Serikali, huu ndiyo muda muafaka wa kubadilisha sheria za wafanyakazi; Nyongeza ya mishahara iwe ni kwa wafanyakazi bora au maalum tu

dmkali

JF-Expert Member
Nov 17, 2014
11,276
21,395
Naomba kutoa Rai kwa serikali!

"Ukicheka na nyani Utavuna mabua" TUCTA must watch out!

Kuna HAKI na WAJIBU wa kila MTU

Haki ya mfanyakazi ni kulipwa ujira wake kama kanuni zinavyosema! LAKINI wajibu wa mfanyakazi ni kufanya kazi bora ili mwajili awe na sababu ya kulipa ujira huo hata Zaidi.

Sakata la nyongeza ya mishahara liwe fursa kwa serikali kubadilisha sheria za mfanyakazi ili kuongeza uwajibikaji!
Tiba ya kudumu ya sakata hili iko kwenye mageuzi ya sheria mbili

1. Sheria ya kumlinda mfanyakazi itazamwe upya

2. Sheria ya kibenki kwa mfanyakazi kukopea mshahara iwekewe spidi gavana

Ni kweli walistahili kuongezwa lakini je kuna tija gani kwa serikali kuwaongezea mishahara?

1. Unawaongezeaje mishahara wafanyakazi wavivu?

2. Unawaongezeaje mishahara wafanyakazi watoro kazini?

3. Unawaongezeaje mishahara wafanyakazi wabadhilifu?

4. Unawaongezeaje mishahara wafanyakazi wala rushwa?

5. Unawaongezeaje mishahara wafanyakazi wanaotegemea makal** kama CV?

6. Unawaongezeaje mishahara wafanyakazi waolalamikiwa na kila mwananchi mnyonge anaehitaji huduma bora?

Hata siku moja SIJAWAHI kuona TUCTA wakisimama kidete kuwakumbusha na kuwaonya wafanyakazi kuwajibika!

Sheria za mfanyakazi Tanzania zina mpa ulinzi mkubwa mno mfanyakazi kiasi kwamba haoni sababu ya kuwajibika ipasavyo kazini!

Mfanyakazi anaweza asiwajibike kazini sheria inamlinda, anaweza kula rushwa na akahamishwa, anaweza lewa chakali kazini na asifukuzwe, anaweza kunyonya hata mafuta ya gari la serikali na asifukuzwe, utoro, umalaya, uchelewaji, uzembe wa kila aina n.k na bado serikali ikamkubatia au kumhamisha idara.

Sheria za wafanyakazi ziliundwa enzi hizo kulikuwa hakuna wafanyakazi wa kutosha! LEO HII Sioni sababu ya kukumbatia sheria zinazompa Amani mfanyakazi wakati SERIKALI ikitukanwa kila kona kwa kuwakumbatia WAZEMBE.

Ukichunguza taasisi nyingi sana zinabebwa na watu wachache waojituma, asilimia kubwa wengi ni bora liende.

Kama ni benki utashangaa anaechapa kazi ni mmoja au wawili, kama ni shirika anaejituma katika 100 utakuta ni wafanyakazi 10 tu!

Sasa kwanini serikali isiweke sheria za kuwaongezea mishahara wale wafanyakazi bora wanaojituma kuliko kuhangaika na wafanyakazi wasio na tija?

Wafanyakazi wa kima cha chini huenda wameonekana bora kwasababu wengi wao wanajitahidi kiasi chake, kama ni usafi maofisini wanafanya, chai wanawapikia n.k

Je ni kweli Kwamba mishahara HAUTOSHI?

Jibu ni rahisi sana, Mishahara haujawahi kutosha hata iwe milioni 100 kwa mwezi HAUTATOSHA!

Tatizo kubwa sasa ni sheria na kanuni za mikopo hizi ndizo zinawatesa wafanyakazi!

Wanakopa na kutop-up pesa asilimia kubwa ya mishahara na kubakiwa na kitu kidogo ambacho hakiwatoshi kwa mwezi!

Mfano mtu alipwa 1mil, anakopea benki kununua SUBARU anabakiwa na mshahara wa laki mbili. kwa mwezi!
Gari lake kwa siku linataka elf 30! Sasa mtu kama huyu unafikili atasema mshahara unamtosha?

Wekeni sheria za ukomo wa kukopea mishahara iwe ni 30% tu, ili abakiwe na hela ya matumizi.

Sakata la mishahara likawe fursa kwa selikali kufumua sheria kwa dharura kuongeza uwajibikaji.

Kelele za Tucta zikizidi ndugu zangu kina "Flamingo" mnajua kazi yenu! ombeni kibali mmalize mchezo.
IMG-20220728-WA0000.jpg
 
Hawawezi..jinsia ke huko maofisini inavyoomba kila kitu isaidiwe itatoboa??
Mbona huko sekta binafsi wadada wanapiga kazi vizuri roho inapenda!
Kwanini serikalini ni mizigo kama siyo kwamba wanabebeka migongoni na serikali halafu wanapanda na viwembe!

