Serikali, Habari na Makanjanja!

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
Katika vitu ambavyo bado naishangaa leo hii, ni Serikali yetu kuwa na Sheria ya Habari ambayo inalazimisha kuwepo kwa Waziri wa habari.

Nimejiuliza, kwa nini tunaendelea kuwa na Waziri Kamili ambaye anakuwa na Naibu Waziri, Katibu Mkuu na wataalamu kibao kwa shughuli ambayo si ya uzalishaji mali bali yahitaji mwongozo na uratibu wa cheo cha Kamisheni na kuongozwa na Kamishna au Mkurugenzi?

Nikiangalia jinsi Mamlaka ya Kodi livyo na kazi nyingi, ni heri basi kungekuwa na Waziri wa Kodi lakini si Waziri wa habari na Michezo!

Je tangu tupate uhuru wa pili baada ya kuzaliwa kwa Azimio la Zanzibar na Vyama vingi, kumekuwa na umuhimu gani wa kuwa na Waziri kamili na manaibu kwa ajili ya Habari, Michezo na utamaduni?

Hatuna miundombinu ya kuendeleza michezo na kufanya michezo iwe ni sehemu ya Uzalishaji mali, Utamaduni tunaupuuzia kuwa ni kujiliwaza na si kuweka kipaumbele kulinda Utamaduni wa asili na kutumia elimu kuboresha shughuli za Utamaduni, iwe ni maigizo, muziki, mila au desturi.

Jana Rais wetu Kikwete akifungua rasmi kuzaliwa kwa mara ya Tatu kwa TBC (Tanzania Broadcating Corportation) amesifia jinsi anavyoheshimu fani ya Uandishi wa habari. Nikajiuliza, kwa nini Serikali inaendelea kuwa na mashirika kama TBC na TVT? kwa madhumuni gani? Tayari tuna idara ya maelezo, Shihata ambayo ilikuwa ni sawa na Associated Press au Reuteurs imekufa, lakini Serikali inatumia kodi zetu kuwana na Magazeti, Tovuti na Redio?

Kwenye hii karne ya nano technology ambapo traditional media zinakufa kutokana na Internet, sisi bado tunakimbilia kutumia pesa za walipa kodi kuchapa magazeti? je mapato yanatoka wapi? Je Magazeti, redio na tovuti ya Serikali vinajiendesha kutoka pesa gani? je wanavianzio vvya pesa kibiashara amabzo si fungu la Bajeti?

Ndipo narudi kwenye kauli za Mheshimiwa Kikwete. katika kusifia uandishi, katoa tahadhari, onyo na kuonyesha kukwerwa kwa ke kwa habari ambazo ni za upande mmoja, ambazo zinamlena mtu mmoja au taasisi na kazipa jina la Ukanjanja.

Ametoa tamko rasmi kutaka udhibiti wa mfumuko wa Makanjanja na waandishi wawe waadilifu. Amekiri kukerwa sana na huu mfumuko wa Makanjanja!.

Nanukuu

WAVAMIZI wa taaluma ya habari maarufu kama makanjanja, wamemkera Rais Jakaya Kikwete ambaye sasa amewataka wanahabari kuwadhibiti ili kulinda heshima ya taaluma hiyo.

Rais Kikwete alisema hayo jana alipokuwa akizindua Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) katika sherehe zilizofanyika kwenye makao makuu ya shirika hilo, jijini Dar es Salaam.

"Mimi ni mmoja wa watu wanaounga mkono taaluma ya habari. Hivyo, msiiache ikachukuliwa na makanjanja. Nasema haya kutoka rohoni na nina nia njema," alisema Rais Kikwete.

Alisema wavamizi hao wamekuwa wakiivunjia heshima taaluma ya habari kwa kuandika habari za upotoshaji, uzushi na zilizoegemea upande mmoja, kwa nia ya kumbomoa mtu au taasisi kwa maslahi binafsi.

Alisema kama wanahabari wataruhusu taaluma hiyo kuvamiwa na makanjanja, watajuta baada ya kuanza kushambuliana wenyewe kwa wenyewe.

Alisema chombo cha habari kinatakiwa kutangaza habari sahihi na za kweli kama maadili ya taaluma yenyewe yanavyotaka kinyume chake, ni kutowatendea haki na kuwadharau wananchi.
Aliwataka wanahabari kutumia maadili ya taaluma hiyo na kuepuka uchochezi wa kidini na ukabila, lakini akawataka pia kutokuwa waoga na kuoneana haya katika mambo ya msingi yanayikera jamii na Watanzania kwa ujumla.

My first reaction was the saga tha led to Mike and Mac the JamboForums operative in ground zero to be arrested!

We live in a modern world where freedom of speech and opinion is the key. Our government is still operating and runs itself in medieval times, enzi za habari kutumia kopo na ngoma kwa chifu!

Uhuru wa habari (information) umefanya Watanzania tuwe mahuiri sana kuchangua mambo mengi mazuri na hata mabaya. Sikatai kuwa mara nyingine, uhuru wetu hukosa mwelekeo au uadilifu na kuishia kuonekana kana kwamba ni uzushi uzushi au ukosefu wa maadili.

