Sera za Majimbo ni za Lazima! Asiyetaka ahame Nchi!

Hivi mnaojadili kwa kusema U.S.A imefanikiwa kwa kuwa na Majimbo mbona mnashindwa kutumia uwezo wenu kutafakali?

Unaweza kweli kulinganisha Tanzania na U.S.A?

Taaluma ya Ulinganifu inasema linganisha vitu vinavyoweza kulinganishwa.
Tanzana Kenya na Count zao hadi sasa wameshindwa kuafikiana kuhusu uendeshaji wa Mabunge ya Count zao.

1. Suala la Gavana kuwajibika kwani Mbunge hawezi kuwajibika?
2. Hivi mnao sema Serikali za Majimbo zitaleta Maendeleo je hamuwezi kuzungumzia suala la kuziimarisha Serikali za Mitaa au hamzijuwi?
 
Watu wanaofikiria majimbo ni wale ambao wanakubalika katika maeneo machache ya nchi kwa hiyo wanataka kutumia sera ya kuwagawa watanzania ili waongoze vipande vya mikoa wanayokubalika
 
Unajua kuna kipimo cha ujinga na upumbavu lakini heri mjinga maana anaweza kueleweshwa na mpumbavu katu anajua ukweli ila anaupindisha kwa faida zake

Ridhwan Kikwete na wana CCM wenzie ni moja ya makundi dhaifu kiakili na kihuhalisia, huku kundi linguine la wenye ulemavu wa akili ni baadhi ya wanachadema ambao ni fuata mkumbo, wasiozijua seraza chama chao na hawawezi kuzitetea..poleni!


Faida za sera za majimbo


1. Faida za utawala

Sera za majimbo zinaweza kabisa kufananishwa na Decentralisation system, ambako maamuzi hufanywa na watu wa chini kabisa, kwa jambo husika na kwa wakati husika.

Wananchi wanapewa uwezo wa kujitafuatia uongozi wao, na hivyo kumjweka mtu ambaye anajua mazingira ya eneo hilo, shinda walizonanzo na way forward kuzitatua. Mtu huyu pengine anajua utamaduni wa eneo husika, tabia zao na kupanga mikakati ya kujikwamua kutokana na walivyo.

Kwa kifupi ita improve quality of decision kwa jambo loloye liwe kwa eneo husika kitu ambacho hakipo kwa sasa

2. Faida za uchumi

Mtu yeyote mjinga na asiyeelewa ni yule anayedhani au kufikiri kuwa kuna maeneo nchi hii ni maskini na mengine ni tajiri.

Kansa ya mawazo haya iko kwa viongozi wa CCM na serikali yao wakihubiri kuwa majimbo ni mifarakano na wengine watakuwa maskini
Sema jimbo gani ni maskini, nitakueleza wafanye nini kupata utajiri..

Hakuna kijiji, mkoa au wilaya maskini Tanzania haipo!!! Umaskini ukiwapo ni wa ubongo mdogo wa raia wa mahali hapo

Sera ya majimbo itaharakisha maendeleo kwani ita &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];motivate' au ku'stimulate brain za watu wa eneo husika kuwaza na kufikiri kipi kifanyike kuleta maendeleo

Wataalamu wa sosholojia wanatanabaisha kuwa, jamii inayotengeneza sere zake, au kuamua mambo yake hufanya kazi kwa bidii ili maamuzi na malengo waliyoyaamua yafikiwe&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];.kwa mfano sera ya kilimo kwanza haitaweza kufanikiwa kwa sababu haijaamuliwa na wananchi na haijaingia akilini au mioyoni mwao ..kwa nini &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];kilimo kwanza' hata kama sera hii ni nzuri!!

Ni matatizo waliyoyapata akina Nyerere enzi hizo..wakati mpaka leo hii israel ina vijiji ya ujamaa kama alivyoanzisha Nyerere sisi vyetu havipo na kama vipo ni kibahati tu!!

Leo wengi hawajui wilaya ya Mbinga ndiyo tajiri kuliko zote Tanzania kwa kilimo cha kahawa, ufugaji na sasa wanapanda miti!!Nani anajua kuwa mkoa wa mtwara ni wa saba kuliingizia pato taifa?

Au hamjui kuwa wilaya za Ngaka, kiwira zina makaa ya mawe na liganga kuna chuma, nani asiyejua utajiri wa madini na kilimo morogogoro na mazao ya madawa mkoa wa Pwani?

Au nani asiyetamani kuona utajiri za zabibu Dodoma unavuka mipaka na kushindana na Israel ambayo inategemea zabibu kwa sana
Tanzania haina sehemu maskini, J

Juzi Mkongeumeongelewa sana, Mafuta na ziwa ni utajiri wa Kigoma na Rukwa inasifika kwa kilimo&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];semeni tujue wilaya maskini ni ipi?

Au haiumi kuona Lindi na Mtwara wana gesi ambayo inasafirishwa kuletwa DSM huku wao wakihangaika kucheza ngoma kwa kukosa kazi??

Haiumi kusikia Tanzania ni wazalishaji wakubwa wa dhahabu duniani uku wilaya husika ni maskini wakutupwa, au Almasi ya shinyanga ikiliwa kimya kimya!!! Kweli asali ya tabora na kijani cha Bukoba sio mtaji wa maendeleo ya taifa hili? Nani anabisha??

Sera hii italeta ushindani wa majimbo katika kuongeza kipato cha kaya, kijiji, kata, jimno na taifa!!

Dubai wameweza kuuweka mji wao kuwa sehemu ya kibiashara duniani sehemu ambayo ni jangwa kabisa!!

Kama kuna sehemu kuna jangwa, basi tutaweka DAR LIVE nyingi sana (Ridhwan tenda hiyoo dogo), na starehe nyingine zote ili watu wakipiga kazi ngumu wanaenda kupumzika na kujiburidisha sehemu ambazo zitakuwa haziwezekaniki..japo hamna hizo sehemu

3. Faida za kulinda utamaduni

Hakuna utumwa mbaya na wa kipekee kama kuacha tamaduni zetu, tumeiga wazungu mpaka wanatushangaa, vijana wetu wamekuwa kama mabinti, eti wanabana pua na MASCULINE behavior haipo!!

Malezi duni!!!
Kijana gani leo yuko tayari kupigana na kusema msitu huu wa baba yangu, na yuko tayari kuua simba na kulinda hadhi za kikoo, kifamilia, kikabila na hatimaye taifa??

Sera majimbo japo zimejikita ki-uchumi zaidi, lakini zina faida kubwa sana hata kiutamaduni

Utamaduni wa eneo husika huleta ubunifu wa eneo husika na kuongeza hadhi ya eneo hilo&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];leo hatuangalii nyimbo za wamasai ila tunanunuA MAKHIRIKHIRI kwa raha zooote huku tukijiona tumeendelea!

Kumbuka pia utamaduni hapa pia ni kurithisha vizazi vijavyo mambo ambayo kizazi cha sasa kinafanya, kama kulima, kufuga nyuki, kuchimba madini , kutengeneza vitu mbali mbali! kurithisha kizazi kijacho.......this is called informal education which is sometime far better than formal education!!

kuna faida gani kumaliza na degree uchwara ya uhandisi wa ujenzi na huwezi kazi wakati kuna fundi aliyejifunza tangu utotoni alianzia kubeba vifaa vya baba yake!!! anajua kila kitu kuliko injinia aliyekuwa na stress za bodi ya mikopo na shida za kukosa vifaa vya mafunzo??


4.
Faida ya kukusanya mawazo

Unapoona mwenzio kaendelea utajiuliza how? Kafanyaje? Maendeleo ya baadhi ya sehemu Fulani Fulani zitaleta &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];data collection' na mawazo kuwa kwa nini wengine wameendela wanafanyaje fanyaje.