Mtoto akizidi kukuchezea sharubu usishangae siku akikutia sinki, Muda wa kuwanyoosha wafanyakazi ni sasa! Wamejaa wenyewe
 
Nimekuelewa vyema! Chanzo ni roho za ubinafsi zinawasumbua! Hata huku kwenye sensa eti nako wafanyakazi kazi wamekuja kutuzibia RIZIKI
Tumekosa.
 
Haujui unachokiongea nyongeza ya Msahahara ipo na ni haki ya kila afanyae kazi hata house girl na inapaswa iendane na inflation au mfumko wa bei.

Labda ungeongelea kupandishwa cheo hapo sawa, lkn nyongeza ya Mshahara ni haki maadamu umemuajiri mtu basi una jukumu la kumlipa stahiki zake pia sasa kama hafanyi kazi unaweza mwachisha kazi lkn stahiki zake lazima umlipe!
 
Haujui unachokiongea nyongeza ya Msahahara ipo na ni haki ya kila afanyae kazi hata house girl na inapaswa iendane na inflation au mfumko wa bei.

Labda ungeongelea kupandishwa cheo hapo sawa, lkn nyongeza ya Mshahara ni haki maadamu umemuajiri mtu basi una jukumu la kumlipa stahiki zake pia sasa kama hafanyi kazi unaweza mwachisha kazi lkn stahiki zake lazima umlipe!
Toshekeni na mnachopata ili serikali iwahudumie watanzania
 
Unaowaambia wao tija yao iko wapi ??
Huyu jamaa ameandika kama vile anaishi Canada! Serikali yenyewe imejaa watu wababaishaji tu na watu walioteuliwa kwa vigezo vya kujuana kwa misingi ya kikabila, undugu, udini na ukada!

Halafu anataka wafanyakazi wenye tija! Hiyo tija inatoka wapi kama serikali yenyewe haina tija? Anataka wafanyakazi wakopeshwe hela kidogo kana kwamba serikali inawagharamia nyumba za kuishi, kama ifanyavyo kwa watumishi wa sekta nyingine!
 
Huyu jamaa ameandika kama vile anaishi Canada! Serikali yenyewe imejaa watu wababaishaji tu na watu walioteuliwa kwa vigezo vya kujuana kwa misingi ya kikabila, undugu, udini na ukada!

Halafu anataka wafanyakazi wenye tija! Hiyo tija inatoka wapi kama serikali yenyewe haina tija? Anataka wafanyakazi wakopeshwe hela kidogo kana kwamba serikali inawagharamia nyumba za kuishi, kama ifanyavyo kwa watumishi wa sekta nyingine!
Wakikopa pesa yote ndo chanzo cha kulia lia njaa hadi wanaona kama pesa haiwatoshi
 
Toshekeni na mnachopata ili serikali iwahudumie watanzania

Sawa, lakini kwa nini raisi awadanganye watu? Kulikuwa na ulazima gani? Mbona Wafanyakazi wameishi hivyo bila nyongeza ya mshahara miaka yote? Huyo raisi wako kaja kawaahidi kuwaongeza 23% ya Mshahara watu wamefurahia na kusubiri mshahara kutoka hakuna nyongeza aliyoahidi, sasa kwa nini aseme uongo wakati hata ametoka Uarabuni kuhiji? Mtu tayari ana maisha magumu halafu hapo hapo unamdanganya kwamba nafuu inakuja, kwa nini anawafanyia hivi watu?

Uongo ni dhambi!
 
Sawa, lakini kwa nini raisi awadanganye watu? Kulikuwa na ulazima gani? Mbona Wafanyakazi wameishi hivyo bila nyongeza ya mshahara miaka yote? Huyo raisi wako kaja kawaahidi kuwaongeza 23% ya Mshahara watu wamefurahia na kusubiri mshahara kutoka hakuna nyongeza aliyoahidi, sasa kwa nini aseme uongo wakati hata ametoka Uarabuni kuhiji?

Mtu tayari ana maisha magumu halafu hapo hapo unamdanganya kwamba nafuu inakuja, kwa nini anawafanyia hivi watu?

Uongo ni dhambi!
Aliahidi jambo letu lipo japo kwa kidogo! Hakusema wote mtapata!
Alisema jambo letu lipo ingawa ni kidogo pokeeni! Asilimia 23% ndicho kiwango cha juu ja jambo letu!

Haiwezekani na haitakaa itokee kwa mtu anaelipwa 3mil ukamuongezea asilimia 23% maana yake umuongezee 600000/=

Itakuwa serikali ya ajabu sana iongeze laki 6 kwa mfanyakazi wakati wananchi huko hospital hakuna MADAWA
Hilo halipo na sahau.
 
