Serikali iache kufungia vyuo vikuu binafsi kwa ukosefu wa wahadhiri. Yenyewe ndio iwapeleke na iwalipe mishahara

YEHODAYA

JF-Expert Member
Aug 9, 2015
36,911
51,889
Dini zimekuwa zikijitahidi Sana kuwekeza kwenye miundombinu na majengo ya vyuo vikuu Tanzania kwa kupitia wafadhili wao wa ndani nje ya nchi ambao Mara nyingi wakishamaliza huwa hawaendelei kuchangia gharama za uendeshaji.

Dini Kama Waislamu,wakatoliki,walutheri, waanglikana na wasabato na moravian Wana vyuo vikuu vizuri vyenye miundombinu mizuri sana lakini hupata taabu kuajiriwa wahadhiri na maprofesa mahiri kutokana na uwezo mdogo wa kifedha.

Ushauri wangu kwa serikali badala ya kufungia hivyo vyuo kwa kukosa wahadhiri wenye sifa serikali iwe inatoa wahadhiri na maprofesa na kuwapeleka kwenye hivyo vyuo kwa ajira ya kudumu .Hizo dini zimeshatoa mchango wake kwa kujenga miundo mbinu serikali nayo ichangie nguvu kazi hasa upande wa wahadhiri na maprofesa iajiri na iwapeleke kwenye hivyo vyuo.

Idadi ya wanaomaliza kidato Cha sita ni wengi kuliko uwezo wa vyuo vichache vilivyopo vyenye sifa.Sioni kwa Nini chuo kifungiwe kuendesha kozi kisa eti hakina wahadhiri wenye sifa na serikali ipo Kodi zipo iajiri wahadhiri ipeleke vyuo viendelee kudahili wanachuo.

Dini Zina mchango mkubwa kwa jamii kwa upande wa vyuo vikuu na serikali nayo inatakiwa kuwa na mchango mkubwa kwa jamii kwenye vyuo kwa kutoa wahadhiri na maprofesa
 
Kwenye suala la elimu lazima viwango vya ubora vidhibitiwe. Elimu ndio msingi mkuu wa maendeleo. Kule capetown univeraity kuna bango linasema if you want to destroy a nation, no need of long range missiles or nuclear bombs, you only compromise the education system.

Taasisi za dini zinafanya vizuri kuisaidia serikali kuanzisha au kutoa hiduma za kijamii ila hapa kati zikaingiwa na tamaa ya kupata faida kubwa zikaanzisha tu vyuo visivyo na sifa ya vyuo vikuu na wakaviita vyuo vikuu. Mfano kile st. Augustine cha songea, hata hadhi ya sekondari ya kata hakikufikia ila kikaitwa chuo kikuu.

Wajitahidi kama vile wanavyofanya ngazi ya sekondari wafanye hivyo hata ngazi ya chuo. Waajiri waalimu, walipe mishahara mizuri na kwa wakati watu watajazana huko.

Sioni kosa la serikali hapo, serikali kazi yake ni ku-maintain standards, kama hujafikia lazima wakufungie.
 
Kwenye suala la elimu lazima viwango vya ubora vidhibitiwe. Elimu ndio msingi mkuu wa maendeleo. Kule capetown univeraity kuna bango linasema if you want to destroy a nation, no need of long range missiles or nuclear bombs, you only compromise the education system.

Taasisi za dini zinafanya vizuri kuisaidia serikali kuanzisha au kutoa hiduma za kijamii ila hapa kati zikaingiwa na tamaa ya kupata faida kubwa zikaanzisha tu vyuo visivyo na sifa ya vyuo vikuu na wakaviita vyuo vikuu. Mfano kile st. Augustine cha songea, hata hadhi ya sekondari ya kata hakikufikia ila kikaitwa chuo kikuu.

Wajitahidi kama vile wanavyofanya ngazi ya sekondari wafanye hivyo hata ngazi ya chuo. Waajiri waalimu, walipe mishahara mizuri na kwa wakati watu watajazana huko.

Sioni kosa la serikali hapo, serikali kazi yake ni ku-maintain standards, kama hujafikia lazima wakufungie.
📌
 

UBIA INAWEZEKANA.

Tanzania tunayo sheria inayoweka mazingira na kuwezesha ubia kati ya Serikali na sekta binafsi. Sheria hiyo ni The Public-Private Partnership Act, 2010 kama ilivyorekebishwa mwaka 2018.

