Naanto Mushi
JF-Expert Member
- Oct 16, 2015
- 6,236
- 15,600
Habarini wakuu na raia wenzangu wa taifa la chama kimoja, japo nna uchungu mkubwa, lakini kamwe siwezi kuwa mvivu wa kutumia kalamu yangu kuihabarisha jamii na taifa langu, nimeteseka sana kwenye hii nchi, na nimekuwa nikitamani kuona hii nchi siku moja inapiga hatua moja ama nyingine - socially, economically, politically, legally etc, lakini so far, i am disappointed big time.
*****
Kumekuwepo na malalamiko ya kuadimika kwa Cement na kwamba hata inapopatikana bei inakuwa ni juu sana karibia ongezeko la asilimia zaidi ya 55% kulinganisha na bei ya mwanzo (TZS 14,000 mpaka TZS 22,000) huku baadhi ya maeneo yakishuhudia bei ikikaribia TZS 35,000 kwa mfuko.
Wakati huo huo nimeona viongozi wa serikali; wakuu wa mikoa, wilaya, na hata wakuu wa jeshi la Polisi wakisisitiza nyakati tofauti kwamba, watamchukulia hatua yoyote ambaye watamkuta anauza kwa bei kuzidi bei ya awali, yaani TZS 14,000.
**
Kwanza kabisa niseme, serikali inahusika moja kwa moja na huu upungufu tuonaouona, na visababishi vikubwa ni 1) ‘Sera za miundombinu kwenye utawala wa awamu ya tano wa serikali ya Magufuli’. 2) ‘Serikali kufinya jithada za uwekezaji kwenye sekta ya cement’
1... Serikali ya Magufuli, ilikuja na mkazo wa kasi sana wa kuwekeza kwenye miradi mikubwa ya miundombinu hapa nchini.
Ukiangalia takwimu, ni kwamba kwa kipindi cha utawala wa Magufuli, sekta nzima ya ujenzi (construction) imeweza kuwa na wastani wa ukuaji mkubwa sana (wastani wa asilimia 17.45% kwa miaka mitano iliyopita), na driver kubwa ikiwa ni hiyo miradi mkubwa ya ujenzi ya serikali.
Kwa sababu, Cement ni mali ghafi muhimu sana katika sekta ya ujenzi, unapokuwa na ukuaji wa kasi sana wa sekta ya ujenzi maana yake unatakiwa kuwa na ukuaji wa kasi kubwa maradufu ya uzalishaji wa Cement ili uweze kuhudumia kikamilifu mahitaji ya sekta ya ujenzi.
Kosa kubwa lililofanyika ni kwamba, serikali wali focus zaidi kutekeleza miradi hii mikubwa ya ujenzi bila kuangalia uwezo binafsi wa uzalishaji wa viwanda vya ndani vya Cement (supply capacity).
Mbali na kutokuangalia uwezo wa uzalishaji wa viwanda vya ndani, ni kweli kwamba serikali haikuwa rafiki kwenye kuhakikisha wanawezesha mazingira ya uwekezaji kwenye viwanda vya cement, ukifuatilia fitina alizofanyiwa mwekezaji Aliko Dangote, hakika hutatofautiana na mimi kwamba kuna mahali serikali haikutimiza wajibu wake kudhibiti uimara wa soko la cement.
Ukiangali hizo takwimu, viashiria dhahiri vya msukosuko wa cement vilianza kujitokeza kuanzia mwaka 2017 na 2018, ambapo utaona wazi ukuaji wa uzalishaji wa cement ulikuwa kiduchu sana (3.2% kwa 2017 na 7.4% kwa 2018) ukifananisha na ukuaji wa sekta ya ujenzi (18.0% mwaka 2017 na 17.1% mwaka 2018). Kama ni janga basi lilianzia kwenye hii miaka 2 (2017 & 2018).
Ndo mana unaona, pamoja na ongezeko kubwa la 44% kwenye uzalishaji wa cement kwa mwaka 2019, lakini bado bei ya cement ilianza ku-shoot tangu tuanza huu mwaka, ikimaanisha kwamba supply ya cement bado haitoshelezi mahitaji.
Kwa hiyo, tunachokishuhudia kwa sasa kwenye soko la cement ni kwamba, output ambayo inazalishwa na viwanda vya cement kwa sasa, karibu yote inaliwa na mahitaji kutoa miradi ya serikali, na kupelekea kufubaza output ambayo inatakiwa ikauzwe kwenye soko la wananchi.
Ndo mana sasa unakuta kwa sasa, ukienda viwandani wanakuambia bei bado ni zile zile hazijabbadilika za kwenye Tzs 13,500 lakina hawana supply ya kukupa maana yote ipo booked na contractors wa hii miradi ya serikali, matokeo yake Cement pungufu inayoingia kwenye soko la wananchi inagombaniwa na wananchi na ku trigger profit seeking behaviour ya wafanyabiashara ambao wanacapitalise inefficiency ya soko kwenye demand na supply ili kujinufaisha. Kiuchumi.
Serikali amekuwa akitumia nguvu kubwa ya mabavu aliyonayo, kutoa vitisho kwa wafanyabiashara kwamba wao ndo chanzo cha kupanda kwa bei ya cement, na kusahau kabisa kwamba yenyewe serikali ndio imekuwa haitimizi wajibu wake kikamilifu.
So, ni kwamba kuna mlima mkubwa sana wa kupanda kwa waziri wa ujenzi na viwanda wanaokuja, kuondoa uchafu wa serikali kwenye issue ya cement, ikwezekana, mwekezaji Dangote aitwe na serikali kwa hali ya dharura.
Ni mimi raia mkereketwa wa nchi ya chama kimoja.
N.Mushi
*****
Kumekuwepo na malalamiko ya kuadimika kwa Cement na kwamba hata inapopatikana bei inakuwa ni juu sana karibia ongezeko la asilimia zaidi ya 55% kulinganisha na bei ya mwanzo (TZS 14,000 mpaka TZS 22,000) huku baadhi ya maeneo yakishuhudia bei ikikaribia TZS 35,000 kwa mfuko.
Wakati huo huo nimeona viongozi wa serikali; wakuu wa mikoa, wilaya, na hata wakuu wa jeshi la Polisi wakisisitiza nyakati tofauti kwamba, watamchukulia hatua yoyote ambaye watamkuta anauza kwa bei kuzidi bei ya awali, yaani TZS 14,000.
**
Kwanza kabisa niseme, serikali inahusika moja kwa moja na huu upungufu tuonaouona, na visababishi vikubwa ni 1) ‘Sera za miundombinu kwenye utawala wa awamu ya tano wa serikali ya Magufuli’. 2) ‘Serikali kufinya jithada za uwekezaji kwenye sekta ya cement’
1... Serikali ya Magufuli, ilikuja na mkazo wa kasi sana wa kuwekeza kwenye miradi mikubwa ya miundombinu hapa nchini.
- Nyerere Hydropower Plant – USD 3.9 Billion (TZS 9 Trillioni) Timeline > 2019 - 2022
- SGR Project – USD 14.2 Billion (TZS 32.9 Trillioni) Timeline > 2019 - ?
- Ubungo Flyover & Tazara Flyover - USD 150 Million (TZS 300 Billion)
- Salender Ocean Bridge – USD 126 Million (TZS 292 Billion)
- Kigongo Busisi, Daraja jipya la wami, Ikulu Dodoma, Nyumba za serikali Dodoma n.k
- Upanuzi wa bandari na viwanja vya ndege
- Na tumesikia kwenye hotuba ya Rais leo kwenye ufunguzi wa bunge, inaonekana shuhuli za ujenzi zitaendelea kushamiri miak miwili mpaka mitatu ijayo.
Ukiangalia takwimu, ni kwamba kwa kipindi cha utawala wa Magufuli, sekta nzima ya ujenzi (construction) imeweza kuwa na wastani wa ukuaji mkubwa sana (wastani wa asilimia 17.45% kwa miaka mitano iliyopita), na driver kubwa ikiwa ni hiyo miradi mkubwa ya ujenzi ya serikali.
Kwa sababu, Cement ni mali ghafi muhimu sana katika sekta ya ujenzi, unapokuwa na ukuaji wa kasi sana wa sekta ya ujenzi maana yake unatakiwa kuwa na ukuaji wa kasi kubwa maradufu ya uzalishaji wa Cement ili uweze kuhudumia kikamilifu mahitaji ya sekta ya ujenzi.
Kosa kubwa lililofanyika ni kwamba, serikali wali focus zaidi kutekeleza miradi hii mikubwa ya ujenzi bila kuangalia uwezo binafsi wa uzalishaji wa viwanda vya ndani vya Cement (supply capacity).