Sawa, lakini kwa nini raisi awadanganye watu? Kulikuwa na ulazima gani? Mbona Wafanyakazi wameishi hivyo bila nyongeza ya mshahara miaka yote? Huyo raisi wako kaja kawaahidi kuwaongeza 23% ya Mshahara watu wamefurahia na kusubiri mshahara kutoka hakuna nyongeza aliyoahidi, sasa kwa nini aseme uongo wakati hata ametoka Uarabuni kuhiji? Mtu tayari ana maisha magumu halafu hapo hapo unamdanganya kwamba nafuu inakuja, kwa nini anawafanyia hivi watu?

Uongo ni dhambi!
Ilikuwa lugha Jumuishi! Ni kama vile serikali ilipotangaza itashusha bei ya mafuta kwa BILIONI 100! Uhalisia ilipunguza tsh 50~100 kwa lita siyo bilioni 100
 
Aliahidi jambo letu lipo japo kwa kidogo! Hakusema wote mtapata!
Alisema jambo letu lipo ingawa ni kidogo pokeeni!
Asilimia 23% ndicho kiwango cha juu ja jambo letu!

Haiwezekani na haitakaa itokee kwa mtu anaelipwa 3mil ukamuongezea asilimia 23% maana yake umuongezee 600000/=

Itakuwa serikali ya ajabu sana iongeze laki 6 kwa mfanyakazi wakati wananchi huko hospital hakuna MADAWA
Hilo halipo na sahau

Kwa hiyo Wafanyakazi wote pamoja na vyama vya Wafanyakazi ni wajinga na kwamba hawakuelewa alichosema?
 
Naomba kuongeza machache, wakati tunawaza utekelezaji wa haya mapendekezo yako mazuri, nakumbusha tatizo kubwa linalokabili nchi masikini na zinazoendelea ni uadulifu.

Tusiposhughulikia hili kwanza, kuna hatari wasio na vigezo watapata nyongeza ya mshahara kila siku, ila wenye vigezo wakabaki na malalamiko ya kutoonekana, matokeo yake na wao wataanza kulipua kazi.

Kingine, nadhani malalamiko ya wafanyakazi hayajajikita zaidi kwenye mshahara kutosha, bali ni kuakisi uhalisia wa maisha. Kwa kutumia akili ya kawaida, gharama za maisha ya miaka 5 iliyopita sio sawa na za leo, kwanini wafanyakazi wanaotegemea mshahara kama sehemu kubwa ya kipato chao, malipo yabaki vile vile au kuwa na tofauti ndogo sana!?
 
Ilikuwa lugha Jumuishi! Ni kama vile serikali ilipotangaza itashusha bei ya mafuta kwa BILIONI 100! Uhalisia ilipunguza tsh 50~100 kwa rita siyo bilioni 100

Nafikiri ni bora ungewekeza muda wako kwenye kujifunza lugha kwanza, achilia mbali hata kujua tu maana ya lita!
 
Naomba kuongeza machache, wakati tunawaza utekelezaji wa haya mapendekezo yako mazuri, nakumbusha tatizo kubwa linalokabili nchi masikini na zinazoendelea ni uadulifu.

Tusiposhughulikia hili kwanza, kuna hatari wasio na vigezo watapata nyongeza ya mshahara kila siku, ila wenye vigezo wakabaki na malalamiko ya kutoonekana, matokeo yake na wao wataanza kulipua kazi.

Kingine, nadhani malalamiko ya wafanyakazi hayajajikita zaidi kwenye mshahara kutosha, bali ni kuakisi uhalisia wa maisha. Kwa kutumia akili ya kawaida, gharama za maisha ya miaka 5 iliyopita sio sawa na za leo, kwanini wafanyakazi wanaotegemea mshahara kama sehemu kubwa ya kipato chao, malipo yabaki vile vile au kuwa na tofauti ndogo sana!?
Ndiyo maana wale wa kima cha chini wameongezewa hiyo 23%, lakini kusema umuongezee huyu wa 4mil au 3mil maana yake ukamuongee laki sita au saba kwa mkupuo!
Anyway basi hata kama serikali inapesa za ziada! Je hawa wafanyakazi wanastahili kweli kuongezewa mishahara kwa igoro wanaufanya kwenye huduma za wananchi?
Si bora pesa hizo kama zipo zikanunue madawa hospital?
 
Mbona sasa hizo sababu zote ulizotaja hapo juu zinatoa jibu kwa nini mishahara iongezwe utafanya vipi kazi wakati mishahara midogo hiyo ari unaitoa wapi
 
Mbona sasa hizo sababu zote ulizotaja hapo juu zinatoa jibu kwa nini mishahara iongezwe utafanya vipi kazi wakati mishahara midogo hiyo ari unaitoa wapi
Mishahara pekee haitoshi kuongeza Ari ya uwajibikaji; Kwani wabunge wanaolala bungeni huwa wamenyimwa posho?
 
