Serikali/CCM: Mtazikwepaje hasira zetu kwa uzembe huu!

Waacheni tu CCM wazidi kujizika wenyewe, na hapo sijui hata kama watajinusuru na ghadhabu ya wananchi.
Sasa kwa akili timamu eti nchi ina miaka 50 ya uhuru shule zimechoka namna hii kweli?

NYIE CCM nawauliza kweli namna hii? eti wewe JK unayelia lia na kabla dhahma haijakukuteni tuambie mmefanya nini miaka yote hii? Nchi uchumi mbovu, hebu niambieni CCM, mikoa ya kusini gridi ya taifa haijafika miaka 50 ya uhuru kweli? Mikoa ya magharibi gridi ya taifa haijafika kweli nchi hii itaendelea? sasa umeme ndo huo mmewapa mafisadi na Dowans ndo kila kitu kweli uchumi wa nchi hii utaimarika?

Wewe Pinda unajidai muungwana wakati unatetea mafisadi sitaki kukusikia ni chui ktk ngozi ya kondoo. kwa nini tupate shida kwa ajili ya kikundi cha watu wachache hawa?

Please CCM ondokeni kwa amani mmeshindwa kuongoza nchi hii, mnakashfa nyingi sana kuanzia za Loliondo, mpaka leo Dowans, hakuna mwana CCm anaytetea maslahi ya wananchi leo wanatetea mafisadi tuuu
 
Eti mkurugenzi wa halmashauri anashindwa kuzungumzia suala hili nyeti kisa yuko kwenye kikao cha maandalizi ya mbio za mwenge...UPUUZI!ye anajali sana mbio za mwenge kuliko maendeleo ya elimu!Mwenge unamsaidia nini mwananchi,mlalahoi wa nchi hii zaidi ya kulazimishwa kuuchangia?AIBU HII....

Yeye anafaidika na mbio za mwenge, aende zake huko MKURUGENZI BONGO!?!?
 
Madarasa mawili wasomea chumba kimoja

Saturday, 05 March 2011


balaatz.jpg

Wanafunzi wa darasa la pili na tatu wa shule ya Msingi Magwalasi katika Kata ya Rujewa, wilayani Mbarali, mkoani Mbeya wakiwa darasani wakiendelea na masomo kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa shule hapo imewalazimu chumba kimoja kutumiwa na wanafunzi wa madarasa mawili kwa kila darasa kugeukia upande wake kama walivyokutwa na mpigapicha wetu jana. Picha na Brandy Nelson

Brandy Nelson, Mbarali

UHABA wa vyumba vya madarasa umewalazimu wanafunzi wa madarasa tofauti katika Shule ya Msingi Magwalasi iliyoko Kata ya Rujewa wilayani Mbarali, Mkoa wa Mbeya kusoma katika chumba kimoja kwa kugeuziana migongo.

Waandishi wa habari walifika hapo jana na kukuta shule hiyo yenye wanafunzi 269 na walimu saba wa kuanzia chekechekea, darasa la kwanza hadi la saba ikiwa na vyumba vinne pekee vya madarasa.


Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Jonathan Chengula aliwaambia waandishi wa habari kuwa katika shule hiyo iliyoanza na kusajiliwa mwaka 2003, wanafunzi wa darasa la kwanza wanasoma chumba kimoja kwa wakati mmoja na wale wa chekechea, darasa la pili wanasoma pamoja na wenzao wa darasa la tatu, la sita na la tano, huku wale wa darasa la saba wakitumia chumba kimoja na wa darasa la nne.


“Tatizo kubwa ambalo linatusumbua katika shule yetu ni upungufu wa madarasa. Tuna madarasa manne tu hivyo imetulazimu kuweka mbao za kufundishia mbili katika chumba kimoja ili madarasa mawili yaweze kutumia kwa wakati mmoja,” alisema.


Kwa mujibu wa mwalimu mkuu huyo, ili kukabiliana na upungufu huo wa madarasa na kutokana na mazingira ya shule hiyo, ndiyo maana wameramua wanafunzi wa madarasa mawili tofauti wasome katika chumba kimoja kwa kugeuziana migongo kwa maana ya kuwa wengine wanageukia upande wa kulia na wengine kushoto.


“Kama mnavyowaona hawa waliogeukia huko ni darasa la saba na hawa wengine ni darasa la nne na katika darasa hili jingine wanasoma darasa la pili na tatu ndivyo tunavyo kwenda," alisema.Alisema kuwa mwalimu wa darasa la saba anapoingia kufundisha, wa darasa la nne anasubiri mwenzake amalize huku wanafunzi hao wa darasa la nne wakiwemo humo humo ndani wakisikiliza wale wa darasa la saba wanavyofundishwa.


Alisema wakati mwingine walimu huamua kuwatoa nje na kuwaweka chini ya mti kama umefika wakati wa kusoma kitabu cha Kiswahili ili wasome wakiwa nje na wengine waendelee na masomo.

Mwalimu aliyekuwa darasani akifundisha, Shufaa Ramadhani alisema mazingira hayo ya ufundishaji ni magumu kwani kuna athari kubwa kwa wanafunzi na upande wa mwalimu kwani kufundisha wote kwa pamoja pia ni vigumu.

Alisema kuwa utaratibu huo unawaathiri watoto kisaikolojia kwani kuna uwezekano wa kusahau yale ambayo wamefundishwa na mwalimu wao na badala yake kusikia ya upande wa pili ambayo ni masomo ya darasa jingine ambalo tayari walishayapitia au bado hawajapitia.


Mwalimu Shufaa alisema walimu wanaathirika kwa kupoteza vipindi vingine kwa mujibu wa uandaaji wa masomo na vipindi kwani inamlazimu asubiri mwenzake amalize kufundisha na ndipo aingie na kufundisha somo lake.


Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali, George Kagomba hakupatikana kuzungumzia tatizo hilo na alipotafutwa kwa simu alijibu kuwa yuko kwenye kikao cha maandalizi ya Mbio za Mwenge.


Mkurugenzi huyo aliwataka waandishi kwenda kwa Ofisa Elimu wa Wilaya ya Mbarali. Hata hivyo, aliyekuwa akikaimu ofisi hiyo hakuwepo. Ofisa elimu wa Wilaya alikuwa amesafiri kikazi


My take:
Je hivi ndivyo tunavyowaandaa watoto wetu kwa ushindani katika dunia ya leo? Je matatizo ya madarasa yamesababishwa na kupanda bei za mafuta wiki mbili zilizopita?

Chadema wanaposema hali hii haifai, wanakuwa wamechochea vurugu gani? Kama serikali ina vyombo vya kuishughulikia Chadema, kwanini nguvu hizo zisielekezwe kwenye mambo muhimu kama haya?


Kwanini serikali ipate kiwewe na mikuatano ya ''porojo'' ya Chadema na isipate kiwewe na hatari hii inayo onekana bila microscope. Hivi wananchi wenye watoto katika shule hii kwanini wasiwe na hasira na serikali yao, eti hasira inatokana na maandamano ya Chadema!!

Yan inasikitish sana, sasa hapo ni shule au vurugu tu, nashukuru sana maendeleo ya teknologia, cause haya tungeyaona wapi tungeishia kudanganywa na propaganda za mafisadi, ccm watajibeba mwaka huu, maana wamebanwa haswa, na wale kina mama wakatoliki wa songea washauriwe kujiunga na jamii forums huenda wakawa na akili zaidi, maana naona walizonazo zinawatosha kuvukia barabara tu. Aibu kubwa kwa Tanzania nimesikitika sana.
 
kwa maisha tunayoishi hakuna haja ya kwenda jehanamu tunaomba mungu hatusamehe coz maisha yetu ni adha bu tosha
 
niwakumbushe kauli moja ya Makamba aliyoitoa Tarime wakati wa uchaguzi mdogo wa ubunge ambapo alisema watanzania lazima wajifunze kuuchukia umaskini na wao ndani ya CCM wameanza na viongozi kwanza kuuchukia na ndo mana mijitu inakula pesa za nchi hii bila huruma hadi inaota nundu na watoto na wadogo zetu wanaishia katika hali hiyo. Nimekasrika sana ngoja nikanywe banana moja ntarudi......
 
balaatz.jpg

Wanafunzi wa darasa la pili na tatu wa shule ya Msingi Magwalasi katika Kata ya Rujewa, wilayani Mbarali, mkoani Mbeya wakiwa darasani wakiendelea na masomo kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa shule hapo imewalazimu chumba kimoja kutumiwa na wanafunzi wa madarasa mawili kwa kila darasa kugeukia upande wake kama walivyokutwa na mpigapicha wetu jana. Picha na Brandy Nelson

DOWANS, EPA, MEREMETA etch



Brandy Nelson, Mbarali

UHABA wa vyumba vya madarasa umewalazimu wanafunzi wa madarasa tofauti katika Shule ya Msingi Magwalasi iliyoko Kata ya Rujewa wilayani Mbarali, Mkoa wa Mbeya kusoma katika chumba kimoja kwa kugeuziana migongo.

Waandishi wa habari walifika hapo jana na kukuta shule hiyo yenye wanafunzi 269 na walimu saba wa kuanzia chekechekea, darasa la kwanza hadi la saba ikiwa na vyumba vinne pekee vya madarasa.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Jonathan Chengula aliwaambia waandishi wa habari kuwa katika shule hiyo iliyoanza na kusajiliwa mwaka 2003, wanafunzi wa darasa la kwanza wanasoma chumba kimoja kwa wakati mmoja na wale wa chekechea, darasa la pili wanasoma pamoja na wenzao wa darasa la tatu, la sita na la tano, huku wale wa darasa la saba wakitumia chumba kimoja na wa darasa la nne.

“Tatizo kubwa ambalo linatusumbua katika shule yetu ni upungufu wa madarasa. Tuna madarasa manne tu hivyo imetulazimu kuweka mbao za kufundishia mbili katika chumba kimoja ili madarasa mawili yaweze kutumia kwa wakati mmoja,” alisema.

Kwa mujibu wa mwalimu mkuu huyo, ili kukabiliana na upungufu huo wa madarasa na kutokana na mazingira ya shule hiyo, ndiyo maana wameramua wanafunzi wa madarasa mawili tofauti wasome katika chumba kimoja kwa kugeuziana migongo kwa maana ya kuwa wengine wanageukia upande wa kulia na wengine kushoto.

“Kama mnavyowaona hawa waliogeukia huko ni darasa la saba na hawa wengine ni darasa la nne na katika darasa hili jingine wanasoma darasa la pili na tatu ndivyo tunavyo kwenda," alisema.Alisema kuwa mwalimu wa darasa la saba anapoingia kufundisha, wa darasa la nne anasubiri mwenzake amalize huku wanafunzi hao wa darasa la nne wakiwemo humo humo ndani wakisikiliza wale wa darasa la saba wanavyofundishwa.

Alisema wakati mwingine walimu huamua kuwatoa nje na kuwaweka chini ya mti kama umefika wakati wa kusoma kitabu cha Kiswahili ili wasome wakiwa nje na wengine waendelee na masomo.

Mwalimu aliyekuwa darasani akifundisha, Shufaa Ramadhani alisema mazingira hayo ya ufundishaji ni magumu kwani kuna athari kubwa kwa wanafunzi na upande wa mwalimu kwani kufundisha wote kwa pamoja pia ni vigumu.

Alisema kuwa utaratibu huo unawaathiri watoto kisaikolojia kwani kuna uwezekano wa kusahau yale ambayo wamefundishwa na mwalimu wao na badala yake kusikia ya upande wa pili ambayo ni masomo ya darasa jingine ambalo tayari walishayapitia au bado hawajapitia.

Mwalimu Shufaa alisema walimu wanaathirika kwa kupoteza vipindi vingine kwa mujibu wa uandaaji wa masomo na vipindi kwani inamlazimu asubiri mwenzake amalize kufundisha na ndipo aingie na kufundisha somo lake.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali, George Kagomba hakupatikana kuzungumzia tatizo hilo na alipotafutwa kwa simu alijibu kuwa yuko kwenye kikao cha maandalizi ya Mbio za Mwenge.

Mkurugenzi huyo aliwataka waandishi kwenda kwa Ofisa Elimu wa Wilaya ya Mbarali. Hata hivyo, aliyekuwa akikaimu ofisi hiyo hakuwepo. Ofisa elimu wa Wilaya alikuwa amesafiri kikazi.

Madarasa mawili wasomea chumba kimoja
 
Tatizo ni serikali aumwalimu mkuu, kamati ya shule na wazazi wa watoto hawa? Hivi hata kama Chadema watakuwa madarakani watasimamia mpaka ngazi ya kitongoji. Huu ni ukosefu wa ubunifu. Watakosaje hata kufanya-partition ya plywood au mbao za Mafinga?
Serekali ya CCM imejaa uzembe kweli wa kila namna lakini mengine ni wananchi na watendaji kujitambua.
Ahungu
 
Tanzania Tanzania,
Nakupenda kwa moyo wote,
Nchi yangu tanzania,
Jina lako ni tamu sana,
Nilalapo nakuota wewe,
Niamkapo ni heri mama wee,
Tanzania tanzani,
Heri yako kwa mataifa,
Tanzani tanzania,
Karibuni wasio kwao,
Wenye SHIDA na TAABU,
Kukimbizwa na walowezi,
Tanzania yawakaribisha,
Tupigane kiume chema,
Tanzania tanzania,
Mungu awe na we daima,
MIAKA 50 YA UHURU,BADO TUKO HOOOI,SHAME ON US,MABADILIKO HATUTAKI,CJUI NANI ALIYETUPA ROHO MBAYA SANA YA UOGA,KWA KIVULI CHA AMANI BANDIA,HEBU ONA HAO MAWAZIRI WA BAADAE,HAWATASIGN MIKATABA FEKI KWELI KWA MAZINGIRA KAMA HAYO?
 
Viongozi wetu priority ni kununua Mashangingi swala la madarasa sijui nini nini? hakuna!
Huu ndo utawala wa SISI M.....KIdumu Chama.......cha......Mafisadiiii
SISI M na serikali yenu kweli madogo yamewashinda makubwa je?
Mimi nadhani 2015 inawapasa muondoke kwa amani maana mmeshindwa kuongoza nchi hii, mnakashfa nyingi sana za kifisadi nk.
Nchi Mmeuza mfano Loliondo mawasiliano hakuna waarabu washaleta GHUBA ya Uajemi Pale Loliondo. Inasikitisha, leo kuna Dowans,badala ya kuungana na watanzania wengine kwa maslah ya umma mna jali maslahi yenu ya kifisadi tuuu
 
Back
Top Bottom