Tetesi: Serikali fanyeni tafiti kwenye samaki na mazao ya shamba ongezeko la wagonjwa wa saratani(cancer) kanda ya ziwa

ni kweli kuna idadi kubwa ya wagonjwa wa kansa hasa Bunda ni vema serikali ifanye utafiti kwani kinga ni bora kuliko tiba

Inaelekea kuna katatizo kakubwa huko kanda ya ziwa kanakohusu Cancer, lakini pia kama waliwahi kukana kuwa wanakula mapanki ya samaki iliyoonyeshwa ndani ya "Darwins Nightmare" kwanini matokeo hayo tuyategemee ktk mustakabali wa Cancer study inayoombwa hapa?
 
Ninahisi matumizi holela ya kemikali kama zebaki na nyinginezo zile za kusafishia madini migodini au zinazo tumiwa na wachimbaji wadogo wadogo wa madini, inawezekana hizo ndiyo huchafua mazingira mashambani, mitoni na ziwani.

Ningeshauri serikali ifanyie tafiti juu ya samaki toka ziwa Victoria, mito yote kanda hiyo unaweza kukuta jambo la kushitua.

Tafiti iende mbali na kuchunguza pia mazao toka mashambani mikoa yote ya kanda ya ziwa.

Kama chanzo kinaweza kuwa hicho nilichohisi basi tatizo linaweza kusambaa miji mikubwa kama Dar es Salaam, Dodoma, na mikoa mingine wanayo tumia samaki toka ziwa Victoria kama Sato, Sangara na Dagaa.

Sio vibaya wakichunguza na dawa za mifugo pia.

Serikali ichukue hatua tusisubiri janga kubwa.

Angalizo: Sijasema samaki wa ziwa Victoria wana tatizo.

Bandiko hili limechochewa na hoja hiyo hapo chini kama alivyochangia mjadala flani ndugu Subisubi humu jukwaani JamiiForums.


CC: Mh. Rais John Pombe Magufuli, Maskamu wa raisi Bi SSS, Waziri Mkuu MKM, Waziri wa Afya, Waziri wa Kilimo, Waziri wa Uvuvi,..., .., NEMC, .. et al.

UPDATES:
Kuna baadhi ya hoja za kisiasa kama hizo hiyo hapo chini tuziepuke zitatupotosha


Tukianza kulipa sura ya ukabila au ukanda jambo hili tutakosea sana.
  • Sisi wengine wa kanda mbali mbali tunakula samaki wanaotoka maeneo ya kanda ya ziwa.
  • Madukani tunanunua mchele toka mkoa wa Shinyanga kama ule mchele wa Kahama.
  • Tunakula ndizi toka kanda ziwa kama zile za Bukoba.
  • Tunakula nyama ya ng'ombe toka kanda hiyo.
  • Tunakula viazi vitamu toka kanda hiyo.
  • Tunatumia asali toka kanda hiyo.
  • Tuna ndugu zetu wanafanya kazi na kusoma kanda hiyo.
  • Tuna ndugu zetu wanaishi na kufanya biashara kanda hiyo.
  • Chakula cha kuku kinawekwa dagaa wanaotoka kanda hiyo, na baadae sisi tunakula hao kuku au mayai yao, kama unajua ABC za sayansi basi utajua hatupo salama wote tuliopo ktk huo mnyororo wa chakula(food chain).

Ubaguzi na siasa zitatumaliza ...

Walaji wa mchemsho wa samaki(sato) hapa DSM na mikoa mingine wengi ni wa kabila tofauti na wasukuma.
Na isiwe mwanza tu, maana lile ziwa ni kubwa na linahusisha mikoa kadhaa. KAMA UNAHISI TU SAWA HAKUNA TATIZO,ILA KAMA NI KWELI KUNA HAYO MAMBO HAKIKA HATA SOKO LA HAO SAMAKI LITAATHIRIKA VIBAYA MNO.....
Ushauri wangu ni kwamba kuliko kuropoka na kuandika hovyo ni bora ukaripoti kwenye mamlaka husika.
 
Bahari ndo inajaa uchafu haswa
Sidhani kama samaki wanahusika na Cancer
Maoni yako mazuri mkuu,
Mimi na akili yangu ya kawaida ukichanganya na elimu yetu ya shule za serikali, tena zile za ufundi ambazo walifuta somo la baiolojia na jiografia nikasema baharini maji ni mengi mno inapunguza concetration ya sumu, pia yale machumvi ya baharini huenda kidogo yanapunguza nguvu ya sumu.

Muhimu hapo serikali ifanye tafiti na baharini.
Ahsante mkuu.
 
Na isiwe mwanza tu, maana lile ziwa ni kubwa na linahusisha mikoa kadhaa. KAMA UNAHISI TU SAWA HAKUNA TATIZO,ILA KAMA NI KWELI KUNA HAYO MAMBO HAKIKA HATA SOKO LA HAO SAMAKI LITAATHIRIKA VIBAYA MNO.....
Ushauri wangu ni kwamba kuliko kuropoka na kuandika hovyo ni bora ukaripoti kwenye mamlaka husika.
Ninahisi tu, hakuna haja ya kuwatisha watu.
Wakati naandika hili bandiko nilikuwa nakula hao samaki na nimetoka kupokea mzigo mwingine.

Pale ktk hoja kuu nimeshauri madawa ya mifugo, na mazao ya shamba yachunguzwe pia.

labda waende mbali na kuchunguza tabia za wahanga mfano matumizi ya vyombo vya plastiki kwa kuwekea vyakula vya moto, au kuweka juani inaweza kusababisha gesi za sumu zinazochangia saratani.

Matumizi ya madawa ya asili(mimea) ya mimea flani kupita kiasi huweza kusababisha saratani, wengi hili hatulijui lakini kuna mimea tunaitumia sana kama dawa za tumbo na vidonda kumbe ukizidisha ni hatari.
 
Elimu kuhusu madhara ya kemikali za migodini na dawa za kuua viatirifu Wananchi wengi hawana elimu ya kutosha. Wakazi wengi wa kanda ya Ziwa wanalima zao la Pamba na kitu ambacho ni kibaya wanachangamya na mazao mengine kama mahindi na maharage. Tatizo linakuja pale wanapotumia madawa makali kuulia viatirifu zinaathiri mazao kama Mahindi au Maharage pia kinaweza kuwa chanzo cha magonjwa mengi ya Kansa.
Pia kuna baadhi ya wakulima wanaolima mazao kama Kabeji(Cabbage) kando kando ya Ziwa wakati Kabeji zinachanua wanatumia madawa makali ya Pamba,wakati Kabeji inapojifunga dawa inakuwa ndani ya kabeji hadi inapokomaa.Hivyo basi kwa matumizi yasiyo sahihi ya madawa ya kuua viatirifu kwa mazao ambayo hayaitaji madawa makali au dawa ambazo zinachukua muda kupoteza makali nadhani pia inaweza kuwa chanzo cha magonjwa ya Kansa.
Kuna ulazima wa hizi taasisi kutoa elimu na kufanya ukaguzi kila wakati ili kuondoa hatari za visabishi vya Kansa na pia Serikali/Bunge iwape fedha za kutosha kwa ajili ya kufanya tafiti.
 
Bahari ni dampo kuu la taka chafuzi duniani hiyo ndio tofauti na hayo maji ya ziwa yana ishia baharini kupitia mto nile

Sasa ningependa tofauti hiyo ndio ukaihusisha na maudhui ya huu uzi.
Hilo ndio lengo hasa la kutaka utafiti ufanyike.
 
Elimu kuhusu madhara ya kemikali za migodini na dawa za kuua viatirifu Wananchi wengi hawana elimu ya kutosha.
Wakazi wengi wa kanda ya Ziwa wanalima zao la Pamba na kitu ambacho ni kibaya wanachangamya na mazao mengine kama mahindi na maharage. Tatizo linakuja pale wanapotumia madawa makali kuulia viatirifu zinaathiri mazao kama Mahindi au Maharage pia kinaweza kuwa chanzo cha magonjwa mengi ya Kansa.
Pia kuna baadhi ya wakulima wanaolima mazao kama Kabeji(Cabbage) kando kando ya Ziwa wakati Kabeji zinachanua wanatumia madawa makali ya Pamba,wakati Kabeji inapojifunga dawa inakuwa ndani ya kabeji hadi inapokomaa.Hivyo basi kwa matumizi yasiyo sahihi ya madawa ya kuua viatirifu kwa mazao ambayo hayaitaji madawa makali au dawa ambazo zinachukua muda kupoteza makali nadhani pia inaweza kuwa chanzo cha magonjwa ya Kansa.
Kuna ulazima wa hizi taasisi kutoa elimu na kufanya ukaguzi kila wakati ili kuondoa hatari za visabishi vya Kansa na pia Serikali/Bunge iwape fedha za kutosha kwa ajili ya kufanya tafiti.
Mkuu umeleta hoja nzuri sana sana.
Matumizi ya madawa ya kuuwa wadudu shambani (sijui wanaita ni viwatilifu) na mbolea mbalimbali.

Kuna dawa flani ya copper imeuwa baadhi ya watu kwa saratani maeneo wanayolima kahawa. Wanatumia bila vifaa vya kujikinga kama gloves, mask, n.k.

Pia kuna mbolea flani sitaitaja sababu za kibiashara, imeandikwa wazi unapochanganya tumia mask na gloves maalum kuepuka madhara. Tatizo elimu ya wakulima wengi ni ndogo hupuuza haya maelekezo.
Ndani yake kuna phosphorus ambayo inasababisha matatizo kwa watoto ambao hawajazliwa kwa wamama wajawazito, au inaweza kuzuwia kuzaa kabisa, nadhani hii inaitwa teratogenic chemical.
Juu ya yote hii kemikali pia ni mutagenic, teratogenic or carcinogenic, nephrotoxic, myelotoxic, or pneumotoxic.

Kuna hoja pia ya watu kutumia madawa kama ngao ya kutibu vyandarua vya mbu kutibu magonjwa sugu ya zao la nyanya. Angalizo hii ni tuhuma inaweza kuwa ni uzushi tu.

Mtanisamehe kwa maelezo mengi na marefu mno lakini hii yote ni ktk kujadili na kuwahabarisha wenye dhamana.
 
Back
Top Bottom