Nikajiuliza, hivi Rais Kikwete akisoma ile mada yangu ya Screw Muungwana http://www.jamboforums.com/showthread.php?t=2204&highlight=screw+muungwana si atapata shinikizo na kuamuru nikamatwe na kuwekwa ndani?

Uhuru wa maoni ni haki ya kila mtu. Sheria za habari zinahusu habari na si maoni! Maoni ni mapokeo na makisio ya mtoa maoni, ndio maana yanaitwa maoni. Maoni yanaweza kuwa na nguvu kubwa za ushawishi hasa ikiwa maoni yanaandamana na vigezo na nyenzo ambazo zaonekana wazi machoni, masikioni na mawazoi pa wasomaji na wasikilizaji.

Maoni kuhusu udhauifu wa Serikali yetu kuhusiana na suala la IPTL,BOT-EPA, Richmond, Radar, Buzwagi, Madini, Kiwira, Uwajibikaji, Ufisadi ulitoka kwa hawa makanjanja na ni ujasiri wao ulioshinikiza Serikali ikae chini na kuamua kufanya ufuatiliaji ambao tayari tunaona matokeo yake.

Walichotumia Makanjanja ni vigezo halisi (facts and data) kuoanisha udhaifu, uzembe na hata ubadhrifu na uhujumu wa wazi ambao ulitishia usalama wa Taifa letu.

Kilichokera na nahisi kndiyo kiini cha kwako mheshimiwa Raisi kufoka kistaarabu, ni unazi wa makanjanja, tunashupalia kwa hali ya juu na hata kuwaumbua na kuwasurubu bila huruma wote ambao wanaelekea ni wazembe, dhaifu, wakiuka maadili na wabangaizaji, wewe ukiwa mmojawapo.

Hivyo basi, nakuomba ujifunze kwenda na wakati na kujua kuwa hatuko kwenye nyakati za Ujamaa au nyakati za Mtawala asemalo basi ni sheria na kila mtu alitetemekee. Ukisema kitu tutakichambua na kama umetoa pumba au ulaghai, tutakwambia wazi bila kuficha.

Wakasirikie wale wanaokudanganya kwa kusema "yes" kwa kila kitu, wao ndio wakosa maadili.
 
Good Drop Kishoka,

The local media are unable or unwilling to provide space for embarrassing and tedious issues such as democracy and constitution debates. Yet at the same time they eagerly act as willing and uncritical sounding boards for the various undemocratic and unaccountable quangos that run our country. This contrast reflects a deeper malaise.

JK was his own undoing, he (& his office) lied to the country about Ricmond,BOT,BUZWAGI,ATC debased the power of the parliament, allowed sleaze on a scale that is unbelievable and led us into a foreign adventure of which we will be lucky to extricate ourselves from in one or two years.

If I had to sit through 60 minutes of JK's patronising, disingenuous, self-aggrandising garbage, I'm afraid I might lose the will to live.Thats why i cant be bothered watching his hotuba kwa Taifa.

Like the tedious 'interviews' he grants to selected radio and TV programmes, you never emerge any the wiser.

That doesn't stop CCM's terracotta army clapping like seals, or political anoraks scouring the entrails for some deep, meaningful significance. Leave them to it.


In short i have given up on our North Korean style media. The best bet lies on blogs and sites like JF
 
Rev. unasema

"Kwenye hii karne ya nano technology ambapo traditional media zinakufa kutokana na Internet, sisi bado tunakimbilia kutumia pesa za walipa kodi kuchapa magazeti?"

Rev., kuna mambo nakubaliana nawe, lakini hebu eleza, una maana kwa kuingia kwa Internet basi vyombo vingine havina nafasi? Wapi? Hebu elezea kwa mfano, ni traditional media gani zinakufa kwa sababu ya kuibuka Internet? Are you serious? Kama wewe unaifahamu Tanzania, ni kwa kiwango gani Internet unayoisema imesambaa? watu wetu vijijini wataweza kuhudumiwa kwa Internet wakati umeme hakuna? Huko uliko wewe, magazeti na redio hakuna tena kwa sababu watu wote wanapata habari toka kwenye Internet? Wapi huko?

Redio, Magazeti, Majarida, televisheni na sinema bado vimeendelea kuwa vyombo muhimi vya mawasiliano kwa mwanadamu wa sasa hata baada ya teknlojia ya kisasa zaidi, yaani Internet kuingia. Hii inasababishwa na sababu mbali mbali ambazo zinatokana na asili na muundo wa vyombo hivyo katika kufikisha ujumbe kwa mlengwa.Kama hili nakosea naomba unieleze wewe unalionaje.

"je mapato yanatoka wapi? Je Magazeti, redio na tovuti ya Serikali vinajiendesha kutoka pesa gani? je wanavianzio vvya pesa kibiashara amabzo si fungu la Bajeti?"

Mfano mmoja tu, ni kwamba Daily News, kwa mara ya kwanza, mwaka 2007 wameipa serikali dividend ya sh. milioni 5 baada ya kuweza kujiendesha kwa faida. Kwa TvT na vingine, wameanza kujitegemea kibiashara japo sina rekodi za fedha zao, lakini hili pia liliongelewa sana mwaka jana juu ya umuhimu wa kujitegemea kiuendeshaji.

"Uhuru wa maoni ni haki ya kila mtu. Sheria za habari zinahusu habari na si maoni! Maoni ni mapokeo na makisio ya mtoa maoni, ndio maana yanaitwa maoni. Maoni yanaweza kuwa na nguvu kubwa za ushawishi hasa ikiwa maoni yanaandamana na vigezo na nyenzo ambazo zaonekana wazi machoni, masikioni na mawazoi pa wasomaji na wasikilizaji."

Pengine sijakuelewa hapo, lakini, hivi maoni binafsi na nguvu yake kubwa kama unavyoielezea, kama yakiwa na athari kubwa kwa umoja na usalama wa kitaifa, yanashughulikiwaje? hayabanwi kisheria? Unatofautishaje athari za habari na maoni?
 
ni lini tumewahi kusoma habari za uongo? yaani mtu amefabricate story... au tatizo lao ni maoni na siyo habari?
 
ni lini tumewahi kusoma habari za uongo? yaani mtu amefabricate story... au tatizo lao ni maoni na siyo habari?

When the Media becomes a tool for powerful individuals
Makwaia wa KUHENGA
Daily News; Thursday,March 27, 2008 @19:01

Said she: “An impression has steadily built up recently that some journalists were deliberately flouting journalistic ethics of standing for truth, facts and objectivity. For example, whereas everyone was there to see the colour of given shirt as black, these journalists would announce, quite to the astonishment of everybody; that the colour of that shirt was white!”

Eh! Bwana! Elaborating, Editor Nyaronyo Kicheere of Kulikoni newspaper gave a most current case in point. Said he: “When the immediate former Prime Minister recently left for his home district of Arusha after his resignation in parliament last fall, he was accompanied by a powerful brass from the Press Corp. What was reported subsequently in the print media was astonishing.

He went on: “It was reported that the former premier was received by a large motorcade involving dozens of cars and a crowd of more than 10,000 people. The actual truth was that the number of cars in the motorcade was not that big as mentioned in news- reports in some tabloids and the actual crowd not in the multitude mentioned.

“In fact, before the arrival of the former PM, there was a youth demonstration against ufisadi (lootocracy) in the country, but some of these tabloids never made any mention of these demonstrations by the youth of Arusha the morning preceding the arrival of the former premier.

Instead there were near-editorializing comments in these tabloids that while what they had reported about the former Premier’s “triumphant return” was mild - a more graphic and great or “kiboko” report would follow in subsequent editions,” said Editor Nyaronyo to my considerable bewilderment."
 
Rev. unasema

"Kwenye hii karne ya nano technology ambapo traditional media zinakufa kutokana na Internet, sisi bado tunakimbilia kutumia pesa za walipa kodi kuchapa magazeti?"
Rev., kuna mambo nakubaliana nawe, lakini hebu eleza, una maana kwa kuingia kwa Internet basi vyombo vingine havina nafasi? Wapi? Hebu elezea kwa mfano, ni traditional media gani zinakufa kwa sababu ya kuibuka Internet? Are you serious? Kama wewe unaifahamu Tanzania, ni kwa kiwango gani Internet unayoisema imesambaa? watu wetu vijijini wataweza kuhudumiwa kwa Internet wakati umeme hakuna? Huko uliko wewe, magazeti na redio hakuna tena kwa sababu watu wote wanapata habari toka kwenye Internet? Wapi huko?

Redio, Magazeti, Majarida, televisheni na sinema bado vimeendelea kuwa vyombo muhimi vya mawasiliano kwa mwanadamu wa sasa hata baada ya teknlojia ya kisasa zaidi, yaani Internet kuingia. Hii inasababishwa na sababu mbali mbali ambazo zinatokana na asili na muundo wa vyombo hivyo katika kufikisha ujumbe kwa mlengwa.Kama hili nakosea naomba unieleze wewe unalionaje.

"je mapato yanatoka wapi? Je Magazeti, redio na tovuti ya Serikali vinajiendesha kutoka pesa gani? je wanavianzio vvya pesa kibiashara amabzo si fungu la Bajeti?"

Mfano mmoja tu, ni kwamba Daily News, kwa mara ya kwanza, mwaka 2007 wameipa serikali dividend ya sh. milioni 5 baada ya kuweza kujiendesha kwa faida. Kwa TvT na vingine, wameanza kujitegemea kibiashara japo sina rekodi za fedha zao, lakini hili pia liliongelewa sana mwaka jana juu ya umuhimu wa kujitegemea kiuendeshaji.

"Uhuru wa maoni ni haki ya kila mtu. Sheria za habari zinahusu habari na si maoni! Maoni ni mapokeo na makisio ya mtoa maoni, ndio maana yanaitwa maoni. Maoni yanaweza kuwa na nguvu kubwa za ushawishi hasa ikiwa maoni yanaandamana na vigezo na nyenzo ambazo zaonekana wazi machoni, masikioni na mawazoi pa wasomaji na wasikilizaji."

