Serengeti: Wananchi wawatuhumu wanaodhaniwa kuwa Askari wa Wanyamapori kwa utekaji

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
422
1,049

Baadhi ya wananchi wamewatuhumu wanaodhaniwa kuwa ni askari wa wanyamapori katika Hifadhi ya Serengeti kwa kuteka wananchi huku ikidaiwa kuna baadhi ya watu wanapotea kusikojulikana katika mazingira ya kutatanisha.

Gumzo kubwa kwa sasa ni kupotea kwa Nyamuhanga Mnanka (40) mkazi wa Mtaa wa Lubana, Kata ya Balili ambaye alipotea tangu Januari 5, 2022.

Bhoke Mnanka ni kaka wa Nyamuhanga, anasema: “Siku ya tukio walikuja magari mawili ya askari hao wakiwa katika mgari ya hifadhi wakamkamata na kuondoka naye, alikuwa shambani, wakazungumza naye kirafiki ghafla wakamkamata na kumtupa kwenye gari wakaondoka naye, hawakurudi tena, hizo gari hazikuingia ndani ya hifadhi zilipotea kusikojulikana.”

Naye, kaka mkubwa wa Nyamuhanga, Marwa Mnanka anasema: “Mpaka sasa hawajui alipo, wahifadhi majibu yao nao wanasema wameuliza kambi zote, hawajamkamata, ndiyo maana watu hawana imani na askari wenye hifadhi.”

Jambo jingine linalodaiwa kutokea ni vipigo kwa raia.

Mkazi wa eneo hilo, Emmanuel Mayila Abdallah (60) amedai kuwa amewahi kuwa mwathirika kwa hao wanaodhaniwa ni askari wa wanyamapori, anasema:

“Kuna vijana waliwahi kunivamia nikiwa ndani ya eneo la kiraia, nikawaambia sipo sehemu ya hifadhi lakini walinivamia na kunipiga sana, wakaniwekea silaha kitovuni, niliokolewa baada ya mke wangu kutokea, alinikuta kwenye hali mbaya sana.”

Mwenyekiti wa Mtaa wa Lubana, Kata ya Balili, mzee Marase Kilangi anasema matukio kama hayo ni kawaida kutokea mtaani hapo.

“Kuna watu kama sita wamepotea na hatujui wako wapi. Tumepambana kuwatafuta lakini hatujawapata, tumeshirikiana na Askari Polisi lakini hatujafanikiwa,” anasema.

Kamishna wa Hifadhi Kanda ya Magharibi, Martine Bhoke alipoulizwa kuhusu hilo alisema: “Ndio kwanza tunasikia hizo taarifa, tutafuatilia, kama wananchi wana malalamiko wafikishe katika vyombo stahiki.”

Chanzo: Watetezi TV
 
Balaaa lao linajulikana bora wananchi mkimbie hawa jamaa nahs wanavuta hewa ya pilipili kichaa
 
Kuna ukakasi hapo, Kijiji kina watu wangapi? Kwanini achukuliwe yeye tu? Chunguza vizuri wewe mleta mada hakuna kitu kinachotokea kwa bahati mbaya.
 
Acheni tabia ya UJANGILI mnawinda wanyama pori haswa Tembo na Nyati halifu mkichukuliwa hatua za kisheria mnataka tuwonee huruma hilo halikubaliki.

Acheni vitendo vya Kijangili.
Hata Kama wamevunja sheria ya Wildlife conservation wanatakiwa wapelekwe mahakamani
 
Mwenyekiti wa Mtaa wa Lubana, Kata ya Balili, mzee Marase Kilangi anasema matukio kama hayo ni kawaida kutokea mtaani hapo.
 

Baadhi ya wananchi wamewatuhumu wanaodhaniwa kuwa ni askari wa wanyamapori katika Hifadhi ya Serengeti kwa kuteka wananchi huku ikidaiwa kuna baadhi ya watu wanapotea kusikojulikana katika mazingira ya kutatanisha.

Gumzo kubwa kwa sasa ni kupotea kwa Nyamuhanga Mnanka (40) mkazi wa Mtaa wa Lubana, Kata ya Balili ambaye alipotea tangu Januari 5, 2022.

Bhoke Mnanka ni kaka wa Nyamuhanga, anasema: “Siku ya tukio walikuja magari mawili ya askari hao wakiwa katika mgari ya hifadhi wakamkamata na kuondoka naye, alikuwa shambani, wakazungumza naye kirafiki ghafla wakamkamata na kumtupa kwenye gari wakaondoka naye, hawakurudi tena, hizo gari hazikuingia ndani ya hifadhi zilipotea kusikojulikana.”

Naye, kaka mkubwa wa Nyamuhanga, Marwa Mnanka anasema: “Mpaka sasa hawajui alipo, wahifadhi majibu yao nao wanasema wameuliza kambi zote, hawajamkamata, ndiyo maana watu hawana imani na askari wenye hifadhi.”

Jambo jingine linalodaiwa kutokea ni vipigo kwa raia.

Mkazi wa eneo hilo, Emmanuel Mayila Abdallah (60) amedai kuwa amewahi kuwa mwathirika kwa hao wanaodhaniwa ni askari wa wanyamapori, anasema:

“Kuna vijana waliwahi kunivamia nikiwa ndani ya eneo la kiraia, nikawaambia sipo sehemu ya hifadhi lakini walinivamia na kunipiga sana, wakaniwekea silaha kitovuni, niliokolewa baada ya mke wangu kutokea, alinikuta kwenye hali mbaya sana.”

