Serengeti yaibwaga TBL ‘kortini’

Balantanda

JF-Expert Member
Jul 13, 2008
12,476
4,752
KAMPUNI ya Bia Tanzania (TBL), imeagizwa kulipa faini ya asilimia tano ya mapato yake yote ya mwaka jana kwa Tume ya Ushindani (FCC), baada ya kubainika kuihujumu Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) kibiashara.

Hukumu hiyo dhidi ya TBL, ilisomwa makao makuu ya Tume hiyo, Dar es Salaam jana na Mwenyekiti wa FCC, Nikubuka Shimwela, kutokana na kesi mbili zilizofunguliwa na kampuni hizo mbili TBL na SBL, kila moja ikimshitaki mwenzake kwa ‘kumchezea rafu' sokoni.


TBL ilitakiwa kulipa asilimia tano ya mapato ambayo tayari yamekaguliwa na Mkaguzi wa Nje ili kuondoa uwezekano wa kudanganya mapato halisi iliyopata mwaka jana.


Shimwela alisema baada ya kusikiliza mashitaka ya pande zote mbili, Tume hiyo ilibaini kuwa TBL iliihujumu SBL kutokana na kuendesha kampeni ya kuondoa alama zake sokoni na kuagiza wamiliki na mameneja wa baa mbalimbali nchini, kutouza bidhaa za SBL na badala yake kuuza za TBL pekee.


Alisema kupitia kampeni hiyo, TBL iliwaamuru wamiliki wa baa na mameneja, kuondoa mabango na vipeperushi vinavyoitambulisha SBL sokoni na vifaa vinavyotumika kibiashara kama majokofu, viti na meza na kuweka mabango na meza zake pekee, hatua ambayo ni kosa kwa mujibu wa sheria ya ushindani wa kibiashara ya mwaka 2003.


Katika hukumu hiyo iliyosomwa kwa zaidi ya saa moja, Mwenyekiti wa FCC alisema pia Tume hiyo ilibaini kuwa TBL iliingia mikataba na wamiliki na mameneja wa baa, ili kuwashinikiza kuuza bia za TBL na kutouza za SBL, hatua ambayo pia ni kosa katika ushindani wa kibiashara.


Alisema pamoja na kuita mashahidi kutoka mikoa mbalimbali waliothibitisha TBL kuhusika na kampeni hiyo, TBL yenyewe katika utetezi wake uliowasilishwa katika Tume hiyo na shahidi wake wa kwanza, David Mgwasa, ilikiri kuhusika na vitendo hivyo kwa madai kuwa ilikuwa inaondoa 'takataka' katika baa ilizozifanyia ukarabati kwa kupaka rangi na kuweka alama zake.


Alisema katika uamuzi wake, Tume hiyo pamoja na kuitaka TBL kulipa faini hiyo au kukata rufaa katika kipindi cha siku 21 tangu siku ya hukumu, lakini imetengua makubaliano yote yaliyokuwa yamefanywa baina yake na wamiliki au mameneja wa baa, ya kutaka kuuza bidhaa za TBL pekee na kutengua pia maafikiano ya kuweka alama za TBL pekee.


Alisema hatua ya kuondoa mabango au alama zinazoonesha uwepo wa bidhaa za SBL ni kosa kisheria, kwani inahujumu jitihada zinazofanywa na SBL katika kuwafahamisha wateja wake maeneo yanayouza bidhaa zake, hatua ambayo haikubaliki katika soko la ushindani.


Wakati SBL ilifungua mashitaka mawili katika Tume hiyo la kuondolewa kwa mabango na alama zake kwenye baa na la TBL kufanya kampeni za kushawishi wenye baa na mameneja kutouza bidhaa za SBL, TBL ilifungua kesi ikiilalamikia SBL kuwa ilikuwa inatumia masanduku na chupa za TBL kujaza bidhaa zake na kuzisambaza badala ya kuingiza kwenye soko chupa na masanduku yake.


Katika uamuzi wake, Tume hiyo ilisema hoja hiyo ya TBL ilishindwa kuwatia hatiani SBL, kwa vile chupa na masanduku vilivyokuwa vikitumiwa na kampuni zote mbili, vilikuwa vikifanana kwa kiasi kikubwa na hivyo kushindwa kubaini ni mali ya nani baina yao, kwa vile hakukuwa na alama zinazotambulisha kampuni mojawapo.


Source: Gazeti la Habari Leo


Hatimaye haki imetendeka hapa.............TBL wameonesha udhaifu hasa katika ushindani mbele ya SBL
 
Ni vizuri kuwa haki imetendeka,TBL wamekuwa wakiyatenda hayo kwa muda sasa na kwa kiasi flani waliathiri sana soko la SBL.
 
Mkuu Balatanda,

Asante kwa kupost habari hii njema kwani TBL walitumia msuli wa kibiashara kujaribu kuwamaliza SBL. Ila kitu sijakielewa hapa, hiyo faini itakayolipwa na TBL, SBL watapata mgawo au ndo zinakuwa ni pesa za tume? Mimi nilifikiri pesa hiyo ingelipwa SBL. Lakini ingependeza zaidi kama TBL wangeamuliwa vile vile kurudisha mabango yote ya SBL waliyoyang'oa kwa gharama zao.

Tiba
 
Dada yangu aliyasema haya wazi hapa JF kuwa hawa akina Kavishe sijui na mwenzake nani yule, wataitia kampuni pabaya. Haka kamchezo kao sijui kama walitumwa au walifikiria wao wenyewe kwa kupewa habari jinsi nchi nyingine wanavyofanya na wao wakaiga. Ila wao wakawa wanafanya kwa NGUVU na kwa fujo mno kiasi kwamba kila mtu akafahamu.

Poleni watoto wa MUJINI. Ndiyo ukubwa huo. Ila asilimia 5 ya mapato, mhhh? Sasa zile walizompa tayari Joe Kusaga na Sean Kingston sijui nazo zinahesabiwa? Au hizo wataita ni matumizi? Udhamini sasa utatetereka.
 
hii ndio fundisho kwa wengine wote, TBL inabidi walipe billion 528 kwa FCC. HAO KINA KAVISHE NA MINJA WAKAJIFUNZE MARKETING SIO KUWAONEA WADOGO
 
Duuu! Kavishe, shelukindo na Minja, ubunifu uko wapi? Akina Kanjabahi full mgalagazo! Mko juu wazee wa chui
 
Baada ya kubwagwa na serengeti kortini, sasa TBL yatakiwa kulipa billion 528 kwa FCC, hapo bado Serengeti hawajadai chochote! Du! huu ufadhili wa michezo utaendelea tena kweli! Ama kweli biashara ya bia inalipa 5% ya total annual revenue ya TBL ni Billion 528!

Habari ndio hiyo!
 
Natumai hiyoo kama itakamilika kulipwaa kama ilivyoagizwaa itakuwa ndo penalty kubwaa kutokea katika business environment ya bongo..

Tbl natumai watakata rufaa kwenye tribunal ile kwani hizoo pesaa ni nyingi sanaa na zitawafanya wayumbee kwenye opersheni zao. Napongeza huu uamuzi kwani unaonyeshaa tunawezaa kusimamia level playing field ya kibiashara nchini wenyewe..bravo to FCC..
 
Hebu tuhabarisheni kidogo jamani. Kwani ni faini ya nini na juu ya nini. Sorry kama nitakuwa nauliza taarifa ambayo labda ilishawahi kubandikwa hapa nisiione. Ni taarifa tu!
 
Hii ni faini iliyotolewa na tume ya ushindani wa kibiashara ya Tanzania inayojulikana kama Fair Competition Committee kwa unprofessional behavior na misconduct za idara ya sales and marketing ya TBL katika kukabiliana na ushindani wa Serengeti Breweries. sometimes mwaka jana walivyoona ushindani mkali toka kwa serengeti wakaamu kuleta ubabe wa mtaani kwa kun'goa mabango ya matangazo ya mamilioni ya shilingi ya serengiti, kuvunja mafriji yao kwenye maeneo ya biashara na mwisho kuwakataza wauzaji wa bia yao hata kwenye mabaa kama kwa macheni wasiweke bidhaa za serengeti. Wanang'oa point of sales material na kujidai wababe. wakafika mbali nakukusanya kikundi cha wanafiki wakajiita wenye mabaa dar na kusainiana nao MOU na hawa watu badala ya kufanya biashara wakaanza kwenda kwenye magazeti kutoa statement kwamba TBL wamekua wakiwasaidia, eti umeshaona akili ya watanzania. Pia wakawa wanawapa wenye mabaa fedha taslimu hadi sawa na bei ya crate 4 kwa kila anayekataa kuweka products za serengeti. Hii ikaendana na wao kupinga ubia wa SBL na East African Breweries ya Kenya mahakamani uingereza. Na kudai kwenye vyombo vya habari kwamba wao wanaletea nchi yetu ajira nyingi na faida nyingi. Hapo ndipo walipojua kwamba wana deal na wasomi, SBL wakatoa statement kuwajibu kwamba si kweli zaidi ya 75% ya faida yao inapelekwa south africa na wao sio kampuni ya kitanzania ni ya nje kwa ownership structure yao. Pia wakaoonyesha kwamba ajira wanazo create ni cha mtoto ukilinganisha na zile wanazo create serengeti. Baada ya hapo Serengeti wakaenda kwenye tume kuelezea na kutoa vidhibitisho, TBL hoi hawana hili wala lile na Serengeti wameshaingia ubia na East African Breweries wazee wa Tusker na mambo yao super hao TBL wamefundishwa adabu. Sasa tusubiri watu wa simu nao maana wanatuibia sana na mis representation kwenye matangazo yao na hata garama za matumizi, punde tu tutawapeleka kwenye tume. Kwa hiyo kwa vijana wanaotafuta kazi wekeni Serengeti Breweries kwenye preferred employers wanakuja vizuri sana na wana recruit kwa sasa. Tusiogope TBL kupandisha bei hawawezi kwa sasa, wakifanya hivyo wao ndio loosers, kama wana akili wanajua hilo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom