Richard Robert
JF-Expert Member
- Dec 21, 2012
- 632
- 340
Rasimu ya katiba inasema:
Mpaka sehemu Hii hapo juu mambo safi! .........
Pabaya ni Hapa kwenye kijani:...
Huu ni ulaji tu!.. Hauna tija kwa mwanamke wala jamii ya kitanzania... Ni mfumo wa kunufaisha wachache na kuumiza wengi.
Maoni yangu:
Sikubaliani na uwakilishi wa wanaume na wanawake kwenye majimbo kwa sababu zifuatazo:
1. Mfumo huu utaongeza gharama kubwa sana za kuendesha bunge.
2. Mfumo huu utakuwa ni mzigo mkubwa kwa walipa kodi.
3. Hii inamaana majimbo 239 yatatoa wabunge 478 (pengine yataongezwa mengine)
4. Je, usawa wa kijinsia ukiibua hoja za usawa wa dini, na makabila tutaelekea wapi?
Nini kifanyike
1. Tume ipunguze majimbo ya uchaguzi na kufikia 100;
2. Nguvu ielekezwe kukomboa wanawake kielimu na kupanua wigo wa ajira.
3. Wanawake wagombee majimboni kama wengine, vinginevyo serikali iandae utaratibu wa uwiano wa kidini na kikabila.
4. Ukombozi uelekezwe kwa wanawake walio wengi.
Kuhusu Bunge kutakuwa na wabunge wa aina mbili. Kutakuwa na Wabunge wa kuchaguliwa na wabunge watano wa kuteuliwa na Rais kuwakilisha Watu wenye Ulemavu.
Tume inapendekeza kwamba, Mbunge akifukuzwa na Chama cha Siasa abaki kuwa Mbunge lakini akihama Chama atapoteza Ubunge wake.
Inapendekezwa ukomo wa Ubunge uwe vipindi vitatu vya miaka mitano mitano. Hata hivyo, wananchi wanaweza kumwondoa mbunge wao kabla ya mwisho wa kipindi chake.
Inapendekezwa pia kusiwepo na uchaguzi mdogo isipokuwa kama nafasi inayokuwa wazi inatokana na Mbunge huru ndipo utafanyika uchaguzi mdogo kujaza nafasi hiyo, lakini kama nafasi ikiwa wazi kutokana na Mbunge wa Chama cha Siasa basi nafasi hiyo, ijazwe na mtu kutoka Chama hicho.
Inapendekezwa Spika na Naibu Spika wasitokane na Wabunge na wasiwe Viongozi wa vyama vya Siasa.
Mpaka sehemu Hii hapo juu mambo safi! .........
Pabaya ni Hapa kwenye kijani:...
Kila Jimbo la Uchaguzi litakuwa na Wabunge Wawili mmoja mwanamke na mwingine mwanamume.
Huu ni ulaji tu!.. Hauna tija kwa mwanamke wala jamii ya kitanzania... Ni mfumo wa kunufaisha wachache na kuumiza wengi.
Maoni yangu:
Sikubaliani na uwakilishi wa wanaume na wanawake kwenye majimbo kwa sababu zifuatazo:
1. Mfumo huu utaongeza gharama kubwa sana za kuendesha bunge.
2. Mfumo huu utakuwa ni mzigo mkubwa kwa walipa kodi.
3. Hii inamaana majimbo 239 yatatoa wabunge 478 (pengine yataongezwa mengine)
4. Je, usawa wa kijinsia ukiibua hoja za usawa wa dini, na makabila tutaelekea wapi?
Nini kifanyike
1. Tume ipunguze majimbo ya uchaguzi na kufikia 100;
2. Nguvu ielekezwe kukomboa wanawake kielimu na kupanua wigo wa ajira.
3. Wanawake wagombee majimboni kama wengine, vinginevyo serikali iandae utaratibu wa uwiano wa kidini na kikabila.
4. Ukombozi uelekezwe kwa wanawake walio wengi.