Serikali-Bima ya Afya kwa wote inawezekana kwa kila mwananchi kutoa shilingi 5,000 kwa mwaka

The Sunk Cost Fallacy

JF-Expert Member
Dec 1, 2021
19,589
14,135
Moja kwa moja kwenye mada.

Kila mtu ni mhanga wa ughali wa gharama za matibabu,tumeshuhudia jamii zikipata mgonjwa wa mda mrefu zinavyofirisika kwa kuuza kila mali yao Ili kugharamia matibabu ya mgonjwa na pengine asipone.

Kwa muktadha huo,wananchi wako tayari kuchangia walau sh.5,000 kwa kichwa kwa kila mwaka Ili kupata pesa za kuwa na bima.

Kwa kuwa wananchi wako tayari kulipa Serikali iandae sheria ya bima ya Afya kwa wote yaani universal healthcare act na Mfuko wa bima ya Afya ndio uratibu moja kwa moja jambo hili.

Ikiwa kila mwananchi au kichwa kitatoa sh.5,000 kwa mwaka kwa watu 60,000 serikali itapata wastani wa Bilion 300 Kwa mwaka pesa ambazo ni robo ya bajeti ya Wizara ya Afya.

5,000*60,000,000=3.E11

Ikiwa watu walilipishwa sh.20,000 kwa kununua vile viliitwa vitambulisho vya ujasiliamali na pesa ikapatikana ni dhahiri kwa wazo kama hili wananchi wataliunga mkono maana kila mtu atalipa kwa idadi ya watoto alionao.

Kila una watoto 6 utalipia hivyo hivyo,kama wako 10 utalipia watoto kumi.Lakini makundi maalumu kama walemavu, watoto wa mitaani,wazee na watu wengine maskini Sana watalipiwa na Serikali kuu na makundi mengine kama vile wafanyakazi ambao hukatwa kwenye mishahara yao kila mwezi ambao wao wataendelea kukatwa kila mwezi ila viwango vitashushwa kutoka 3% to 2% .

Aidha pesa ziwe ni mahsusi kwa ajili ya dawa,vitenganishi na vifaa tiba vya kisasa wakati huo huo bajeti ya Wizara ya kawaida itaendelea kuwepo kama kawaida Ili kuzalisha wataalamu,maslahi Bora kwa watumishi,utawala na kugharamia ujenzi wa miundombinu mipya.

Utaratibu huu ukianzishwa hatutegemei tena kusikia eti ugonjwa fulani ni gharama sana na hivyo watu wachangie.Kila ugonjwa utakuwa ndani ya bima.Kama Til.1.5 ya covid imejenga madarasa 15,000 nchi nzima,imejenga majengo ya emergency,imejenga masoko ya machinga,imeleta maji,imenunua ambulance,x-rays,MRI nk ni wazi zikipatikana japo til.Bil.300 zitaleta mapinduzi kwenye sekta ya Afya Nchini.

Ni vyema serikali iamue sasa kuleta mjadala huu kwa umma na iweke utaratibu mzuri wa kulipa hizo pesa kwa njia ya mitandao ya simu na Benki Ili tuanze rasmi kuwa na bima ya Afya kwa wote.

Kiukweli gharama za matibabu zinaumiza na zinafukarisha Sana,tunaomba serikali ichukue hili wazo kwa sababu halihitaji pesa ya serikali bali pesa itatoka kwa sisi wananchi moja kwa moja.

Kwa mujibu wa Utafiti,73% wako tayari kulipa Bima ya Afya.Ni wakati sasa wa Serikali kuchukua hatua za utekelezaji.

Screenshot_20220519-161059.png


Screenshot_20220519-161115.png
 
Watanzania wenyewe hawako serious na Bima, wacha tu tuendelee kuteseka.
Mkuu watu wote hawawezi kuwa serious ndio maana ya serikali kuingilia.

Unakuta anatembeza kibarua cha kuomba achangiwe ugonjwa na unakuta mtu anaenda kuomba msaada kwenye vyombo vya habari watu wamchangie.

Case kama ya Prof angekuwa na bima tusingefika huko na ashukuru alikuwa anafahanika sasa maskini wa kijijini si angeshajifia?
 
Tatizo hawajaelewa umuhimu wa Bima.
Ni ajabu kwamba hawaelewi ,kwamba wao huwa hawaugui au kuuguliwa?

Ukiugua kadi tuu 2,000 bado hujamuona daktari,vipimo na dawa na huo ni ugonjwa mdogo tuu wa malaria unatumia si chini ya 15,000.

Bima ingekuwepo ni sh.5,000 tuu maana malalamiko ya kukosa dawa ni kwa sababu dawa zenyewe ni chache na wahitaji ni wengi hivyo kutoa upenyo wa wizi.
 
Muhimu hum badala ya kulipia bando 10000 kwasiku basi jibane usichati kwa wiki 5 mkatie mwanao bima ya afya ya 50,400/= halafu wewe mkeo baba na mama katehi ile ya 30,000/= au 50,000/= kwa familia utakuja kushukuru siku moja utapouguliwa ukiwa huna kitu
 
The Sunk Cost Fallacy hayo yamesemwa na Serikali au maomi na mapendekezo yako? Sijaelewa. Nimesoma post lakini sijaona aya hata moja inayoonesha tamko wala commitment ya Serikali juu ya hiyo shilingi elfu 5.

Kama ni maoni yako unatuchosha bure.
 
Mkuu watu wote hawawezi kuwa serious ndio maana ya serikali kuingilia.

Unakuta anatembeza kibarua cha kuomba achangiwe ugonjwa na unakuta mtu anaenda kuomba msaada kwenye vyombo vya habari watu wamchangie.

Case kama ya Prof angekuwa na bima tusingefika huko na ashukuru alikuwa anafahanika sasa maskini wa kijijini si angeshajifia?
Huo ni wizi bima ya 5,000/ utatibiwa wapi?
 
a major concern is willingness and ability to pay.

Citizens are willing but not able to pay.

They are able to pay but not willing to join health insurance.

Currently, the country is planning for mandatory health insurance (every citizen should have any form of health insurance), there a lots of issues around its implementation.
 
The Sunk Cost Fallacy
Wazo lako zuri, lakini hebu Cross check hizo hesabu zako hapo...

Trillion tatu haiwezi kupatikana kutoka katika watu elfu 60 wanaochanga elfu 5 kila mmoja kwa mwaka.
60,000 * 5,000 = 300,000,000 (M 300)

Ili kupata Trillion 3 kwa mwaka kwa michango ya shilingi 5,000 unahitaji watu milioni mia sita.
 
This is useless post na mtoa Mada Hana uelewa wowote kuhusiana na masuala ya bima ya afya, unafanyia hesabu kama mauzo ya njugu, unajua effectiveness ya NHIF ya sasa?
 
14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom