Sera ya Chadema ya huduma bure kwa afya kwa wazee yakumbatiwa sasa!

Uko sawa lakini tukitaka kupata defintion sahihi ya mzeee tunayetaka kumsadiai tunatakiwa kuangalia beyong age?

Nimelisoma wazo lakini ingawa kuna complication katika kuwatambua lakini bado ni wazo sahihi . Hii complication ni kama ya wanafuzi wa vyuo vikuu kupata mikopo. nadhani tujairibu kupendekeza njia sahihi za kuweza kuwaweka watu katika kundi hili la "wazee" wanahitaji msaada.


  • Mfano mzee mwenye miaka 50 yuko dar na mwingine ana miaka 50 yuko mAnyoni. Kama ni definiton sahii basi huyu mwenye makazi manyoni ni ndio anaqaulify kupata upendeleo wa afya .
  • Kama mzee ana nyumba zake mbili anapata kodi mwingine anategemea wajukuu na watoto. yupi ana qualify
  • Kuna wazee ambao walikuwa wakulima hawakuwai kupata mishahara na ajira za ofisini na wameishiwa nguvu
Kwa hiyo tukichanganya umri, location, vipato, rasilimali na tukiwashirkiza viongozi wa mitaa tunaweza kupata wazee sahihii wanaotakiwa kusaidiwa.

Ni kweli mkuu kupata standard definition ni ngumu na ni swala linalo hitaji majadiliano mazito na si kwa serikali kulala leo na kuamka Jumatatu na kuamua kupachika pachika vitu. It is very hard kuja na standard definition kwa sababu Tanzania yenyewe haiko uniform. Kwa nchi kama za wenzetu hata uishi wapi ndani ya nchi standard of living ni almost za same kwa hiyo hata life expectancy kimaeneo haipishani. Lakini kwa Tanzania mtu wa Dar Es Salaam na mtu wa vijijini mikoani ni kama vile wanaishi dunia mbili tofauti.

Mkuu Kibunago alitoa point moja nzuri sana ambayo nadhani ndiyo tatizo letu kubwa nalo ni kuidentify watu hata hapo ambapo tumesha pata definition ya kitu fulani. Tuseme kwa mfano tu tuna kubaliana mzee ni mtu mwenye miaka 50 je hii healthcare ya bure apewe hata mtu wa miaka 50 ambae bado ana fanya kazi? Maana kwa wenzetu mfano Marekani Medicare ya wazee inaanzia 65 ambayo ndiyo umri nao wa kustaafu.

Halafu pia kama tukisema healthcare ya bure kwa wazee ina maana lazima iwe standard. Huwezi kusema healthcare ya bure kwa mzee halafu uanze kubagua na useme lakini mzee mwenye kipato fulani au uwezo fulani au mwenye watoto wenye kipato fulani asipewe. Haiwezekani. Marekani Medicare ni kwa mtu yoyote 65+ regardless ya kipato chake. Sasa sisi mtu akisha kuwa mzee lakini tuseme mzee mwenye uwezo fulani haqualify basi hiyo siyo free healthcare kwa wazee tena tuite kitu kingine. Maana as the name suggest free healthcare for the elderly should be free healthcare for the elderly sasa kama siyo kila mzee ana qualify tutai itaje free healthcare for the elderly?

Ndiyo maana mimi nasuggest tuwe na free healthcare for the poor tukiangalia kipato cha mtu. Hata kama wazee wengi ni masikini kama unavyo sema haina shida because kama ni masikini it means they will fall under the policy. Kuhusu nani ni masikini hiyo ni easy kudefine kwa sababu tuna weza kusema kwa standard za Tanzania mtu mwenye kipato chini ya kiwango fulani basi ni masikini.
 
Mwanakijiji swali lako ulilomaliza nalo ni zuri lakini sikubaliani na kichwa cha habari kwani kama alivyosema Katibu Mkuu wa Wizara sera ya kutoa msamaha kwa baadhi ya makundi ya wagonjwa (watoto, wazee, wafungwa, maskini), aina ya magonjwa (mf. magojwa sugu) na aina ya huduma (mfano za ukunga na uzazi) ilikuwepo hivyo si ya CHADEMA. Aidha mlengo wa CHADEMA ulikuwa si huu wa ku- target makundi yanayostahili kupata msamaha, wao katika Afya na Elimu waliongelea 'bure' kwa watu wote.

Hapana hawajawahi kufanya hivyo; soma Ilani yao. Wagombea wa CCM ndio waliwaaminisha watu kuwa Chadema wanamaanisha watu wote.
 
WANA JF -Bongo TZ, Mzee Mwanakijiji na great thinkers wote -mimi nakubaliana na CHADEMA afya bure inawezekana na mkitaka tuangalie wapi tuanzie nadhani kwa sasa mzizi wa fitina ni katiba, ambayo itatupa viongozi bora regardless wametoka vyama gani, then tutadhibit ufisadi, then mengine yote yatawezekana kadri tutakavyopanga au serikali itakavyoamua. Contrary to dhati hawa wanahangaika kudandia sera bila mipango madhubuti na usimamizi-hili la kuwapa wazee afya bure ni zuri lakini litakuwa zigo na ufisadi mwingi utatokea mno. Wanaopinga mambo haya kupewa msukumo na CHADEMA sio waungwana, kimsingi CHADEMA haifanyi kitu kipya ila inatoa CHANGAMOTO na kuonesha kumbe inawezekana LAKINI kwa uongozi bora na ni kwasababu hiyo wanakurupuka au wanatumia pesa nyingi kuweka mipango ila watekelezaji wanakosa usimamizi -KWAHIYO NINAWAOMBA WANAJF tuelekeze nguvu kwenye Katiba mpya, tukifanikiwa hili tutapata viongozi bora ama kupitia chadema au ccm au vyama vingine manake kutakuwa hakuna kubeba matapishi kama mahanga aliyetanganzwa kwa mabavu, au blandes kule karagwe, au selukamba kule kigoma, au kibaha au shinyanga mjini
 
