Uzalendo wa Kitanzania
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 2,205
- 4,695
Happy Nyasumo (18) mkazi wa Wilaya ya Serengeti amemuua mumewe, Bebe Mbogo (26) kwa madai kuwa hampendi na hakuwa chaguo lake zikiwa zimepita siku 14 tangu walipofunga ndoa.
Akizungumza na Mwananchi Digital leo Alhamisi Aprili 14, 2021 mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Nurdin Babu amesema tukio hilo limetokea jana Aprili 14, 2021 saa 4 usiku katika kitongoji cha Pengo kijiji cha Iseresere.
Amesema chanzo ni mgogoro wa ndoa na mtuhumiwa anashikiliwa na polisi kwa hatua zaidi.
Diwani wa Majimoto, Johannes Masirori ambaye ni mjomba wa marehemu amesema Mbogo na Happy walifunga ndoa Machi 31, 2021 na kudai kuwa mwanamke huyo amekiri kufanya mauaji hayo.
"Kabla ya mauaji anadai kuwa mumewe alimlazimisha kufanya tendo la ndoa na baada ya kumaliza mwanaume alilala na yeye alipobaini amesinzia akachukua panga na kumkata mara tatu shingoni,” amesema.
Amesema baada ya kufanya kitendo hicho Happy alikwenda kwenye nyumba ya mkwewe na kuchukua chakula na kuanza kula.
Akizungumza na Mwananchi Digital leo Alhamisi Aprili 14, 2021 mkuu wa Wilaya ya Serengeti, Nurdin Babu amesema tukio hilo limetokea jana Aprili 14, 2021 saa 4 usiku katika kitongoji cha Pengo kijiji cha Iseresere.
Amesema chanzo ni mgogoro wa ndoa na mtuhumiwa anashikiliwa na polisi kwa hatua zaidi.
Diwani wa Majimoto, Johannes Masirori ambaye ni mjomba wa marehemu amesema Mbogo na Happy walifunga ndoa Machi 31, 2021 na kudai kuwa mwanamke huyo amekiri kufanya mauaji hayo.
"Kabla ya mauaji anadai kuwa mumewe alimlazimisha kufanya tendo la ndoa na baada ya kumaliza mwanaume alilala na yeye alipobaini amesinzia akachukua panga na kumkata mara tatu shingoni,” amesema.
Amesema baada ya kufanya kitendo hicho Happy alikwenda kwenye nyumba ya mkwewe na kuchukua chakula na kuanza kula.