Mashirika ya Dini yaangalie uwezekano wa kufanya makubaliano na Serikali chini ya Sheria hiyo ili kumiliki na kuendesha vyuo vikuu hivyo kwa njia ya ubia (PPP).
 
Kile chuo ni hovyo mkuu
Kwenye suala la elimu lazima viwango vya ubora vidhibitiwe. Elimu ndio msingi mkuu wa maendeleo. Kule capetown univeraity kuna bango linasema if you want to destroy a nation, no need of long range missiles or nuclear bombs, you only compromise the education system.

Taasisi za dini zinafanya vizuri kuisaidia serikali kuanzisha au kutoa hiduma za kijamii ila hapa kati zikaingiwa na tamaa ya kupata faida kubwa zikaanzisha tu vyuo visivyo na sifa ya vyuo vikuu na wakaviita vyuo vikuu. Mfano kile st. Augustine cha songea, hata hadhi ya sekondari ya kata hakikufikia ila kikaitwa chuo kikuu.

Wajitahidi kama vile wanavyofanya ngazi ya sekondari wafanye hivyo hata ngazi ya chuo. Waajiri waalimu, walipe mishahara mizuri na kwa wakati watu watajazana huko.

Sioni kosa la serikali hapo, serikali kazi yake ni ku-maintain standards, kama hujafikia lazima wakufungie.
 
Vyuo vikuu viendane na ajira ili wanaomaliza wapate matunda ya elimu yao...sio mtu anasoma then ajira hakuna anashinda mitaani mpaka aaliyosomra anasahau..
Now institution nyingi zinaajiri certificate na diploma so degree nyingi zinazagaa mtaani maana mashirika hayana pesa za kuwalipa
 
Itakuwa ni visasi tu, baada ya kuona hawalambwi tena miguu, si unajua hii serikali ni ya visasi.
Upo sahizi,ndicho kinachoigharimu St.Fransis Ifakara.kisa ni Mbunge alitaka kupigwa na polisi akakimbilia kujiokoa kwenye majengo ya kanisa,toka hapo mpaka Leo ni visasi kwenda Mbele
 
Mkuu mngemwambia huyo 'bwana' wenu ambaye mnamsifia ndio kakazana kuwateua kwenye nafasi za kisiasa ambapo huko nako wamegeuka vituko kwa kutetea upuuzi. Na ungeenda mbali kidogo kutazama na vyuo vya serikali,kwa kasi hii ya uteuzi wataanza kuvifungia na vya serikali kwa same reasons muda si mrefu.
Dini zimekuwa zikijitahidi Sana kuwekeza kwenye miundombinu na majengo ya vyuo vikuu Tanzania kwa kupitia wafadhili wao wa ndani nje ya nchi ambao Mara nyingi wakishamaliza huwa hawaendelei kuchangia gharama za uendeshaji.

Dini Kama Waislamu,wakatoliki,walutheri, waanglikana na wasabato na moravian Wana vyuo vikuu vizuri vyenye miundombinu mizuri sana lakini hupata taabu kuajiriwa wahadhiri na maprofesa mahiri kutokana na uwezo mdogo wa kifedha.

Ushauri wangu kwa serikali badala ya kufungia hivyo vyuo kwa kukosa wahadhiri wenye sifa serikali iwe inatoa wahadhiri na maprofesa na kuwapeleka kwenye hivyo vyuo kwa ajira ya kudumu .Hizo dini zimeshatoa mchango wake kwa kujenga miundo mbinu serikali nayo ichangie nguvu kazi hasa upande wa wahadhiri na maprofesa iajiri na iwapeleke kwenye hivyo vyuo.

Idadi ya wanaomaliza kidato Cha sita ni wengi kuliko uwezo wa vyuo vichache vilivyopo vyenye sifa.Sioni kwa Nini chuo kifungiwe kuendesha kozi kisa eti hakina wahadhiri wenye sifa na serikali ipo Kodi zipo iajiri wahadhiri ipeleke vyuo viendelee kudahili wanachuo.

Dini Zina mchango mkubwa kwa jamii kwa upande wa vyuo vikuu na serikali nayo inatakiwa kuwa na mchango mkubwa kwa jamii kwenye vyuo kwa kutoa wahadhiri na maprofesa
 
Taasisi za dini zinafanya vizuri kuisaidia serikali kuanzisha au kutoa hiduma za kijamii ila hapa kati zikaingiwa na tamaa ya kupata faida kubwa zikaanzisha tu vyuo visivyo na sifa ya vyuo vikuu na wakaviita vyuo vikuu. Mfano kile st. Augustine cha songea, hata hadhi ya sekondari ya kata hakikufikia ila kikaitwa chuo kikuu.
Siongelei vyuo visivyo na standard hasa kwenye miundo mbinu Hilo naungana na wewe.Mimi naongelea vyuo vyenye miundo mbinu standard.

Kuna kitu viongozi wa dini hufanya.Serikali Mfano ikisema ina uhaba wa vyuo vikuu viongozi wa dini huenda kwa wafadhili kuwalilia kwa kusema waumini wetu wanamaliza elimu ya sekondari lakini wengi hukosa natasi vyuo vikuu tunaomba mtusaidie kujenga vyuo .Wafadhili huitikia ila kwa masharti kuwa wao watagharimia miundo mbinu yote ila mengine ya uendeshaji hapana.Hapo viongozi wa dini hukubali something is better than nothing ngoja wajenge wakimaliza mengine tutahangaika nayo .Kweli wanajenga wanamaliza na wanakabidhi .Kivumbi kinakuja chuo kipo tayari wahadhiri Sasa wanapatikanaje mapato ya sadaka hayatoshi hata kuajiri wahadhiri watano wenye hadhi.Hapo ndipo serikali inatakiwa iingilie kati.kusaidia.Sababu viongozi wa dini wamejitahidi kwa uwezo wao Hadi viwanja,majengo na miundo mbinu imepatikana tena mizuri ya uhakika.Serikali hapo inabidi iwe na fungu la donation kusaidia hivyo vyuo kwa kuvipa wahadhiri.

Tume ya utumishi serikalini inatangaza nafasi za wahadhiri halafu inawapeleka kwenye hivyo vyuo Kama sehemu ya serikali kuhudumia jamii na kuifikia huko iliko viliko hivyo vyuo Kama inavyowapelekra maji,barabara nk iwapelekee wahadhiri

Hiyo ingesaidia hata kwa kiwango Fulani ada kupungua na kuwezesha vijana wengi zaidi kupata elimu za vyuo vikuu .

Sekondary wanaweza sababu nyingi hujengwa na waumini wazazi na miundo mbinu yake na gharama za uendeshaji sio kubwa Kama za vyuo vikuu ndio.maana ni rahisi kwao
 
UBIA INAWEZEKANA.

Tanzania tunayo sheria inayoweka mazingira na kuwezesha ubia kati ya Serikali na sekta binafsi. Sheria hiyo ni The Public-Private Partnership Act, 2010 kama ilivyorekebishwa mwaka 2018.

Mashirika ya Dini yaangalie uwezekano wa kufanya makubaliano na Serikali chini ya Sheria hiyo ili kumiliki na kuendesha vyuo vikuu hivyo kwa njia ya ubia (PPP).
Mkuu hili wazo lako zuri Sana.Ila Mara ingine si vizuri kusubiria hizo dini zije kuomba ubia wengi wa viongozi wa dini si wataalamu wa hayo mambo ya PPP ni vizuri serikali ku take iniatiative kuongea nao kuhusu Hilo kabla ya kuvifungia.Kuwa mna tatizo la wahadhiri mnaonaje tuingie ubia na nyie Kama wamiliki ardhi na miundombinu tuingie ubia kwa masharti moja mbili tatu .Kuongea tu kwa lugha ya upole tu maelewano yaweza kuwepo tu mbona.Kuliko time kuwa aggressive na ubabe kufunga funga tu sio vizuri.

Hili wazo lako serikali ilifanyie kazi haraka ipeleke proposal yake ya Ubia wa hiyo PPP kwa vyuo ilivyofungia kudahili vile tu vyenye miundo mbinu standard .Sidhani Kama watakataa kujadiliana kwenye Hilo.Serikali ndio ianze kwenye Hilo iwaite iongee na hao viongozi wa dini wenye hivyo vyuo.
 