Sera za majimbo zinaweza kupelekea kubadilisha sera za uongozi wa taifa na kufikia kufanya maamuzi ambayo huwezi kuyajutia na una mifano yake.


5.
Kulinda Rasilimali za Taifa

Kumbuka ikiwa kama majimbo yatagawanywa na kuwa mfumo wa states&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];.basi taifa la Tanzania lina weza kuitwa &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];United Sates of Tanzania' majimbo ambayo yana dola ya local na kitaifa, kulinda maeneo husika.

Ukiwa na mali lazima ulinde mali&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];kutorosha vitu kama wanyama hakutakuwepo, kuiba michanga ya madini hakutakuwepo, kukata miti ovyo na kuuza kwa bei ya kutupa hakutakuwepo!!! Do I need to say more here??...no!


6.
Kujenga Taifa Imara na viongozi wazuri wa kitaifa


Tuna taifa dhaifu kwa sababu tuna viongozi dhaifu! Tuna viongozi dhaifu kwa sababu tuna taasisi dhaifu, tuna taasisi dhaifu kwa sababu tuna familia dhaifu!


Taasisi kama uongozi wa ngazi mbalimbali ukiwa makini unaleta viongozi makini, taasisi hata za kidini zinaweza kuchochea kupata viongozi wazuri na akina baba wazuri
Ikiwa tyuna kiognozi wa jimbo Fulani aliweka strategy za kupata maendelao na yakaoneka, je hawezi kuwa ndio candidate mzuri wa wizara husika na hata taifa??

Viongozi watakuwa judged na kazi zao za kwenye majimbo na tutakuwa na hakika ya kuwa atafanya jambo akiwa rais let say&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];sio kuwa na viongozi vimeo kama hawa wasasa ambao haujui katoka wapi, kafanya nini, anaweza nini, unashtukia tu kiongozi na kesho mnalia HAWEZI&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];kwani nani alisema anaweza??


7.
Mwingiliano wa watu


Uzuri wa sera hizi kwa sababu tunaongelea taifa moja, mtu ataishi sehemua mabayo anajua atazichanga. &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];atatoka' atatengeneza fedha kulingana na akili zake na ujuzi wake!! Hili huleta maendeleo ya haraka kwa wenye akili! Sio wanaokalia majungu, kuchezabao na kuwaza uchawi!

Sera za majimbo kwa maendeleo ya Taifa, kumbuka kuna limitation zako au hasara zake, japo ni ndogo sana kw ataifa letu change sera za majimbo is not a matter of discussion&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];is a must!!

8. Kodi husika

Kodi inakatwa kulingana na eneo husika, kwa mfano kodi ya jimbo la Ontario nchini kanada iko tofauti na kodi ya British Columbia japo wako nchi moja, ukasanyaji wa kodi utakuwa rahisi na itafanya kazi iliyokusudiwaLeo hii kaodi zetu hatujui zinafanya nini na haujui umuulize nani! Aibu

9. Watu watapungua DSM (miji mikubwa) ha ha ha ha!!

I hate DSM but I am in!..ila nina kazi yangu na some prospects&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];ila naona watu wakitaabika, hawajui wafanye nini, hawana future, asubuhi tunajaziana foleni wengine wakiwa na decent jobs wengine hawana na cha ajabu ambao hawana kazi wanaishi maisha mazuri kabisa&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];sisi wafanya kazi tunakatwa kodi kubwa na ilimradi vituko tupu

Hawa wenyeji wengi waDSM ambao ni jobless ambao wanaweza kwenda elfu arobaini kwenye msiba wa kanumba siku ya kazi asubuhi..wakisikia wenzao mikoani wanazalisha na maisha yao yanaenda vizuri watarudi tu!!

Hata kama wasipoondoka hawa kwasababu wameishalemaa at least tutazuia watu kukimbilia mijini. Maisha ya bahati bahati , maisha yasiyo na muda wala malengo&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];maisha ambayo unatoka nyumbani saa kumbi na mbili na kufika kazini saa nne!!

