Ndallo
JF-Expert Member
- Oct 1, 2010
- 7,619
- 4,292
Kutokana na majanga yaliyojitokeza kwa upande wa ukanda huu wa East Africa nikimaanisha Kenya na Tanzania kutokana na majanga makubwa kuzikumba nchi hizi mbili, moja ni hili la meli kuzama huko Pemba na kuuwa zaidi ya watu 190 usiku wa kuamkia Jumapili! bado tena hapo jana asubuhi tumesikia tena nchini Kenya zaidi ya watu 100 kufariki na kuteketea kabisa na kuwa majivu baada ya bomba la mafuta kupasuka! Je wamarekani wakiwa wanaadhimisha miaka 10 tokea kwa majengo pacha kushambuliwa na magaidi na sisi September hii East Africa tumepata janga kubwa tena la kitaifa, tumemkosea nini Mungu? Tunatakiwa kusali mno! Eeeh Mungu twakuomba uzipokee roho za marehemu na kuziweka maali pema peponi Amina.