Serekali ya CCM haitatekeleza ahadi zake ziko maalum kwa ajili ya kuombea kura mwaka 2015

Tukundane

JF-Expert Member
Apr 17, 2012
11,455
8,247
Ahadi nyingi ambazo zili ahidiwa na chama cha CCM kupitia mgombea wake kipindi cha uchaguzi hazitatekelezwa kwa sababu nyingi zililenga kuwashawishi wanachi waweze kukipa kura chama hicho. Hata zile ambazo zimeanza kutekelezwa hazitakamilishwa zitaachwa maalum kwa ajil kuombea kura mwaka 2015.

Kwani wakati huo CCM watakosa cha kumwahidi mwananchi kwani ahadi hizo zimeahidiwa Tanzania nzima kwa wakati huo hawatakuwa na jipya isipokuwa ni kuwambia wananchi kuwa ahadi tulizo ahidi tumeanza kutekeleza hivyo tuchagueni tena ili tuweze kumalizia pale tulipo ishia.

Huku wakijuwa fika ahadi hizo hazitekelezeki kutokana na uwingi wake na ukosefu wa fedha. Hadaa watakayo itumia ni kusema kuwa tumejenga shule, vyuo vikuu, barabara za rami, tumeunda wilaya na mikoa mipya wasielewe kuwa kazi hizo ni wajibu wa rais na chama kilichopo madarakani kuzifanya wakati huo.

Labda rais asie juwa wajibu wake ni upi ndie anae weza asifanye kazi hizo wakati amechaguliwa kwa kazi kama hizo.
 
Back
Top Bottom