Unafikia chai,kucheza karata kufacebook kidogo, lunch na unasinzia kidogo saa tisa unaanza kuangalia usafiri wa kurudi&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];asilimia 90 ya wafanya kazi wa serikalini ndio wanavyoishi!! Ha ha ha ha!


Watu hukimbilia mijini wakidhani ndiko kuna hela, sera ya majimbo itazuia hili! Japo hatari yake ni kuwa jimbo Fulani kukiwa kuzuri zaidi watu watakimbilia huko&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];.

lakini kama wanazalisha is okay hakuna shida, siyo kama wakazi wa DSM wengi&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG];hawaishi bali wanatafuta maisha!


10.
inatosha

wenu

Waberoya s. Waberoya

N.B huu sio uchambuzi wa sera rasmi ya chadema, maneno rasmi ya sera za chadema kuhusu hili , tafuta sera zake fika ofisi ya chadema iliyo karibu nawe utaipata, hapa nimeelezea tu kwa ufahamu wangu ubora wa sera hii, kumbuka pia kuwa mimi sio mwana chadema wala chama chochote cha siasa.
Utashangaa leo mtu huyuhuyu analikana hili andiko lake.
 
Ni ushauri tu

Yawezekana Sera ya Majimbo siyo mbaya kama tunavyofikiria.

Nashauri CCM ifanye utafiti wa kina kama Sera ya Majimbo inaweza kuharakisha maendeleo

Nawasilisha.
 
Una hoja ya msingi sana ambayo inahitaji tafakari ya kina, kwa kuongezea- ni vyema CCM kusikiliza watu wote wenye mawazo tofauti tofauti na siyo tu CDM ili kujenga mustakabali mwema, nashukuru kwa sehemu fulani serikali imeanza kuyafanyia utekelezaji baadhi ya mambo kwenye bajeti ambayo CDM waliyapendekeza miaka ya nyuma.
 
Kinachosababisha CCM kushindwa kulifanyia kazi suala la Sera ya majimbo ni '' ITIKADI Yao'' ya ujamaa ambayo sasa imeshakwama kwa karne tuliyonayo na huko tuendako.
Hakuna namna zaidi ya kuanzisha utawala wa majimbo, kwa maendeleo ya Taifa letu.
Mfumo wa utawala wa majimbo huleta ushindani wa fikra na huibua vipaji ambavyo kwa utawala tulionao havipewi umuhimu.
Kwa kuwa wananchi wengi hutegemea kilimo, mfumo wa majimbo utakuwa na faida kubwa kwa wakulima.
Leo kila sehemu Tanzania inazalisha zao/mazao kadhaa, lakini kuna sehemu mazao hayana soko kulingana na miundo mbinu na au masoko kutokidhi viwango.
Ikiwa tutakuwa na utawala wa majimbo, kila jimbo litapambana kukuza uchumi wake, na hivyo ujenzi wa viwanda utasambaa nchi nzima tofauti na Leo ambapo mikoa kadhaa ndiyo viwanda hujengwa kwa sababu ya urahisi na miundo mbinu bora.
 
Utashangaa leo mtu huyuhuyu analikana hili andiko lake.
Why nilikane mkuu

Hii ni imani yangu, msimamo wangu, mtazamo wangu, na mpaka kesho nasimamia hili

Kitu gani kimekufanya uhisi nitalikana?

i am genuine, nasimamia ukweli wa ukweli na siangalii mtu au watu..
 
Why nilikane mkuu

Hii ni imani yangu, msimamo wangu, mtazamo wangu, na mpaka kesho nasimamia hili

Kitu gani kimekufanya uhisi nitalikana?

i am genuine, nasimamia ukweli wa ukweli na siangalii mtu au watu..
Wakweli wa aina yako ndio wawezao kuleta na kusukuma maendeleo ya watu na hatimae Taifa.
lAKINI nyimbo na ngonjera za waimba mapambio zinaishia kwa waimbaji kuneemeka mmommoja. AMEEN
 
Back
Top Bottom