Uchaguzi 2020 Serikali Amkeni: Taarifa lukuki za kutekwa wagombea wa chama kimoja tu cha siasa zisizo na uthibitisho ni hatari kwa usalama wa taifa

Mgombea wa Chadema Kongwa kavamiwa na watu wakamnyanganya begi ambalo lilikuwa na copy ya fomu. Hivyo original form ilikuwa salama. Kesho yake mgombea wa CDM akaipeleka kwa msimamizi ikapokelewa.

Ona kichekesho:
Job akaweka pingamizi kuwa FOMU ILIIBIWA SASA HII ULIYORUDISHA UMEIPATA WAPI?

Maana yake nini:
Job anajua fika kuwa fomu imechukuliwa ... hivyo aliwatuma yeye kufanya aborted kitendo hicho cha uvamizi!
Huu ujumbe wako umenifikirisha sana mkuu.
Kama alitangaza fomu yake imeibiwa basi alitaka kusababisha taharuki, naona kama kuna kutafuta umaarufu na kuchafuana tu kwenye tukio hili.
Kosa la aliyeweka pingamizi ni mwanasiasa, ilitakiwa jeshi la polisi lifanye uchunguzi kama mgombea aliyedai kuibiwa nakala ya fomu alisema ukweli au aliongopa kuchochea vurugu.

Kama mwongo hii ni jinai.
 
Wagombea wengi wa Chadema wameuza fomu wakaamua kujiteka ili wasilaumiwe na uongozi wa chama chao.

Angalau kwa ACT Wazalengo wagombea wao hawauzi fomu kwa fujo!! Kwa kweli ndg zangu CDM jitafakarini. Mmeweka wagombea bila kuwafanyia vetting!!

Najaribu kujiuliza, Watanzania wenzangu kweli hawa watu ndio wanaweza kushika dola? Si watauza nchi?

Mungu atuepushie mbali, wana tamaa hawa kubwa sana. Walifanya fomu ni dili la kupata fedha.

Queen Esther
Wamewauzia nani, huyo anunuaye hajakosea?

Sent from my Nokia 6.1 using JamiiForums mobile app
 
IGP ni mtoa miongozo na maamuzi hivyo kauli yake ni muhimu
IGP atatolea kauli matukio mangapi ya kihalifu yanayotokea kila siku hapa Tanzania? Mkuu, au unafikiri CHADEMA peke yao ndio watanzania? Mimi juzi kati hapa kuna mdogo wangu aliporwa simu na vibaka kule Tandale akaenda kutoa taarifa Police. Kwa hiyo mpaka hii nayo IGP atoe kauli yake?
 
Haki HUINUA TAIFA.

Nyie chama cha kishetani CCM tendeni haki ktk uchaguzi huu la sivyo mnataka kuendelea kudidimiza taifa.
Jinga kabisa cdm na vichaa wengine. Mnaigiza kutekwa ili kuichafua serikali ya ccm.
 
Unasema propaganda? Kwa sasa nipo Tunduma hapa mambo yalitokea tangu jumapili ni aibu, sili zilivuja kuwa ccm inataka kupora kata nane, kweli jumapili waliwakamata wagombea wa CHADEMA wakawasweka mahabusu kisha kuwanyima dhamana kwa wale walioshindwa kuwakamata wamewaengua kihuni ili mradi tu watimize ushetani wao, aibu kabisa.
 
Mhh bado naamini mwaka huu October tutakuwa na uchaguzi bora zaidi ya ule wa Serikali za mitaa
 
Jinga kabisa cdm na vichaa wengine. Mnaigiza kutekwa ili kuichafua serikali ya ccm.
We mbwa endelea kufurahia hayo mambo mnayotekelezwa huku mkilindwa na polisi...... Ng'ombe kabisa nyie jamaa

ccm ni chama cha kishetani
 
Kuna taarifa mpya ya kutekwa mgombea wa CHADEMA kwa ngazi ya UDIWANI na UBUNGE kila baada ya dakika chache ndani ya siku 5 za mwisho kuelekea siku ya leo tarehe 25/08/2020 ya kupitishwa majina ya wagombea na NEC.

Nyingi ya hizi taarifa hazina uthibitisho kiasi kwamba zinaleta hofu kuna watu wamepanga kuichafua nchi kwa makusudi na kutaka kupata uhalali wa kuja kufanya vurugu na kuomba jumuiya za kimataifa kuingilia mambo ya ndani ya Tanzania.

Sasa ifike wakati Tanzania iwe mbele kuliko maslahi binafsi. Kuna uwezekano mkubwa huu ni ushauri hatari uliopendekezwa na watu wa ndani au wa nje ya nchi ambao wana maslahi binafsi. Ninacho kiona ni hatari ya vita kama nchi zingine zilizo ingia kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe au kuvamiwa na majeshi ya kigeni kwa mlango wa kukomesha vurugu, kulinda amani na kusimamia demokrasia.

Vita hivi havitachagua familia za wana CCM au wana CHADEMA, ACT, NCCR-Mageuzi, ADC, CHAUMA au CUF pekee.
Mnaofanya mambo haya na kushawishi vijana wasiojielewa kutumika katika mipango hovu, haya mambo yatatudhuru wote na biashara zetu wote.
Msitumike na nchi jirani au watu wa mabara mengine kama hamjitambui.

Napata shida kuishauri serikali hasa Idara ya Usalama wa Taifa, JWTZ, na jeshi la polisi kuanza kuchukua hatua ngumu zaidi kwa waeneza taarifa hizi. Lakini sina budi niwashauri ikiwalazimu fanyeni hivyo, kama media zikishindwa kuwadai uthibitisho zaidi basi ziwekeeni speed governor maana hakuna namna, hapo baadaye watanzania wema watawashukuru kwa kuwaokoa na mkono wa mtoa roho. Wanasema 'the end justifies the means'.

Jukwaa letu pendwa JF nawashauri mjisafishe mikono yenu na damu zinazokaribia kumwagika sababu ya habari hizi za propaganda, jifuteni mikono yenu machozi ya watoto yatima watakao telekezwa na familia zao wakati wa vurugu, picha maarufu ya mtoto wa Sudan aliyekaribia kuliwa na tai baada ya kukosa uangalizi wakati wa vita inatembea kwenye akili yangu na kunitia simanzi sana nikiwaza jambo kama lile linaweza kuwatokea maelfu ya watoto wa kitanzania.

Ile picha ni mbaya kiasi kwamba mpigaji alikufa kwa msongo wa mawazo na kujutia kuchukua picha kama ile ingawa ilimpa utajiri, fikiria wewe unaye leta taarifa za uzushi zikija kusababisha mambo kama yale unafikiri utaishi kwa amani ndani ya nafsi yako hata kama unayemtaka ataingia Ikulu na kukupa ulaji wa keki ya taifa?

Mambo yalianza kama hivi hivi propaganda kwenye media kule kwa wenzetu nchi za jirani maziwa makuu. Yale mafuvu yanatisha zaidi kama ukiona ulikuwa sehemu ya jambo ovu kama lile kutokea.

Yale magofu ya Libya na biashara ya utumwa inasikitisha zaidi kama wewe ni sehemu ya waliochangia kutokea jambo lile.

Mchana mwema.
Wewe ni Msengwe sana ujue
 
Wewe ni Msengwe sana ujue
Umemaliza matusi yote mkuu?
Kama vipi niongezee kunitukana matusi mazito zaidi ya nguoni au hata mababu zangu watukane tu ili mradi uridhike, kisha njoo tujadili hoja au toa maoni yako nini kifanyike na nini kisifanyike.
 
Umemaliza matusi yote mkuu?
Kama vipi niongezee kunitukana matusi mazito zaidi ya nguoni au hata mababu zangu watukane tu ili mradi uridhike, kisha njoo tujadili hoja au toa maoni yako nini kifanyike na nini kisifanyike.
Hakuna hoja hapo zaidi ya Usengwe
 
6 Reactions
Reply
Back
Top Bottom