Vyuo vikuu viendane na ajira ili wanaomaliza wapate matunda ya elimu yao...sio mtu anasoma then ajira hakuna anashinda mitaani mpaka aaliyosomra anasahau..
Now institution nyingi zinaajiri certificate na diploma so degree nyingi zinazagaa mtaani maana mashirika hayana pesa za kuwalipa
Tatizo la graduate Ni majizi na wazembe Ina kila Kona wasomi Ni tatizo, kule tabora mwanri anahangaika na mainjinia mtwara yaleyale dar tabu tupu mwanza Arusha mainjinia Ni tatizo, na wasipoajitiwa haohao ndio wa kwanza kulalamika ajira hakuna
 
Serikali hii hii au ipi?!
Wanaruhusu private lakini wanataka private iwalambe miguu serikali. Masharti mengi ya hovyo kutengeneza mianya ya rushwa kwa watumishi serikalini.
Mazoea ni tatizo. Unaweza kuta mtu anakwambia wahindi wababaishaji, lakini tunaona Agha Khan Hospital inakua na inafanya vizuri, Chuo chao kinafanya vizuri na kina kua, lakini waliifungia IMTU sikuona sababu, wahadhiri wazawa walitoka Muhimbili, hao hao walifundisha HKU. Wao walikataa kutoa rushwa?!
 
Dini zimekuwa zikijitahidi Sana kuwekeza kwenye miundombinu na majengo ya vyuo vikuu Tanzania kwa kupitia wafadhili wao wa ndani nje ya nchi ambao Mara nyingi wakishamaliza huwa hawaendelei kuchangia gharama za uendeshaji.

Dini Kama Waislamu,wakatoliki,walutheri, waanglikana na wasabato na moravian Wana vyuo vikuu vizuri vyenye miundombinu mizuri sana lakini hupata taabu kuajiriwa wahadhiri na maprofesa mahiri kutokana na uwezo mdogo wa kifedha.

Ushauri wangu kwa serikali badala ya kufungia hivyo vyuo kwa kukosa wahadhiri wenye sifa serikali iwe inatoa wahadhiri na maprofesa na kuwapeleka kwenye hivyo vyuo kwa ajira ya kudumu .Hizo dini zimeshatoa mchango wake kwa kujenga miundo mbinu serikali nayo ichangie nguvu kazi hasa upande wa wahadhiri na maprofesa iajiri na iwapeleke kwenye hivyo vyuo.

Idadi ya wanaomaliza kidato Cha sita ni wengi kuliko uwezo wa vyuo vichache vilivyopo vyenye sifa.Sioni kwa Nini chuo kifungiwe kuendesha kozi kisa eti hakina wahadhiri wenye sifa na serikali ipo Kodi zipo iajiri wahadhiri ipeleke vyuo viendelee kudahili wanachuo.

Dini Zina mchango mkubwa kwa jamii kwa upande wa vyuo vikuu na serikali nayo inatakiwa kuwa na mchango mkubwa kwa jamii kwenye vyuo kwa kutoa wahadhiri na maprofesa
Kitu ambacho serikali ya CCM ikijui na itakijua ni kutambua kwamba private sector kwenye elimu ni muhimu na inamchango mkubwa kuzidi public sector, wanahitaji msaada mukubwa kwasababu wanafanya kazi nzuri iliopaswa kufanywa na serikali,

Angalia shule binafsi za msingi na sekondari zinatowa product nzuri sana kuliko hizi za kata, na watoto wa viongozi wengi wana soma hizo shule wenyewe hawana imani na shule za sarikali.

Lakini serikali ya Ccm inachukulia shule hizi kama mpizani wa biashara, "foolish" wakati zinatowa huduma muhimu, nyingi zinawekewa vizingiti ili zife kama leseni ya biashara kodi ukagunzi wakushutukiza, nk na nyingi zimefunga hususani awamu hi ya tano, Kenya na Uganda wakati wanaanzisha hizi shule binafsi serikali ilisaidia sana kwa kulipa waalimu mishahara mizuri bila kuangalia private au serikalini, ndomaana wana shule nzuri sanaa ambazo watanzania wengi wanakimbilia kupata elimu bora.

Serikali inapashwa ibadilike iache wivu na fitna kwenye private sector ili tupige hatua
 
Tatizo la graduate Ni majizi na wazembe Ina kila Kona wasomi Ni tatizo, kule tabora mwanri anahangaika na mainjinia mtwara yaleyale dar tabu tupu mwanza Arusha mainjinia Ni tatizo, na wasipoajitiwa haohao ndio wa kwanza kulalamika ajira hakuna
Sema baadhi sio wote
 
Ukianzisha taasisi yako binafsi lazima ufuate miongozo na vigezo.....chuo,shule,hospitali nk lazima vijitosheleze Kila idara ili kutoa huduma Bora na si Bora huduma.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom