Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,445
- 3,403
Askari wa Jeshi la Wananchi (JWTZ), ambaye ni mshauri wa msaidizi wa mgambo wilayani hapa, Ramadhani Hamisi (46) amefikishwa Mahakama ya wilaya kujibu mashtaka mawili ya kubaka na kumpa mimba mwanafunzi.
Askari huyo mkazi wa Kebanchabancha, alikamatwa Januari 25 na kuwekwa mahabusu baada ya kutajwa na mtoto huyo kuhusika na kitendo hicho kilichomsababishia kukatisha masomo yake.
Juzi, mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Ismael Ngaile, Mwendesha Mashtaka wa Jamhuri, Renatus Zakeo alidai kuwa Hamisi alitenda makosa hayo Juni, 2018.
Alidai alimbaka mwanafunzi huyo wa kidato cha nne mwenye umri wa miaka 17 aliyekuwa akisoma Sekondari ya Ikorongo mashtaka ambayo mshtakiwa huyo aliyakana yote .
Askari huyo yupo nje kwa dhamana baada ya kukidhi masharti yaliyotolewa na Hakimu Ngaile ya kuwa na wadhamini wawili, mmoja akiwa mtumishi na kila mmoja asaini dhamana ya maneno ya Sh9 milioni na kesi hiyo itatajwa tena Februari 27.
Sent using Jamii Forums mobile app
Askari huyo mkazi wa Kebanchabancha, alikamatwa Januari 25 na kuwekwa mahabusu baada ya kutajwa na mtoto huyo kuhusika na kitendo hicho kilichomsababishia kukatisha masomo yake.
Juzi, mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Ismael Ngaile, Mwendesha Mashtaka wa Jamhuri, Renatus Zakeo alidai kuwa Hamisi alitenda makosa hayo Juni, 2018.
Alidai alimbaka mwanafunzi huyo wa kidato cha nne mwenye umri wa miaka 17 aliyekuwa akisoma Sekondari ya Ikorongo mashtaka ambayo mshtakiwa huyo aliyakana yote .
Askari huyo yupo nje kwa dhamana baada ya kukidhi masharti yaliyotolewa na Hakimu Ngaile ya kuwa na wadhamini wawili, mmoja akiwa mtumishi na kila mmoja asaini dhamana ya maneno ya Sh9 milioni na kesi hiyo itatajwa tena Februari 27.
Sent using Jamii Forums mobile app