Mbali na kutokuangalia uwezo wa uzalishaji wa viwanda vya ndani, ni kweli kwamba serikali haikuwa rafiki kwenye kuhakikisha wanawezesha mazingira ya uwekezaji kwenye viwanda vya cement, ukifuatilia fitina alizofanyiwa mwekezaji Aliko Dangote, hakika hutatofautiana na mimi kwamba kuna mahali serikali haikutimiza wajibu wake kudhibiti uimara wa soko la cement.
2014 | 2015 | 2016 | 2017 | 2018 | 2019 | |
Uzalishaji wa Cement kwa Tani - Tanzania | 2,809,100 | 3,134,900 | 4,071,400 | 4,199,900 | 4,509,100 | 6,514,700 |
Ukuaji wa uzalishaji wa Cement - % | n/a | 11.6% | 29.9% | 3.2% | 7.4% | 44.5% |
Asilimia za ukuaji wa sekta ya ujenzi - % | n/a | 15.9% | 17.8% | 18.0% | 17.1% | 18.6% |
Wastani wa ukuaji wa pato la taifa (GDP) - % | n/a | 6.0% | 6.0% | 6.0% | 6.0% | 6.0% |
Multiplier ya ukuaji wa sekta ya ujenzi ukifananisha na ukuaji wa pato la Taifa | n/a | 2.65 | 2.97 | 3.00 | 2.84 | 3.10 |
Ukiangali hizo takwimu, viashiria dhahiri vya msukosuko wa cement vilianza kujitokeza kuanzia mwaka 2017 na 2018, ambapo utaona wazi ukuaji wa uzalishaji wa cement ulikuwa kiduchu sana (3.2% kwa 2017 na 7.4% kwa 2018) ukifananisha na ukuaji wa sekta ya ujenzi (18.0% mwaka 2017 na 17.1% mwaka 2018). Kama ni janga basi lilianzia kwenye hii miaka 2 (2017 & 2018).
Ndo mana unaona, pamoja na ongezeko kubwa la 44% kwenye uzalishaji wa cement kwa mwaka 2019, lakini bado bei ya cement ilianza ku-shoot tangu tuanza huu mwaka, ikimaanisha kwamba supply ya cement bado haitoshelezi mahitaji.
Supply of Cement = f(Demand from Government funded projects + Demand from Households + Demand for Export) |
Kwa hiyo, tunachokishuhudia kwa sasa kwenye soko la cement ni kwamba, output ambayo inazalishwa na viwanda vya cement kwa sasa, karibu yote inaliwa na mahitaji kutoa miradi ya serikali, na kupelekea kufubaza output ambayo inatakiwa ikauzwe kwenye soko la wananchi.
Ndo mana sasa unakuta kwa sasa, ukienda viwandani wanakuambia bei bado ni zile zile hazijabbadilika za kwenye Tzs 13,500 lakina hawana supply ya kukupa maana yote ipo booked na contractors wa hii miradi ya serikali, matokeo yake Cement pungufu inayoingia kwenye soko la wananchi inagombaniwa na wananchi na ku trigger profit seeking behaviour ya wafanyabiashara ambao wanacapitalise inefficiency ya soko kwenye demand na supply ili kujinufaisha. Kiuchumi.
Serikali amekuwa akitumia nguvu kubwa ya mabavu aliyonayo, kutoa vitisho kwa wafanyabiashara kwamba wao ndo chanzo cha kupanda kwa bei ya cement, na kusahau kabisa kwamba yenyewe serikali ndio imekuwa haitimizi wajibu wake kikamilifu.
- Haikutathmini uwezo wa uzalishaji wa cement kabla ya kutekeleza miradi mikubwa ya ujenzi, na
- Ame discourage uwekezaji wa kiwanda kikubwa cha cement cha Dangote, mtu ambaye ana capital muscles za kuwekeza na kuzalisha cement nyingi walau kukidhi mahitaji yaliyopo kwa sasa na yatayojitokeza mbeleni, ukizingatia bado Magufuli anatilia mkazo sekta ya ujenzi.
So, ni kwamba kuna mlima mkubwa sana wa kupanda kwa waziri wa ujenzi na viwanda wanaokuja, kuondoa uchafu wa serikali kwenye issue ya cement, ikwezekana, mwekezaji Dangote aitwe na serikali kwa hali ya dharura.
Ni mimi raia mkereketwa wa nchi ya chama kimoja.
N.Mushi