GwaB
JF-Expert Member
- Mar 19, 2014
- 3,575
- 4,634
Kati ya mambo yanayochelewesha maendeleo ya watu au taasisi binafsi zinazonuia kutoa huduma vijijini kwa wananchi pale ambapo kuna mahitaji ni kukosekana kwa miundombinu kiunganishi kati ya serikali kuu na serikali za mitaa. Kwenye ngazi ya kata kuna viongozi wanaoitwa wenyeviti wa vitongoji au kijiji ambao nagundua kuwa wao kazi yao ni kuonyesha njia na kuhamasisha.Katika ngazi hiyo hiyo ya kata kuna watendaji ambao wanatekeleza sera zilizowekwa na serikali iliyoko madarakani,hapa kuna watendaji wa kitongoji au kijiji ambao hadi leo najitahidi kujua kama wanateuliwa au wanaajiriwa kwa nafasi hizo.Watendaji katika ngazi ya kata ikiwa ni pamoja na jopo zima la watumishi wa halimashauri wana aina yao ya uongozi au utendaji ambao mimi binafsi nimeshindwa kuuelewa maana mara nyingi hawataki kuhimizwa kufanya kazi ambayo wanawajibika nayo, labda kwa kuwa hawasimamiwi na mtu au kwa kuwa wana mamlaka kamili na hawapaswi kusimamiwa na mtu mwingine isipokuwa wakurugenzi wa halimashauri.Kwa kuwa JF kuna hazina kubwa ya michango ya mawazo ningeomba wale wanaofahamu vizuri muundo na utendaji wa vyombo hivi viwili wanipe darasa ili nami niweze kuelimika kwenye hili. Nimeanza mada hii kwa kutoa angalizo la ucheleweshaji wa maendeleo ya watu kwa kuwa ndivyo ninavyodhani,ninapotafakari jinsi mambo yanavyoendeshwa ngazi za chini za utawala.Huo ni mtazamo wangu ambao yawezekana siyo sahihi na niko tayari kukosolewa.Natanguliza shukurani,