Naomba kutoa Rai kwa serikali!

"Ukicheka na nyani Utavuna mabua" TUCTA must watch out!

Kuna HAKI na WAJIBU wa kila MTU

Haki ya mfanyakazi ni kulipwa ujira wake kama kanuni zinavyosema! LAKINI wajibu wa mfanyakazi ni kufanya kazi bora ili mwajili awe na sababu ya kulipa ujira huo hata Zaidi!
Sakata la nyongeza ya mishahara liwe fursa kwa serikali kubadilisha sheria za mfanyakazi ili kuongeza uwajibikaji!
Tiba ya kudumu ya sakata hili iko kwenye mageuzi ya sheria mbili

1. Sheria ya kumlinda mfanyakazi itazamwe upya
2. Sheria ya kibenki kwa mfanyakazi kukopea mshahara iwekewe spidi gavana

Ni kweli walistahili kuongezwa lakini je kuna tija gani kwa serikali kuwaongezea mishahara?

1. Unawaongezeaje mishahara wafanyakazi wavivu?
2. Unawaongezeaje mishahara wafanyakazi watoro kazini?
3. Unawaongezeaje mishahara wafanyakazi wabadhilifu?
4. Unawaongezeaje mishahara wafanyakazi wala rushwa?
5. Unawaongezeaje mishahara wafanyakazi wanaotegemea makal** kama CV?
6. Unawaongezeaje mishahara wafanyakazi waolalamikiwa na kila mwananchi mnyonge anaehitaji huduma bora?

Hata siku moja SIJAWAHI kuona TUCTA wakisimama kidete kuwakumbusha na kuwaonya wafanyakazi kuwajibika!

Sheria za mfanyakazi Tanzania zina mpa ulinzi mkubwa mno mfanyakazi kiasi kwamba haoni sababu ya kuwajibika ipasavyo kazini!
Mfanyakazi anaweza asiwajibike kazini sheria inamlinda, anaweza kula rushwa na akahamishwa, anaweza lewa chakali kazini na asifukuzwe, anaweza kunyonya hata mafuta ya gari la serikali na asifukuzwe, utoro, umalaya, uchelewaji, uzembe wa kila aina n.k na bado serikali ikamkubatia au kumhamisha idara!

Sheria za wafanyakazi ziliundwa enzi hizo kulikuwa hakuna wafanyakazi wa kutosha! LEO HII Sioni sababu ya kukumbatia sheria zinazompa Amani mfanyakazi wakati SERIKALI ikitukanwa kila kona kwa kuwakumbatia WAZEMBE.

Ukichunguza taasisi nyingi sana zinabebwa na watu wachache waojituma, asilimia kubwa wengi ni bora liende!
Kama ni benki utashangaa anaechapa kazi ni mmoja au wawili, kama ni shirika anaejituma katika 100 utakuta ni wafanyakazi 10 tu!

Sasa kwanini serikali isiweke sheria za kuwaongezea mishahara wale wafanyakazi bora wanaojituma kuliko kuhangaika na wafanyakazi wasio na tija?

Wafanyakazi wa kima cha chini huenda wameonekana bora kwasababu wengi wao wanajitahidi kiasi chake, kama ni usafi maofisini wanafanya, chai wanawapikia n.k

Je ni kweli Kwamba mishahara HAUTOSHI?
Jibu ni rahisi sana, Mishahara haujawahi kutosha hata iwe milioni 100 kwa mwezi HAUTATOSHA!

Tatizo kubwa sasa ni sheria na kanuni za mikopo hizi ndizo zinawatesa wafanyakazi!
Wanakopa na kutop-up pesa asilimia kubwa ya mishahara na kubakiwa na kitu kidogo ambacho hakiwatoshi kwa mwezi!

Mfano mtu alipwa 1mil, anakopea benki kununua SUBARU anabakiwa na mshahara wa laki mbili. kwa mwezi!
Gari lake kwa siku linataka elf 30! Sasa mtu kama huyu unafikili atasema mshahara unamtosha?

Wekeni sheria za ukomo wa kukopea mishahara iwe ni 30% tu, ili abakiwe na hela ya matumizi

Sakata la mishahara likawe fursa kwa selikali kufumua sheria kwa dharura kuongeza uwajibikaji!

Kelele za Tucta zikizidi ndugu zangu kina "Flamingo" mnajua kazi yenu! ombeni kibali mmalize mchezo!
View attachment 2306509
Amino nakwambia hayo usemayo yakizingatiwa hata Chief atajikuta haongezewi au hajiongezei mshahara. Niamini
 
Back
Top Bottom