Sera ya uchokozi dhidi ya China inayotekelezwa na Marekani yazidi kuwa wazi

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
VCG211233342044 (1).jpg

Fadhili Mpunji


Wiki mbili baada ya Spika wa baraza la wawakilishi la bunge la Marekani kutembelea Taiwan, kinyume na kanuni za Umoja wa Mataifa kuhusu uhusiano wa kidiplomasia, na kinyume na makubaliano yaliyofikiwa na serikali za China na Marekani, kwa mara nyingine tena Marekani imefanya kitendo kama hicho.

Kabla ya Bibi Nancy Pelosi kwenda Taiwan, China ilipinga vikali na kuwasiliana na Marekani na kuikumbusha kuwa kitendo hicho sio kama tu ni uingiliaji wa mambo ya ndani ya China, bali pia kinahatarisha hali ya usalama wa eneo la mlango bahari wa Taiwan. Ili kuficha undani wa suala hilo, Marekani ilitoa visingizio mbalimbali ikiwa ni pamoja na kusema Ikulu ya Marekani haijaibariki safari ya Bibi Pelosi, na hata baadhi ya wachambuzi wa maswala la kidiplomasia wa Marekani walisema kitendo cha Bibi Pelosi ni hatari na si cha busara.

Ndani ya mwezi mmoja baada ya safari ya Bibi Pelosi, wabunge watano wa Marekani wamefanya safari kisiwani Taiwan. Safari hii imekuwa ni wazi zaidi kuliko ile ya kufichaficha ya Bibi Pelosi, na pia imethibitisha kuwa ziara ya Bibi Pelosi kimsingi ilikuwa ni jambo la uchokozi wa makusudi, na ya hii ya wawakilishi wanne, ni ya makusudi na mwendelezo wa uchokozi ule ule.

Mwanzoni wakati China inatoa malalamiko yake, baadhi ya watu walitaka China ijizuie kwa kudhani au kuamini kuwa safari ya Bibi Pelosi lilikuwa ni tukio la bahati mbaya kidiplomasia lililotokana na ujeuri binafsi wa Bibi Pelosi, ambao amekuwa akiuonesha dhidi ya China tangu akiwa mdogo.

Ni wazi kabisa kuwa hakuna mwenye kuthubutu kusema ziara ya wawakilishi ni tukio la bahati mbaya.

Ni wazi kuwa hakuna kisingizio chochote kinachohalilisha safari ya wawakilishi hao kisiwani Taiwan.

Kwa mujibu wa azimio namba 2750 lililopitishwa mwaka 1971 kwenye mkutano wa baraza la Umoja wa Mataifa, Taiwan ni sehemu ya ardhi ya China.

Nchi zote zinazoheshimu sheria ya kimataifa na hasa maazimio ya Umoja wa mataifa zimekuwa zinataja kuheshimu azimio hilo.

La muhimu zaidi ni kuwa China na Marekani zimekuwa na makubaliano maalum ya pande mbili kuhusu suala hilo.

Kwanza, ni taarifa ya pamoja ya Shanghai iliyotolewa Februari 1972 na China na Marekani, ambayo pamoja na mambo mengine inatambua mamlaka ya China juu ya kisiwa cha Taiwan.

Pili, ni taarifa ya pamoja iliyotolewa Januari 1979 ya kuanzisha uhusiano kati ya China na Marekani, ambayo msingi wake ni Marekani kutambua kuwa China ndio mamlaka pekee na halali ya China yote ikiwemo kisiwa cha Taiwan.

Tatu, ni taarifa ya Agosti 1982, ambayo kimsingi inasisitiza kutambua taarifa mbili za mwanzo, na haswa swala la mamlaka ya China kwenye kisiwa cha Taiwan na Marekani kutoa uhakikisho kwenye mambo sita kuhusu kuheshimu mamlaka ya China kwa kisiwa cha Taiwan.

Kwa watu wanaofuatilia kwa karibu mwenendo wa Marekani katika kufuata na kuheshimu sheria za kimataifa, wanaweza kukumbuka wazi kupuuza au hata kukiuka sheria za kimataifa si jambo jipya kwa Marekani.

Ikumbukwe kuwa wakati wa vita ya pili ya Iraq, Marekani iliamua kupuuza sheria za kimataifa na kuvamia mamlaka ya Iraq. Ikumbukwe pia hata baada ya kusaini makubaliano ya nyuklia ya Iran (JCPOA) pia iliamua kuyapuuza makubaliano hayo.

Mbali na hayo Marekani pia iliamua hata kupuuza na kujitoa kutoka Shirika la Afya Duniani, kwa sababu zisizoeleweka.

China inatambua wazi kuwa hii ni tabia ya Marekani, na kitendo cha Bibi Pelosi na wawakilishi wengine watano, si kitendo cha bahati mbaya.

Ni kitendo cha makusudi na ni tabia iliyozoeleka ya Marekani, inachokifanya China inapolalamika ni kuikumbusha jumuiya ya kimataifa na kulinda mamlaka yake.
 
Siku watu weusi tukaja juu kiuchumi na kijeshi wallahi roho zetu mbaya tutauwa jamii zote ulimwenguni isipokuwa wanawake tu.

Eehh ndio nimesema wanawake tu sasa tutachepuka wapi na nyapu za Kichina, Kihindi na Wazungu na Waarabu waruwaruuu.
 
Back
Top Bottom