Pengine sijakuelewa hapo, lakini, hivi maoni binafsi na nguvu yake kubwa kama unavyoielezea, kama yakiwa na athari kubwa kwa umoja na usalama wa kitaifa, yanashughulikiwaje? hayabanwi kisheria? Unatofautishaje athari za habari na maoni?

Mbalamwezi,

Inaelekea hujanielewa au uko katika mazingira ambayo bado yanategemea Serikali ifanye kila kitu.

Serikali kwa sasa kazi yake ni kupanga Sheria, kudhibiti. kuratibu, na kulinda Katiba. Serikali ina majukumu ya kutoa uhamasishaji, kukusanya mapato na kuhakikisha kuwa kuna mwamko wa uazlishaji mali, kujengwa kwa miundo binu na kuhakikisha kuwa Taifa linaendelea na nguzo za maendeleo na haki za watu kama afya, elimu, chakula, nyumba na kazi vinapatikana.

Ninachopinga ni suala zima la Serikali kuwa chombo cha habari, kutumia pesa za walipa kodi kuendesha magazeti, Redio na Tovuti. Nimehoji hata sababu na maan yeyote ya kuwa na Waziri wa Habari, ikiwa kazi ni kuratiibu.

Nilichokitolea mfano wa kukuwa kwa internet na kuuliza ni kwa nini Serikali itumie kodi kuuza magazeti? Kwa nini kazi ya kuuza magazeti, kuwa na Redio au Televisheni isiwe ni mashirika yanayojitegemea na kuwepo kwa ubia hata kwa wananchi na si kusubiri ruzuku ya serikali kujiendesha?

Wewe umesema Daily News ilipata mavuno ya Shilingi milioni 5 kwa mwaka 2007, je matumizi yalikuwa kiasi gani? Kwangu mimi hayo si mavuno ya kujivunia hata kidogo. Shillingi milioni 5 kwa mwaka ni mshahara wa watu 3 wakubwa wa idara kwa mwaka mzima!

So if these were dividends (from investments I presume) where is other source of capital? what are the expenses incurred?

Mimi niko Marekani, na nimeona jinsi gani magazeti na redio (95% of media is privately owned in US) ambavyo kila mwaka (for the past 10 years) yamekuwa yakipoteza mapato kutokana na internet, na inabidi wawe creative kuhimili matumizi na kuongeza mapato.

Sasa najiuliza kwanini Serikali yetu ambayo iliunda shirika na taasisi maalum kuuza mashirika kama ATC, TRC, Dawasco na hata kushindwa kutoa schorlaship kwa wanafunzi iendelee kufanya biashara ya magazeti? Kwa nini kazi hii wasiachiwe kina Mengi, Rostam na Ulimwengu?

KUhusu maoni, ikiwa utoaji mani ni pamoja na kutoa mianya ya ufupi wa mawazo au utendaji, utawekeaje maoni sheria? Mtoa maoni ni lazima ajijue kuwa kuna athari katika maoni na kama atakuwa mkosefu basi ni lazima ajue kuwa akivunja sheria, basi anastahili adhabu.

Maoni yangu kutamka wazi siridhishwi na utendajiwa Kikwete unataka yatungiwe Sheria gani? au unataka yadhibitiwe vipi ikiwa 90% ya kila nililosema sasa linaonekana wazi ni kweli mpaka wengine mwanipa cheo nisichostahili cha Unabii? J

ee nami nifungwe mdomo kwa kutoa maoni ambayo ni hisia za vipimo vyangu na akili zangu kuwa tuna uongozi mbovu?

Naomba utulie, halafu usome tena maoni yangu haya kuhusu habari na makanjanja ili unielewe vizuri. Na kama kukusaidia tuu, basi usitegemee kusoma Daily news pekee kujua kuwa print media duniani inaweweseka kujiuliza ni vipi itaweza ku-survice electroni media!
 
Nabii, kama unaona mimi nategemea kusoma Daily News pekee pengine nisingekutana na wewe humu JF, make no mistake about that.

Pengine sikuelewa vema au hukupresent vema hoja yako, lakini hatima ya yote ninachopata kwenye hoja zako ni kulinganisha hali ya maendeleo US media na bongo. Hapo nadhani utakuwa si sahihi, kwa sababu ya mambo kadhaa.

Enterprenuership ya bongo, kuna selfishness kubwa bila kujali consumer anapata value for money au la. Hilo ni kutokana na political background yetu, na wewe unajua. Leo hii, hao wote unaowataja kwamba wanaweza kuachiwa majukumu ya kuendesha media, unajua namna wanavyoziendesha? Nimekuwekea hiyo piece hapo juu uone namna wanasiasa wawekezaji wanavyoweza kutumia media zao kifisadi, na kuacha mlaji bila faida ya maana. Wengi wanataka media houses zi serve their own interests, as a result, hata habari za rural development hazipatikani kwa kuwa rural coverage haina faida. Wao wanaangalia faida tu. Faida zinapatikana kwa press yao kufanya mainly urban covarage, na si kuelezea habari za ukulima wa kisasa na umwagiliaji maji.

Hata wao private media pia hawataki kuikosoa serikali kwa sababu wanaogopa watakosa matangazo, ambayo ni muhimu kupata faida.

US unaotolea mfano, unajua ICT infrastructure jinsi ilivyoendelea. Leo hii Masasi na umeme wa dizeli kwa nyumba chache za mjini, Internet inaweza kuitishia RTD au Radio Free Afrika kwa news covarage? Na kwa elimu ipi Mtanzania wa kijijini akatumie Internet lkama chanzo cha habari?

Watoto wetu mijini wanafurahia Internet kwa kuangalia ngono badala ya masomo.

Huo mfano wa Daily News ni kujaribu kuonyesha namna mambo yanavyoweza kubadilika na tutaachana na kuzipa pesa taasisi za habari za serikali. Dont be mad about financial statements. Kama walikuwa wanategemea serikali 100%, na sasa wanajitegemea na kulipa dividends, huoni kama ni positive move?

NI kweli hata mimi sioni haja ya kuwa na mawaziri kama viongozi wa sekta ya habari, kwa sababu ulizozieleza.

Lakini the government should retain its mouthpiece for serving better its people.

Kuhusu kipengele cha maoni, i still do not gather what is ur point. Lakini nahisi unaongelea press freedom? Kama ni hilo, nadhani inabidi tuje na takwimu zinazoonyesha how much press freedom does the media at home enjoys, pengine ukilinganisha na nchi zingine. But what should be know ni kwamba press freedom is a must for press to work effectively, ikiwemo na wewe kutoa maoni. Lakini ujue kuwa in the world, hata huko US uliko, NO PRESS FREEDOM IS ABSOLUTE, kama ambavyo ungependa niamini.Ndiyo maana kuna media freedom, regulation, and ethics. Hayo yote ni kwa ajili ya kulinda haki za kisheria za wale wanaoandika, na wanaoandikwa.
 
Kuhusu kipengele cha maoni, i still do not gather what is ur point. Lakini nahisi unaongelea press freedom? Kama ni hilo, nadhani inabidi tuje na takwimu zinazoonyesha how much press freedom does the media at home enjoys, pengine ukilinganisha na nchi zingine. But what should be know ni kwamba press freedom is a must for press to work effectively, ikiwemo na wewe kutoa maoni. Lakini ujue kuwa in the world, hata huko US uliko, NO PRESS FREEDOM IS ABSOLUTE, kama ambavyo ungependa niamini.Ndiyo maana kuna media freedom, regulation, and ethics. Hayo yote ni kwa ajili ya kulinda haki za kisheria za wale wanaoandika, na wanaoandikwa.


Mkuu Mbalamwezi,

Unajua kuna vitu viwili ambavo ni muhimu sana kwa nchi yoyote ile iliyo na demokrasia ya kweli.

Vitu hivo ni haki na uhuru wa kupata habari (freedom of information) ambayo serikali inatakiwa ipitishe sheria (freedom of information act) na imuajiri kamishna ili asimamie utoa habari yoyote ile iwe ya siri ya serikali na mambo mengine kwamba mbunge gani anatumia vipi fwedha za posho na mali yake aliipata vipi na imesimama vipi.

Hapa kama pamefeli ambapo tumeona kwamba hata wanachama wa JF wanakamatwa kwa kisingizio cha kuvujisha habari kwa kukosekana haki yao ya kikatiba ya kupata habari na kuamua kuitafuta, ndio tunaona kwamba Tanzania bado hakuna haki ya kupata habari na ndio maana serikali ina uwezi wa kuwa-manipulate wale wananchi wa vijijini unaowasema kwa mambo mbalimbali na kwa ujinga wao wa kutokujua wao hupiga kura na kumpitisha mbunge huku wakijua au kutojua wazi kuwa ni fisadi.

Jambo lingine ndio lenye utata ni uhuru wa vyombo vya habari (freedom of press) ambao ndio unawafanza watu wawe na haki ya kupata habari yenye uhakika na kuielimisha jamii na ikaelewa.

Kwa mfano unapoandika habari kuhusu Tanesco na ujinga wao wa kutoiwezesha nchi yote ya Tanzania kupata umeme kwa miaka 47 iliyopita, baadae unapaswa kupata "data" zaidi kuhusu tathmini, upembuzi yakinifu kuhusu hali ya umeme kutoka kwa shirika lenyewe ambazo shirika hilo limekuwa likifanza kwa miaka yote hio na sio kuambiwa kwamba labda Dr Rashidi amesafiri na kupewa ahadi kibao na katibu muktasi wake.

Baada ya hapo ndio unamwambia mwananchi wa maeneo uliyoyataja kwamba hayana umeme kwamba ni kwanini hawana umeme.

Sasa Tanzania mimi nakubali kwamba tumepiga hatua lakini bado tupo nyuma mno.

Sasa namalizia kwa kusema kwamba katika demokrasia hiohio ilikuwa ni vizuri waandishi wa habari kwenda Butiama ili kupasha habari ya nini kinaendelea huko badala ya kuonekana wananusanusa tu.
 
