Nimetafakari kwa muda sana baada ya mimi binafsi kuamua kujiingiza kwenye kilimo kama mkakati wa kujiajiri na kuajiri watu wengine. Kama kijana wenye uelewa na nilipata elimu nzuri na kupambana na tatizo la ajira, kilimo ingekuwa njia nzuri ya kunikomboa, bahati mbaya sana naona maamuzi ya serikali kwenye kilimo yanaturudisha nyuma nap engine kutukatisha tamaa.
Leo unawekeza mtaji, na labda unakopa vifaa vya kilimo unaamua kulima kisasa kabisa kwa mfano zao la mpunga ambalo binafsi niliamua kulima. Pembejeo ziko juu, na gharama zingine za uzalishaji. Kwa mfano kama unaamua kulima kilomo cha kisasa mvua zinapokata inabidi kutumia mafuta ku pump maji kwenye mashamba. Zote hizi ni gharama za uzalishaji na zitarudi pale utakapokutana na bei nzuri ya soko.
Kwa bahati mbaya sana serikali imekuwa ikifanya juhudi kudhibiti bei na kumdhibi mkulima, kwa lugha nyingine serikali inanyonya watu wake yenyewe. Inafikia sehemu tunasikia kauli kwamba chakula kisitoke nje ya mkoa kwenda mkoa mwingine. Maamuzi ya aina hii hayana tija na hayawezi saidia kukuza kilimo.
MAOMBI:
Serikali iache soko huru. Ipunguze excessive regulation ya bei na soko. Unaweza kukuza kilimo pale kunapokuwa na uhakika wa soko na bei. Mkulima atafute soko la nje kama soko la ndani si zuri. Auze mazao yake sehemu yoyote ile anayoona itamlipa.
Pia serikali isaidie kupunguza gharama za uzalishaji kwa kuweka miundombinu ya umwagiliaji na kukodisha kwa vijana walioamua kujiajiri kwa bei nafuu ili gharama za uzalishaji zisiwe kubwa.
Leo unawekeza mtaji, na labda unakopa vifaa vya kilimo unaamua kulima kisasa kabisa kwa mfano zao la mpunga ambalo binafsi niliamua kulima. Pembejeo ziko juu, na gharama zingine za uzalishaji. Kwa mfano kama unaamua kulima kilomo cha kisasa mvua zinapokata inabidi kutumia mafuta ku pump maji kwenye mashamba. Zote hizi ni gharama za uzalishaji na zitarudi pale utakapokutana na bei nzuri ya soko.
Kwa bahati mbaya sana serikali imekuwa ikifanya juhudi kudhibiti bei na kumdhibi mkulima, kwa lugha nyingine serikali inanyonya watu wake yenyewe. Inafikia sehemu tunasikia kauli kwamba chakula kisitoke nje ya mkoa kwenda mkoa mwingine. Maamuzi ya aina hii hayana tija na hayawezi saidia kukuza kilimo.
MAOMBI:
Serikali iache soko huru. Ipunguze excessive regulation ya bei na soko. Unaweza kukuza kilimo pale kunapokuwa na uhakika wa soko na bei. Mkulima atafute soko la nje kama soko la ndani si zuri. Auze mazao yake sehemu yoyote ile anayoona itamlipa.
Pia serikali isaidie kupunguza gharama za uzalishaji kwa kuweka miundombinu ya umwagiliaji na kukodisha kwa vijana walioamua kujiajiri kwa bei nafuu ili gharama za uzalishaji zisiwe kubwa.