kapotolo
JF-Expert Member
- Sep 19, 2010
- 3,727
- 2,214
Tunayo mihimili rasmi mitatu ya dola ambayo kazi yake kubwa ni kusimamia shughuli za umma na kuwaletea maendeleo wananchi. Tuna serikali, Mahakama na Bunge. Kwa nchi yetu mihimili hii imekuwa ni kero kubwa kwa watanzania badala ya kusimamia maendeleo, imekuwa chanzo na kudidimiza maendeleo na haki.
1)Serikali.
Ingetakiwa kuwa mfano lakini ni kinyume chake, Serikali :-
a)Imeshindwa Kusimamia uwajibikaji na kubariki wizi kwa kutumia mikataba feki bila kuwachukulia hatua wezi hao japo inawafahamu na wengine kuwapa vyeo serikalini na kwenye chama.
b) imeshindwa kudhibiti mfumuko wa bei na kushuka kwa thamani ya shilingi
c)imeshindwa kusimamia demokrasia, uchaguzi mkuu matokeo kutangazwa kukiwa na kura zilizopotea (Shinyanga) na zisizohesabiwa, Uchaguzi wa Meya arusha kufanywa na wajumbe chini ya 2/3, haki ya kuandamana imeondoka n.k.
d) imeshindwa Kujua vipaombele muhimu vya taifa, wabungwe mil 90 kwa ajili ya mashangingi, akina mama Bajaji ambulance, tusubiri akina mama watakavyokufa kwa 'abruptio placenta' kwa mitikisiko ya bajaji
e)imeshindwa kutupatia umeme wa uhakika na viongozi kujinufaisha kwa ukosefu wa umeme.
f) Imeshindwa kusimamia elimu, wako tayari waingize 100 wakifaulu 11 shauri yao
g) kwenye ajira, zimeongoezeka mil 1 za kuokota makopo.
h)Mizaha kwenye mambo mazito:
- wanaopata ukimwi na mimba ni kiherehere chao
- Dowans siwajui na hawanihitaji - Mwenyekiti wa baraza la mawaziri
- tukio la mbagala ni tofauti na gongo la mboto kwa hiyo sijiuzulu.
- Swala la mgao wa umeme litakuwa historia, sikia mikakati utalia
- n.k.
2) Mahakama- huku nako ndio haki inabadilishwa kwa dola, utasikia hukumu zenye utata, mtu anaua anashitakiwa kwa uzembe na faini laki 700,000/ (sijui ndio thamani ya damu lita 10,000 za watu wawili zilomwagika), imeshindwa kutoa haki kwa wazee wa EAC na kuwapiga kalenda zizisokwisha, nk.
3) Bunge - Hasa hili la kumi ndio hovyo kabisa, ni mipasho kwa kwenda mbele, bunge limekosa mvuto, halina tija kwa taifa, wabunge badala ya kujadili mambo ya msingi ni kujadili upuuzi na kuulizia mil 90 zao zitaingia lini kwenye account zao.
Kumbukeni: Watanzania hawatakuwa wajinga milele, naamini siku moja wataamka na kudai haki zao. Sauti ya umma ni sauti ya Mungu endeleeni kuipuuza.
1)Serikali.
Ingetakiwa kuwa mfano lakini ni kinyume chake, Serikali :-
a)Imeshindwa Kusimamia uwajibikaji na kubariki wizi kwa kutumia mikataba feki bila kuwachukulia hatua wezi hao japo inawafahamu na wengine kuwapa vyeo serikalini na kwenye chama.
b) imeshindwa kudhibiti mfumuko wa bei na kushuka kwa thamani ya shilingi
c)imeshindwa kusimamia demokrasia, uchaguzi mkuu matokeo kutangazwa kukiwa na kura zilizopotea (Shinyanga) na zisizohesabiwa, Uchaguzi wa Meya arusha kufanywa na wajumbe chini ya 2/3, haki ya kuandamana imeondoka n.k.
d) imeshindwa Kujua vipaombele muhimu vya taifa, wabungwe mil 90 kwa ajili ya mashangingi, akina mama Bajaji ambulance, tusubiri akina mama watakavyokufa kwa 'abruptio placenta' kwa mitikisiko ya bajaji
e)imeshindwa kutupatia umeme wa uhakika na viongozi kujinufaisha kwa ukosefu wa umeme.
f) Imeshindwa kusimamia elimu, wako tayari waingize 100 wakifaulu 11 shauri yao
g) kwenye ajira, zimeongoezeka mil 1 za kuokota makopo.
h)Mizaha kwenye mambo mazito:
- wanaopata ukimwi na mimba ni kiherehere chao
- Dowans siwajui na hawanihitaji - Mwenyekiti wa baraza la mawaziri
- tukio la mbagala ni tofauti na gongo la mboto kwa hiyo sijiuzulu.
- Swala la mgao wa umeme litakuwa historia, sikia mikakati utalia
- n.k.
2) Mahakama- huku nako ndio haki inabadilishwa kwa dola, utasikia hukumu zenye utata, mtu anaua anashitakiwa kwa uzembe na faini laki 700,000/ (sijui ndio thamani ya damu lita 10,000 za watu wawili zilomwagika), imeshindwa kutoa haki kwa wazee wa EAC na kuwapiga kalenda zizisokwisha, nk.
3) Bunge - Hasa hili la kumi ndio hovyo kabisa, ni mipasho kwa kwenda mbele, bunge limekosa mvuto, halina tija kwa taifa, wabunge badala ya kujadili mambo ya msingi ni kujadili upuuzi na kuulizia mil 90 zao zitaingia lini kwenye account zao.
Kumbukeni: Watanzania hawatakuwa wajinga milele, naamini siku moja wataamka na kudai haki zao. Sauti ya umma ni sauti ya Mungu endeleeni kuipuuza.