Mkuu Mbalamwezi,

Unajua kuna vitu viwili ambavo ni muhimu sana kwa nchi yoyote ile iliyo na demokrasia ya kweli.

Vitu hivo ni haki na uhuru wa kupata habari (freedom of information) ambayo serikali inatakiwa ipitishe sheria (freedom of information act) na imuajiri kamishna ili asimamie utoa habari yoyote ile iwe ya siri ya serikali na mambo mengine kwamba mbunge gani anatumia vipi fwedha za posho na mali yake aliipata vipi na imesimama vipi.

Hapa kama pamefeli ambapo tumeona kwamba hata wanachama wa JF wanakamatwa kwa kisingizio cha kuvujisha habari kwa kukosekana haki yao ya kikatiba ya kupata habari na kuamua kuitafuta, ndio tunaona kwamba Tanzania bado hakuna haki ya kupata habari na ndio maana serikali ina uwezi wa kuwa-manipulate wale wananchi wa vijijini unaowasema kwa mambo mbalimbali na kwa ujinga wao wa kutokujua wao hupiga kura na kumpitisha mbunge huku wakijua au kutojua wazi kuwa ni fisadi.

Jambo lingine ndio lenye utata ni uhuru wa vyombo vya habari (freedom of press) ambao ndio unawafanza watu wawe na haki ya kupata habari yenye uhakika na kuielimisha jamii na ikaelewa.

Kwa mfano unapoandika habari kuhusu Tanesco na ujinga wao wa kutoiwezesha nchi yote ya Tanzania kupata umeme kwa miaka 47 iliyopita, baadae unapaswa kupata "data" zaidi kuhusu tathmini, upembuzi yakinifu kuhusu hali ya umeme kutoka kwa shirika lenyewe ambazo shirika hilo limekuwa likifanza kwa miaka yote hio na sio kuambiwa kwamba labda Dr Rashidi amesafiri na kupewa ahadi kibao na katibu muktasi wake.

Baada ya hapo ndio unamwambia mwananchi wa maeneo uliyoyataja kwamba hayana umeme kwamba ni kwanini hawana umeme.

Sasa Tanzania mimi nakubali kwamba tumepiga hatua lakini bado tupo nyuma mno.

Sasa namalizia kwa kusema kwamba katika demokrasia hiohio ilikuwa ni vizuri waandishi wa habari kwenda Butiama ili kupasha habari ya nini kinaendelea huko badala ya kuonekana wananusanusa tu.

I agree with you, and i agree with Kishoka too on such issues. But i still do not see the point of leaving the press to the private sector at this early stage, when our investors do not recognize the need for improving their services. When Kishoka talks about the Internet, na kuachana na media nyingine, kwa sababu US kuna kampuni ya magazeti mapato yake yamedrop over years, ndipo ninapomshangaa. Kwa Tanzania kufikia huko we still have a long way to go.

Kishoka, mimi ni msomaji sana wa habari. Lakini ili nijiridhishe na ninachokisoma, huwa nalazimika kusoma magazeti mengi na mchanganyiko, ili nijitengenezee balanced story.

Kila mtu anajua umuhimu wa press freedom, lakini ni wachache wanaojua kuwa press freedom is not absolute.
 
Mbalamwezi,

Mimi nauliza tena, kwa nini Serikali yetu inaendesha shughuli za utoaji habari kama kuuza magazeti, kuendesha redio na tovuti? Ikiwa vitu vya msingi kama elimu na afya Serikali inavikwepa, kwa nini ikimbilie habari ambazo mapato yake ni finyu ukiangalia kwa uwazi kuwa ni Serikali ambayo hugharamia kila kitu na kuambulia ndururu?

I do not hava problem with private sector owning media outlets, let them spend their money and be creative on that. But I will have a beef at this time and age when government spends Tax payers money to run media.

Government job is to regulate and govern not to run the actual day to day activities. Rais ateue Wakurungenzi wakuu wa Daily News, TBC na TVT, it means Serikali inawajibika na gharama hizo!

Let Daily News, TBC, TVT and Shihata run independently from government aorm and protection and be as competitive as IPP, Free Media, Uhuru, Kulikoni, Mtanzania, DTV and other media outlets!

Serikali inaweza kutoa taarifa kwa vyombo vya habari. Ndio maana hata Rais ana mwandishi habari, mwandika hotuba na kitengo kizima cha habari au kama wanavyouita Mawasiliano. Zaidi, si kuna gazeti maalum la serikali ambalo machapisho yote muhimu hufanywa?

CCM wana Uhuru na Mzalendo, they have to be creative to get revenue in addition to print daily sales! Wakienda hazina kuzichota, nitagomba.

Hivyo vbasi narudia hujanielewa au kama umenielewa, basi unaridhia kwa Serikali kufanya biashara ya kuuza magazeti!

