBAY, DAR ES SALAAM
Sent from my SM-N960F using JamiiForums mobile app