Not_Yet_Uhuru
JF-Expert Member
- Oct 11, 2010
- 1,304
- 431
Wana JF;
Mengi yamekuwa yakisemwa kuhusu uanzishwaji holela wa Sekondari ya Kata '(yeboyebo)' na kwa wachambuzi wa masuala ya maendeleo na sera walionya kuwa mwendo huu wa CCM na Serikali yake kuanzisha shule za mkupuo kwa malengo ya kisiasa ni ishara ya kukosa umakini na kutokuzingatia hali ya baadaye ya taifa kielimu lakini CCM walikanusha na kila siku wanataja uanzishwaji wa Serondari hizi kama ufanisi wao kisera!
Kulingana na Matokeo halisi ya Kidato cha nne yaliyotoka, mbali na wasichana kuongoza, shule za kata ndizo zilizofeli kupindukia, na kati ya shule zote za kata, zaidi ya 80% wamefeli vibaya, na hawawezi kuendea. Kwa maana nyingine, ni chini ya 20% ndio angalau wamefaulu kuendelea. Hii imetajwa kama 'JANGA KWA KITAIFA' (Source: Nipashe -28/02/2011)
Janga hili kitaifa linamaanisha nini??
Nomba kuwasilisha Great Thinkers...kwa mjadala....
Mengi yamekuwa yakisemwa kuhusu uanzishwaji holela wa Sekondari ya Kata '(yeboyebo)' na kwa wachambuzi wa masuala ya maendeleo na sera walionya kuwa mwendo huu wa CCM na Serikali yake kuanzisha shule za mkupuo kwa malengo ya kisiasa ni ishara ya kukosa umakini na kutokuzingatia hali ya baadaye ya taifa kielimu lakini CCM walikanusha na kila siku wanataja uanzishwaji wa Serondari hizi kama ufanisi wao kisera!
Kulingana na Matokeo halisi ya Kidato cha nne yaliyotoka, mbali na wasichana kuongoza, shule za kata ndizo zilizofeli kupindukia, na kati ya shule zote za kata, zaidi ya 80% wamefeli vibaya, na hawawezi kuendea. Kwa maana nyingine, ni chini ya 20% ndio angalau wamefaulu kuendelea. Hii imetajwa kama 'JANGA KWA KITAIFA' (Source: Nipashe -28/02/2011)
Janga hili kitaifa linamaanisha nini??
- Wazazi woote walioshawishiwa na Serikali kupeleka watoto wao Sekondari za kata, wameingia shimoni, kwa miaka yao yote minne (4) imepotea bure, wamerudi vijijini kuanza kuhangaikia maisha mbadala.
- Wazazi wao wamevurugwa malengo yao yote kuhusu future ya watoto wao na hivyo maendeleo ya jumla ya kufikra na kijamii yameathirika.
- Mbali na ukweli wa kuanguka huko kwa Sekondari za Kata, ukweli unabaki kuwa, shule hazina vifaa, waalimu, na pia wanafunzi wengi wanapelekwa huko bila hata kujua kusoma au kuandika na hivyo kufeli huku ni continuous, hakutaishia hapa.
Nomba kuwasilisha Great Thinkers...kwa mjadala....