Mwenyekiti wa Mtaa wa Lubana, Kata ya Balili, mzee Marase Kilangi anasema matukio kama hayo ni kawaida kutokea mtaani hapo.

“Kuna watu kama sita wamepotea na hatujui wako wapi. Tumepambana kuwatafuta lakini hatujawapata, tumeshirikiana na Askari Polisi lakini hatujafanikiwa,” anasema.

Kamishna wa Hifadhi Kanda ya Magharibi, Martine Bhoke alipoulizwa kuhusu hilo alisema: “Ndio kwanza tunasikia hizo taarifa, tutafuatilia, kama wananchi wana malalamiko wafikishe katika vyombo stahiki.”

Chanzo: Watetezi TV
Umekurupuka.... BigTall

Kwanza habari yako ulitakiwa kutanabahisha eneo rasmi la tukio kwamba ni wapi?

Hiyo ni kata ya Balili - Kunzugu wilayani Bunda.

Ni eneo linalopakana na hifadhi ya wanyama ya Serengeti.

Lakini wewe umeweka heading inayoshiria kuwa wilaya ya Serengeti.

Hapo kuna vikosi vya TAWA na sio TANAPA.

Pia kuna eneo linalomilikiwa na muwekezaji Grumet reserves.

Kamishina wa TANAPA kanda ya magharibi Anaitwa Martin Loiboki na sio Martine boke.

Hiyo WATETEZI TV station yako ni ya Online au?

Je inaripoti habari katika maeneo gani nchini?
 
Hao ni waalifu na majangili dawa kuyadhibiti tuu
Ndugu Mimi ni mkaazi wa Mtaa wa rubana kata ya balili hakuna ujangili wowote kwenye maeneo haya na niwafahamishe tu nikwamba wanateka watu kutoka kwenye mashamba yaliyopakana na hifadhi ya Serengeti nikweli kabisa watu wanatekwa na sio majangili pia huyo afsa wa kanda ya Magharibi pia analijua sema ndo hivyo maisha ya Sasa mwenye nguvu mpishe Ila nakwambia usiombe ikutokee walie mteka haijulikani alipo mpaka Sasa Tawa na Tanapa wanasema hawajateka wakati watu wanapotea kabisa wanaacha familia zao zikitaabika
 
Acheni tabia ya UJANGILI mnawinda wanyama pori haswa Tembo na Nyati halafu mkichukuliwa hatua za kisheria mnataka tuwonee huruma hilo halikubaliki.

Acheni vitendo vya Kijangili

Ndugu acha kabisa kusema hivyo maana hayajakutokea sie ni mashuhuda na waathirika hujui shida iyowapata watu wa Mtaa wa Rubana kata ya Balili Bunda mjini nikwamba wanatekwa watu kwenye mashamba wakiendelea na shughuli zao za kilimo sio majangili na Wala hawako kwenye hifadhi kabisa sisi ni waathirika wa hayo matukio hakuna ujangili kabisa hapa Wala hakuna tembo Wala faru yeyote aliyeuwawa maendeo haya Kwa takriban Miaka mitano, pia hao tembo mpaka Sasa wanazagaa mpaka barabarani unawakuta hakuna mtu anaeuwa tembo Ila Kuna Jambo ambalo lazima lifanyike kukomesha haya maana sio mtu Mmoja aliyepote ni wengi sana
 
Umekurupuka.... BigTall

Kwanza habari yako ulitakiwa kutanabahisha eneo rasmi la tukio kwamba ni wapi?

Hiyo ni kata ya Balili - Kunzugu wilayani Bunda.

Ni eneo linalopakana na hifadhi ya wanyama ya Serengeti.

Lakini wewe umeweka heading inayoshiria kuwa wilaya ya Serengeti.

Hapo kuna vikosi vya TAWA na sio TANAPA.

Pia kuna eneo linalomilikiwa na muwekezaji Grumet reserves.

Kamishina wa TANAPA kanda ya magharibi Anaitwa Martin Loiboki na sio Martine boke.

Hiyo WATETEZI TV station yako ni ya Online au?

Je inaripoti habari katika maeneo gani nchini?
Huyu jamaa ni mpuuzi Kama wapuuzi wengine mkuu.
 
Ndugu acha kabisa kusema hivyo maana hayajakutokea sie ni mashuhuda na waathirika hujui shida iyowapata watu wa Mtaa wa Rubana kata ya Balili Bunda mjini nikwamba wanatekwa watu kwenye mashamba wakiendelea na shughuli zao za kilimo sio majangili na Wala hawako kwenye hifadhi kabisa sisi ni waathirika wa hayo matukio hakuna ujangili kabisa hapa Wala hakuna tembo Wala faru yeyote aliyeuwawa maendeo haya Kwa takriban Miaka mitano, pia hao tembo mpaka Sasa wanazagaa mpaka barabarani unawakuta hakuna mtu anaeuwa tembo Ila Kuna Jambo ambalo lazima lifanyike kukomesha haya maana sio mtu Mmoja aliyepote ni wengi sana
Kati ya hao wengi kwanini wewe haumo??
 
Acheni tabia ya UJANGILI mnawinda wanyama pori haswa Tembo na Nyati halafu mkichukuliwa hatua za kisheria mnataka tuwonee huruma hilo halikubaliki.

Acheni vitendo vya Kijangili.
Una uhakika mkuu? Isije kuwa ndio nyie mnauza viungo vya binadamu hao watu wamepotelea wapi!!!! Kama wawindaji haramu si tungewaona mahakamani?haikubaliki kabisa kufanya mauaji kwa Raia mbwa nyie

Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom