MzalendoHalisi
JF-Expert Member
- Jun 24, 2007
- 4,519
- 1,367
Nyani,
Unafahamu kuwa kuna wahindi kibao wamejazana bongo ilihali hawana shule kabisa???ukipita kwenye viwanda vya wahindi bongo maana ndio wengi wenye viwanda, nenda migodini na kwenye makampuni mengi tu unakuta watu wameajiriwa kwa sababu mwenye mali ni mhindi mwenzake, kaburu mwenzake au mzungu mwenzake.
Tembea kwenye viwanda vya sukari uone kama wale makaburu waliojazana pale wamesoma, tembelea meli za uvuvi bahari ya hindi uone kama wale wahindi na wafilipino kama wamesoma, nenda migodini uone kama wale askari wa kinepali(nepalese) kama wamesoma kama unavyodai.Ukweli ni kuwa hawa wenzetu wanawezeshana, huku wabongo wakigeuka watumwa ndani ya nchi yao.Waulize watanzania waliojaribu kuwekeza nyumbani vikwazo walivyokumbana navyo, manake usije ukadhani wabongo-wazawa hawajui kuchakarika.
ndio maana tunasema ni muhimu mno kuwawezesha wazawa ili wafaidike na rasilimali za nchi yao.
kama kila siku watu wanahamishwa kutoka kwenye maeneo yao yanayowapatia rizki kwa kisingizio cha kupisha wawekezaji, mona huo uwekezaji wa wageni hususani migodi haina tija yeyote kwa serikali na kwa wananchi, fedha yote wanapeleka kwao, wasukuma, wakurya na wamasai wamebaki kutaabika tu huku wakwapuaji wakizidi kufaidi rasilimali madini za watanzania.
Hata Mengi amewezesha kwanza ndugu zake..angalia Elitiira, Benjamen, yaani wana pesa chafu!
Sasa mimi nikiwa na kiwanda changu nisiwape kazi kwanza ndugu zangu?