La mwisho, si nia yangu kulinganisha Media ya marekani na ya Tanzania. Nimetumia mifano hai na labda kosa langu ni kutumia Marekani kusema kuwa Print media, inapoteza nguvu na umaarufu kutokana na Electronic media! Jambo hili la watu kuachana na print media ni la kweli na hata huku Tanzania kwa taarifa yako, Watu wa Raia Mwema pamoja na kuwa wana uwezo wa kutoa gazeti lao mtandaoni kabla ya kugusa mtaani, wanaonelea wachelewe japo kwa siku moja na nusu ili yale ya mtaani (print) yanunuliwe na hivyo kupunguza kiu ya wale walioko Tanzania wenye access kwenye Internet kusoma gazeti wavuni lwa bure na si kununua magazeti!

So do not get me wrong on that at all, kutumia mfano wa Marekani ni kigezo tuu, kuashiria tunakokwenda print media haina nguvu na ndio maana nauliza katika uwanja huu wa fujo wa kubana matumizi, kwa nini serikali iendelee kuwa na mashirika ya habari?
 
I agree with you, and i agree with Kishoka too on such issues. But i still do not see the point of leaving the press to the private sector at this early stage, when our investors do not recognize the need for improving their services. When Kishoka talks about the Internet, na kuachana na media nyingine, kwa sababu US kuna kampuni ya magazeti mapato yake yamedrop over years, ndipo ninapomshangaa. Kwa Tanzania kufikia huko we still have a long way to go.

Kishoka, mimi ni msomaji sana wa habari. Lakini ili nijiridhishe na ninachokisoma, huwa nalazimika kusoma magazeti mengi na mchanganyiko, ili nijitengenezee balanced story.

Kila mtu anajua umuhimu wa press freedom, lakini ni wachache wanaojua kuwa press freedom is not absolute.

So in other words, you want Government to control media and run day to day business of media. I am glad you have come out and show your stance.

Here is a question to you, if you want Serikali to run Media, mbona tunakimbilia kuuza kila kitu? Wasn't it too early to sell TBL, TOL, Sigara (mind you these were profitable) ATCL, TRC and allowing TTCL and Tanesco to go through stiff competition of those who have money? Mbona Serikali haipeleki subsidies kwa tanesco na TTCL tena?

I have no problem with government as regulator, I have a big problem with government running business.


Yes I concur that Freedom of press has its limitations and I respect that and live by that even when airing my opinions!
 
So in other words, you want Government to control media and run day to day business of media. I am glad you have come out and show your stance.

Here is a question to you, if you want Serikali to run Media, mbona tunakimbilia kuuza kila kitu? Wasn't it too early to sell TBL, TOL, Sigara (mind you these were profitable) ATCL, TRC and allowing TTCL and Tanesco to go through stiff competition of those who have money? Mbona Serikali haipeleki subsidies kwa tanesco na TTCL tena?

I have no problem with government as regulator, I have a big problem with government running business.

Yes I concur that Freedom of press has its limitations and I respect that and live by that even when airing my opinions!

Mkuu Kishoka, nadhani ukianzisha mambo ya ubinafsishaji hapa inabidi twende kwa mapana yake pia, ila kwa urahisi zaidi anzisha thread ya faida za ubinasfishaji tuweze kuichambua kirahisi. Kuna faida na hasara za ubinafishaji, na ili tuelewane inabidi iwe thread nyingine. otherwise this gonna be an extra wide discussion which is also tiresome.

Just a quick question, unakumbuka kasheshe ya kupata bia kwa ajili ya sherehe ilivyokuwa kasheshe? Ilikuwa sababu gani? what is the situation now? Thread hii haitoshi kwa mambo hayo anyway.

Sijasema serikali i control media at any time, kwani huo utakuwa wehu. Lakini hata hivyo, media bila regulations ni harmful kwa kila mtu, hata kwa media media yenyewe.

Tunategemea kwamba hata tunapotunga sheria za media, tuna haki ya kugomea sheria kandamizi, this is what i mean. Hatuwezi ku escape regulation of media.

Serikali inaweza kuendelea kuwa na vyombo vyake vya mawasilano as government mouthpiece. Sasa hivi tunawashinikiza akina Salva watengeneze website tupate taarifa, wewe unasema haina haja ya kuwa na government website?

Hata hivyo, naielwa hoja yako katika sehemu kuu mbili: Serikali isimiliki media kwa kuwa ni ku waste taxpayers' money, au serikali izifanye media zake zijiendeshe profitable, na pengine hata kwa kukaribisha ubia. Is this right?

I would prefer the later, kwa sababu ni serikali tu inayoweza kulazimika kulinda interest za minorities katika mass communication. Kama nilivyoeleza awali, kuwaachia entirely private investors wa habarishe umma wa vijijini juu ya ukulima wa kisasa ni ndoto, na pia hawawezi kuandika juu ya tani 120 za mchele mbovu ulioingizwa bandarini tayari kupelekwa sokoni kwa kuwa wanalindana.
 
Serikali inaweza kuendelea kuwa na vyombo vyake vya mawasilano as government mouthpiece. Sasa hivi tunawashinikiza akina Salva watengeneze website tupate taarifa, wewe unasema haina haja ya kuwa na government website?

Hata hivyo, naielwa hoja yako katika sehemu kuu mbili: Serikali isimiliki media kwa kuwa ni ku waste taxpayers' money, au serikali izifanye media zake zijiendeshe profitable, na pengine hata kwa kukaribisha ubia. Is this right?

I would prefer the later, kwa sababu ni serikali tu inayoweza kulazimika kulinda interest za minorities katika mass communication. Kama nilivyoeleza awali, kuwaachia entirely private investors wa habarishe umma wa vijijini juu ya ukulima wa kisasa ni ndoto, na pia hawawezi kuandika juu ya tani 120 za mchele mbovu ulioingizwa bandarini tayari kupelekwa sokoni kwa kuwa wanalindana.

Mbalamwezi,

Kuna Government Gazette, ambako machapisho ya Serikali hutoka. Mimi sijasema Serikali isiwe na website za wizara kutoa taarifa mbali mabli.

Narudia tena, NAPINGA SERIKALI KUENDESHA MAGAZETI (DAILY NEWS/HABARI LEO), TBC(RTD) n TVT!

When you talk about Serikali safegurding interests of minorities, you mus be joking if the minorities you talk about is the majority of Watanzania who are wakulima. But if the minorities you talk about are Mafisadi who have always enjoyed protectionism, I will have to buy your argument!
 
rev kishoka

naomba nikuulize,NENO MAKANJANJA maana yake nini kiswahili sanifu?baadae naomba unipe hilo neno kwa kimombo ili niweze kugoogle nione tafsiri yake ikoje.
 
Mbalamwezi,

Mimi nauliza tena, kwa nini Serikali yetu inaendesha shughuli za utoaji habari kama kuuza magazeti, kuendesha redio na tovuti?...

I do not hava problem with private sector owning media outlets, let them spend their money and be creative on that. But I will have a beef at this time and age when government spends Tax payers money to run media....

Government job is to regulate and govern not to run the actual day to day activities. Rais ateue Wakurungenzi wakuu wa Daily News, TBC na TVT, it means Serikali inawajibika na gharama hizo!

Let Daily News, TBC, TVT and Shihata run independently from government aorm and protection and be as competitive as IPP, Free Media, Uhuru, Kulikoni, Mtanzania, DTV and other media outlets!

Serikali inaweza kutoa taarifa kwa vyombo vya habari. Ndio maana hata Rais ana mwandishi habari, mwandika hotuba na kitengo kizima cha habari au kama wanavyouita Mawasiliano. Zaidi, si kuna gazeti maalum la serikali ambalo machapisho yote muhimu hufanywa?

Kishoka, this is a very interesting topic. Ila inahitaji tuwe waangalifu kwa kujadili hoja. Hoja hizi ziwe zinachambuliwa kwa uwazi, not in a blanket form. So far, kwa hayo maelezo yako ya hapo juu, sijaelewa kama unachopinga ni serikali kuwa na vyombo hivyo, au serikali kuviendesha?

Maana kuna tofauti kubwa katika hayo mawili. Unaweza kumiliki chombo cha habari bila kukigharamia, ukakiacha kijiendeshe kibiashara. Au unaweza kukipa ruzuku ili kisizamie sana katika biashara na kifanye kazi za umma.

Lakini, nikufahamishe kuwa katika sekta ya habari, the prime objective kwa serikali (si Tanzania tu) ku own media ni ku serve its interests upon its people, japo serikali nyingi huchukulia pointi hii kama ya kuzibia midomo jamii,na kufanya solely propaganda.

In this respect, hatuwezi kusema serikali inafanya biashara ya kuuza magazeti, kwa kuwa the prime objective ni kufacilitate tunachokiita mass communication. Kuuza magazeti inatokana na ukweli kuwa the cost involved has to be recovered. Meeting production costs haina maana kuwa biashara. Biashara involves profit aspirations.

Do me a favour, unijibu swali hili tu: hili government Gazzette umewahi kulisoma wewe? Ni la habari zipi categorically?

Ndiyo maana nikakuuliza ndugu yangu, kuwa unachosimamia katika hoja yako pana hasa ni kipi? Matokeo yake unasema tu unapinga serikali kuwa na TvT,Daily News, Tovuti (japo hili umekuja kurekebisha baadaye)nk.

Ukitaka kujua kwa kina athari za kuacha private sector peke yake i facilitate mass communication, inabidi uelewe kwa kina namna private media zinavyo serve the public interest.


Moja ya sifa kubwa ya effective media ni kuweza ku serve public interest, who are also the consumers.

Na pengine unahitaji kufahamishwa kwa kina what is the impact of media in society, na media inaserve vipi hii society. From there you will need to know media ownership, government owned media, private owned media, faida na hasara za upande katika kupeleka ujumbe na mambo mengine mengi.

Kama thread yako unataka inufaishe wachangiaji, twende hoja kwa hoja, usiseme tu kuwa hutaki hiki hutaki kile. Tukifika hapo, basi utakkuwa hutaki tu na nitashindwa kukujibu.

Hivi BBC kwa sasa hivi ownership ikoje? the last time i heeard ilikuwa inafanyiwa ownership restructuring?
 
Back
Top Bottom