Mnapiga kura kama vipofu, halafu mnalalama kama vichaa!Waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi amesema serikali haina pesa waliokosa mkopo wazazi wao watafute namna.
source: ITV kipindi dakika 45 bado anaendelea na mahojiano
Ni kweli hata sisi vipofu tunaona serikali haina hela za kufanyia maendeleo ila za anasa inazo nyingi sana,NYAMBAFU.
Mh waziri kazungumza jana na niliridhika kwa maelezo ya kina ambayo aliyatoa. Ni kweli serikali inatumia pesa nyingi kutusomesha, tofauti na mataifa mengine. Pia bajeti ya mikopo imeongezwa, ni jitihada za wazi kuhakikisha vijana tunasoma. Nadhani nia ya serikali ni nzuri, uwezo ndo mdogo. Nashauri waziri apitie utaratibu wa kutoa mikopo upya uweze kuwabana wenye uwezo kupata mikopo tena kwa asilimia mia. Mimi ni mwanafunzi wa chuo kikuu, nimeshuhudia dosari hiyo. Wenye uwezo kwao ndio wanaopatiwa 100% na watoto wa wanyonge wanakosa au kupata mgao kidogo.
Umechukua hatua gani katika hili la wenye uwezo ndo wanapewa wasio na uwezo hawapewi. Kwa mfano mke wa RZ1 kapewa mkopo halafu masikini wanakosa! Pia mmeshafatilia pale bodi ya mikopo kunasemekana pale ukitoa rushwa unapata mkopo wala siyo issue maana wafanyakazi wa bodi ndiyo deals zao.
Tuna serikali moja tu na kwa maana hiyo kama serikali ingepitia mafungu ya wizara na kuangalia matumizi yasiyo ya lazima hela ingepatikana. Sasa hivi kuna upuuzi unaendelea kwa kila wizara kufanya maonesho ya miaka 50 ya uhuru! Hii ni mara ya pili wanafanya hivyo kwa sababu wiki ya utumishi wa umma kwa mwaka huu ilitumika kama maonesho ya miaka 50, lakini sasa wameona bado wanataka kuendeleza porojo.
Pia kuna hii tabia ya kushona sare na kofia hata kwa shughuli ndogo. Haya ni matumizi mabaya kwa nchi ambayo inasema haina uwezo wa kusomesha wananchi wake! Miaka 50 ya uhuru vipaumbele vya serikali ya ccm ni vipi?
nafikiri mh. waziri kawambwa yupo sahihi; muda wa bure sasa umekwisha, wazazi lazima wachangie; mbona harusi na sherehe nyingine zisizo na tija mnachangia? ila elimu kazi ya serikali peke yake! mbona hamnazo nyie!!!