Serikali hii ya Magufuli itakuwa na ubavu wa kugomea masharti magumu ya Wachina ilhali wanataka kukamilisha miradi hii ndani ya miaka mitano?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,013
144,371
Binafsi naona Serikali hii mpaka sasa imeshajiweka katika mazingira magumu yatayopelekea kukubali mashariti magumu kutoka kwa mtu yoyote (wakiwemo wachina) anaetaka kuwekaza fedha zake katika kukamilisha miradi mikubwa ya awamu ya tano kama ule wa Bwawa la Umeme wa mto Rufiji na ule wa ujenzi wa reli ya kisiasa (SGR).

Kwa mtazamo wangu, sababu ni hizi:

1. Miradi hii imeshaanza kutekelezwa, hivyo ni lazima tupambane iishe vinginevyo itakuwa ni aibu na pigo kisiasa.

2. Tumeshatangaza kwa umma na dunia kuwa miradi hii ni lazima ikamilike na ahadi hii kwa watanzania teyari ni deni la kisiasa na pia ikifeli ni kete kwa wapinzani.

3. Tumeshaingia mikataba na wakandarasi na sijui kama mikataba tulioingia inatambua kusitishwa kwa mradi wakati wowote ule na kwasababu yoyote ile bila kuwa na gharama ya kusitisha mradi husika.

4. Kitaalamu sijui kama inawezekana/ inashauriwa kusitisha miradi ya aina hii pale inapokuwa tayari imeshaanza kutekelezwa.

5. Kusimamisha miradi hii kwa muda sidhani kama ndio itakuwa ni kusimamisha gharama za mradi kwa asilimia 100 ili hali mitambo na vitu vingine tayari viko site na kazi ya ujenzi tayari ilishaanza.

Hivyo basi, kwa kuzingatia sababu hizo hapo juu na nyingine ambazo inawezekana sijazitaja, sioni kama tutaingia kwenye meza ya mazungumzo tukiwa na jeuri ya kukataa mashariti magumu iwapo yatatolewa na Wachina au mtu mwingine yeyote atakaekuwa tayari kuokoa jahazi kwa kuwekaza fedha zake katika hii miradi.

Vile vile sidhani kama mchina au mtu mwingine yeyote ataacha ku-take advantage ya hali hii kutunyonya tofauti na ku-negotiate wakati mradi/miradi bado haijaanza kutekelezwa.

Tusubiri.
 
Teyari Wachina wameshaanza kuzengezengea- ukiona ndege aina ya tai akizunguka angani sehemu fulani ujue chini kuna mnyama anakaribia kuwa mzoga,
Kwa sasa tumeshachemsha, hivyo tutalazimika kukubali hata mashariti ambayo pengine tungeweza kuyakataa as long as miradi hii ilikuwa bado haijaanza kutekelezwa.
 
Teyari Wachina wameshaanza kuzengezengea- ukiona ndege aina ya tai akizunguka angani sehemu fulani ujue chini kuna mnyama anakaribia kuwa mzoga,
Aisee, Kwahiyo miradi hiyo ni mizoga ya CCM?? Tafadhali ndugu😒
 
Kwa sasa tumeshachemsha, hivyo tutalazimika kukubali hata mashariti ambayo pengine tungeweza kuyakataa as long as miradi hii ilikuwa bado haijaanza kutekelezwa.

Nakumbuka misimamo ya Nyerere hadi tukakwama, ila alipoingia Mwinyi hakuwa na jinsi, ilibidi akubali hata yale ambayo angeweza kuyakataa kama angeingia kwenye makubaliano kabla mambo hayajaharibika vile.
 
Nakumbuka misimamo ya Nyerere hadi tukakwama, ila alipoingia Mwinyi hakuwa na jinsi, ilibidi akubali hata yale ambayo angeweza kuyakataa kama angeingia kwenye makubaliano kabla mambo hayajaharibika vile.
Si ajabu hali kama hiyo ikajirudia tena kwenye utekelezaji wa hii mradi.
 
Tulibana sasa tunaanza kuachia, mwishoni mwa utawala wa Awamu ya nne, wachina walizagaa kila kona hadi vijijini, kuzunguka soko la Kariakoo kote walikuwa wachina mpaka wakawa wanafanya kazi ya umachinga, awamu ya tano ilipoingia wakadhibiti hali hii.

Wahamiaji haramu wa kichina walidhibitiwa na kupewa masharti na wengi walirudi kwao. Sasa tena wanaanza kutaka kurudi, simu hizo siyo bureeee, TUMEBANA SASA TUNAACHIA.
 
Sasa mtu anapita karibu na Ziwa, anasema mimi nafikiri tujenge daraja hapa ziwani anaagiza palepale mchakato uanze na pes zitengwe bila kuangalia kwanza pririty ni nini.

Shilingi bilion 700 za ujenzi wa daraja la Busisi zingeingia kwenye barabara au hata Stieglers zingefanya kitu kikubwa zaidi.

Kule Busisi wananchi walikuwa wanahitaji vivuko vizuri tu kwa sasa kwanza
 
Binafsi naona serikali hii mpaka sasa imeshajiweka katika mazingira magumu yatayopelekea kukubali mashariti magumu kutoka kwa mtu yoyote (wakiwemo wachina) anaetaka kuwekaza fedha zake katika kukamilisha miradi mikubwa ya awamu ya tano kama ule wa Bwawa la Umeme wa mto Rufiji na ule wa ujenzi wa reli ya kisiasa(SGR).
Mkuu, kwani serikali imepewa masharti gani mpaka sasa? Au unapiga ramli na kuombea hiyo miradi isikamilike ili ufurahi?!
 
Magufuli hana rafiki; kwa hiyo hashindwi kabisa kuwakatalia Wachina papo kwa papo wakileta masharti asiyokubaliana nayo.
 
Binafsi naona serikali hii mpaka sasa imeshajiweka katika mazingira magumu yatayopelekea kukubali mashariti magumu kutoka kwa mtu yoyote (wakiwemo wachina) anaetaka kuwekaza fedha zake katika kukamilisha miradi mikubwa ya awamu ya tano kama ule wa Bwawa la Umeme wa mto Rufiji na ule wa ujenzi wa reli ya kisiasa(SGR).

Kwa mtazamo wangu, sababu ni hizi:

1.Miradi hii imeshaanza kutekelezwa, hivyo ni lazima tupambane iishe vinginevyo itakuwa ni aibu na pigo kisiasa.

2.Tumeshatangaza kwa umma na dunia kuwa miradi hii ni lazima ikamilike na ahadi hii kwa watanzania teyari ni deni la kisiasa na pia ikifeli ni kete kwa wapinzani.

3.Tumeshaingia mikataba na wakandarasi na sijui kama mikataba tulioingia inatambua kusitishwa kwa mradi wakati wowote ule na kwasababu yoyote ile bila kuwa na gharama ya kusitisha mradi husika.

4.Kitaalamu sijui kama inawezekana/ inashauriwa kusitisha miradi ya aina hii pale inapokuwa tayari imeshaanza kutekelezwa.

5.Kusimamisha miradi hii kwa muda sidhani kama ndio itakuwa ni kusimamisha gharama za mradi kwa asilimia 100 ili hali mitambo na vitu vingine tayari viko site na kazi ya ujenzi tayari ilishaanza.

Hivyo basi, kwa kuzingatia sababu hizo hapo juu na nyingine ambazo inawezekana sijazitaja, sioni kama tutaingia kwenye meza ya mazungumzo tukiwa na jeuri ya kukataa mashariti magumu iwapo yatatolewa na wachina au mtu mwingine yeyote atakaekuwa tayari kuokoa jahazi kwa kuwekaza fedha zake katika hii miradi.

Vile vile sidhani kama mchina au mtu mwingine yeyote ataacha ku-take advantage ya hali hii kutunyonya tofauti na ku-negotiate wakati mradi/miradi bado haijaanza kutekelezwa.

Tusubiri.
Hiyo ndiyo inaitwa kufa na tai shingoni maana hatuwezi kukubali tushindwe kuimaliza hiyo miradi maana tutachekwa na kubezwa,wakati rasilimali michuzi hatuna.
 
Back
Top Bottom