Hakuna kisichowezekana. Ni suala la uamuzi na kuwa na utashi thabiti wa kisiasa. Kama baadhi ya wachangiaji walivyosema ni muhimu sana kuelekeza nguvu za kutosha katika kinga na afya kwa watoto chini ya miaka mitano. Aingii akilini kwa mtoto mdogo kufa kwa kifo ambacho kinaweza kuzuilika kwa gharama ndogo tu.
 
Kwa kweli bora wakope sera kama hizo ni zuri kwa kuwaangalia na kuwajali wazee wetu hakuna kosa kama watachukua sera nzuri kutoka vyama vingine japo walisema haiwezekani
 
Ninachojua mpango huu ulikuwepo before CDM hawajaimba hiyo afya bure, kinachosemwa hapa ni kuuboresha kwa kuwa utekelezaji wake mwanzo ulikuwa na changamoto nyingi, na kwa jinsi ninavyojua mwanakijiji analijua hili kwa sababu limeelezwa vizuri kwenye sera ya afya ya 2007 na muongozo wa kuchangia huduma za afya, anachotaka ni kuwapoza aliowadanganya kuwa watashinda ili wasimdai ushindi wao.
 
Hivi hii serikali iliposema watoto chini ya miaka 5, wazee zaidi ya miaka 60, wagonjwa wa maradhi kama kisukari, kansa, ukimwi, bure hawakuwa wakifanya hivyo? (samahani sijawahi kutumia huduma za hospitali za serikali) naomba ufafanuzi wa ziada
 
Mimi ni msatahafu kisheria mwaka wa pili sasa. Uzoefu wangu kwenye huduma za afya ni kuwa serikali haina uwezo wa kutekeleza cho chote kinachoahidiwa.

1. Fedha zinazokatwa toka kwa watumishi wa serikali kwa lazima ni pato kubwa sana la kikundi fulani. Ni nyingi sana na zinakopwa au kutumika kiholela. Nitatoa mfano wangu binafsi nimekatwa hizo pesa kwa ajili ya mfuko wa afya mpaka nimestahafu, nashukuru Mungu sikupata maradhi ya kuhitaji huduma ya matibabu, sasa ni mzee nahitaji huduma hiyo. Hakuna taratibu yo yote ya mimi kuipata huduma hiyo kwa sababu hakuna utaratibu huo na pili sikuwahi kupewa kadi yao ya huduma ya afya kwa sababu nisizojulikana. Nilidai sana bila mafanikio.

2. Serikalini kuna kitu kinaitwa sera. Maana yake halisi ni mwongozo wa matarajio kwa kipindi fulani. Na serikali hii ya chama tawala (siyo chama kiongozi) ina sera nyingi sana nadhani hata wao hawazikumbuki. Moja wapo ni sera ya huduma ya afya kwa wazee. Utekelezaji wake hauwezekani kwa sababu watawala haiwahusu, hawana mbinu yo yote (mkakati) ya utekezaji kwa sababu serikali haingozwi kwa sera bali kwa ahadi za papo kwa papo, muda ukipita na ahadi imepita hata kama haijatekelezeka.

3. Kwa nini sera hazitekelezeki? Ni kwa sababu hazina sifa za kuitwa sera bali ni mbinu ya kujichanganya kuwa kuna kitu kinafanyika hata kama hakiwezekani; pili wakati mwingine kingeweza kutekelezwa na sera mama kama ipo. Kwa hoja hii utaona sera ya wazee ni kiini macho tu kikidhi matakwa ya kisiasa ya watawala.

4. Sera ya kitaifa kwa maoni yangu ni ile inayoleta matarajio ya huduma bora za kijamii ambayo itaelekeza jinsi rasilimali zitakavyoelekeza kufanikisha matarajio hayo. Kwa hiyo elimu, afya, miunombinu, viwanda, kilimo nk vingetafisiri kufanikisha huduma bora za kijamii. Baada ya matamko hayo serikali makini ingejipanga kuwa wizara zinatekelezaje sera moja ya kitaifa kwa kuweka mikakati ya utekelezaji katika kila sekta.

5. Kwa taarifa zangu sina uhakika kama hata sera lukuki zinazoimbwa zilitengenezewa mikakati elekezi. Kwa sababu ziko diverse hazina convergence.

Ninachojaribu kusema serikali haina sera ya kitaifa ya utekezaji ambayo ingesema wazi itatekelezaje huduma za afya kwa wote wawe wazee au wafanyakazi. Hapa lazima nikiri Chadema walikuwa na wana nia ya kutekeleza hayo kwa umakini kwa kutumia rasilimali iliyopo. Elimu, afya bure, gharama za ujenzi nafuu zinawezekana kuwa na sera mama ya kitaifa. Utekelezaji wake ungepunguza sana ukubwa wa serikali kwa sababu ya convergence ya matarajio ya ujumla kwa kuwatumia watekelezaji wachache makini.

Katibu Mkuu afya anatoa ahadi hewa hana jinsi ya kutekeleza; inahitajika kichwa kibunifu na utekelezaji makini wenye dhamira ya maendeleo ya watu siyo ya vitu. Afya ni maendeleo.
 
Back
Top Bottom