FRANCIS DA DON
JF-Expert Member
- Sep 4, 2013
- 36,060
- 40,723
‘Seppuku’ au ‘Harakiri’ inamaanisha “kukata tumbo kwa kisu”, hii ni aina ya tamaduni ya kujikafiri kwa kujikata na kulichana tumbo kwa kisu iliyokuwa ikifanyika Japan ya kale. Mila hii ya kikatili ilikuwa maalum tu kwa makamanda wa ki- ‘Samurai’ , lakini pia ilitumika ma wa –Japan wengine wa kawaida ili kurejesha heshima yao au ya familia na koo zao.
Mila hii ya ‘Seppuku’ iliyokuwa maalum kwa ma-‘Samurai’, iliweza kufanywa kwa hiari na makamanda ili aweze kufa kwa heshima na kuepuka kukamatwa na adui vitani pamoja na kuepuka kuteswa pale atakapokuwa mateka. Lakini pia ‘Seppuku’ iliweza kutumika kama adhabu ya kifo kwa ma-‘Samurai’ waliofanya makosa mazito sana au waliofanya matendo ya aibu yalioleta fedheha kubwa sana.
‘Sherehe’ ya kujipasua tumbo ambayo ni sehemu ya tamaduni katika utekelezaji wa adhabu ya ‘Seppuku’ huwa inafanyika mbele ya kadamnasi ya watazamaji, na huwa inahusisha kujichoma kisu kifupi maalum, ambacho kiasili kiliitwa ‘Tanto’, kwenye tumbo na kisha kukata tumbo kwa mtindo wa kulichana kutoka kushoto kuelekea kulia hadi viungo vya ndani ya tumbo vimwagike. Kama kisu kitazama ndani vya kutosha basi inaweza ikaukata mshipa mkubwa wa damu wa ‘aorta’ na kusababisha kifo cha haraka kutokana na kupoteza damu nyingi.
Kisa cha kwanza kurekodiwa cha ‘Seppuku’ kilitekelezwa na Minamoto no Yorimasa katika vita ya ‘Uji’ mnamo mwaka 1180. ‘Seppuku’ ilitumika na makamanda ili kuepuka kutekwa na adui na pia kuondoa aibu pamoja na mateso atakayoyapata pale atakapokuwa mateka. Ma- ‘Samurai’ pia waliweza kuamrishwa na wakuu wao kujikafiri kwa njia ya ‘Seppuku’. Baadae pia, makamanda walioleta aibu na fedheha waliruhusiwa kujiua wenyewe kwa mtindo wa ‘Seppuku’ badala ya kuuawa kwa njia nyingine za kawaida.
Njia ya ‘Seppuku’ iliyokuwa inatumiwa sana na wanaume ni ile ambayo baada ya kujichoma kisu na kulichana tumbo lake, mhusika aliinamisha shingo ili msaidizi wake aikate shingo yake kwa pigo moja tu kwa kutumia panga maalum.
Msaidizi alitarajiwa kuikata shingo kwa pigo moja tu la haraka, vinginevyo akishindwa inakuwa ni aibu kubwa sana kwake na kwa familia yake. Wale ambao hawakuwa sehemu ya watu wa ‘Samurai’ hawakupewa amri wala kutarajiwa kufanya ‘Seppuku’. Na hata ‘Samura’ waliruhusiwa kufanya ‘Seppuku’ kwa ruhusa tu.
DON FRANCIS
================================
Update: 18/06/2021
Mila hii ya ‘Seppuku’ iliyokuwa maalum kwa ma-‘Samurai’, iliweza kufanywa kwa hiari na makamanda ili aweze kufa kwa heshima na kuepuka kukamatwa na adui vitani pamoja na kuepuka kuteswa pale atakapokuwa mateka. Lakini pia ‘Seppuku’ iliweza kutumika kama adhabu ya kifo kwa ma-‘Samurai’ waliofanya makosa mazito sana au waliofanya matendo ya aibu yalioleta fedheha kubwa sana.
‘Sherehe’ ya kujipasua tumbo ambayo ni sehemu ya tamaduni katika utekelezaji wa adhabu ya ‘Seppuku’ huwa inafanyika mbele ya kadamnasi ya watazamaji, na huwa inahusisha kujichoma kisu kifupi maalum, ambacho kiasili kiliitwa ‘Tanto’, kwenye tumbo na kisha kukata tumbo kwa mtindo wa kulichana kutoka kushoto kuelekea kulia hadi viungo vya ndani ya tumbo vimwagike. Kama kisu kitazama ndani vya kutosha basi inaweza ikaukata mshipa mkubwa wa damu wa ‘aorta’ na kusababisha kifo cha haraka kutokana na kupoteza damu nyingi.
Kisa cha kwanza kurekodiwa cha ‘Seppuku’ kilitekelezwa na Minamoto no Yorimasa katika vita ya ‘Uji’ mnamo mwaka 1180. ‘Seppuku’ ilitumika na makamanda ili kuepuka kutekwa na adui na pia kuondoa aibu pamoja na mateso atakayoyapata pale atakapokuwa mateka. Ma- ‘Samurai’ pia waliweza kuamrishwa na wakuu wao kujikafiri kwa njia ya ‘Seppuku’. Baadae pia, makamanda walioleta aibu na fedheha waliruhusiwa kujiua wenyewe kwa mtindo wa ‘Seppuku’ badala ya kuuawa kwa njia nyingine za kawaida.
Njia ya ‘Seppuku’ iliyokuwa inatumiwa sana na wanaume ni ile ambayo baada ya kujichoma kisu na kulichana tumbo lake, mhusika aliinamisha shingo ili msaidizi wake aikate shingo yake kwa pigo moja tu kwa kutumia panga maalum.
Msaidizi alitarajiwa kuikata shingo kwa pigo moja tu la haraka, vinginevyo akishindwa inakuwa ni aibu kubwa sana kwake na kwa familia yake. Wale ambao hawakuwa sehemu ya watu wa ‘Samurai’ hawakupewa amri wala kutarajiwa kufanya ‘Seppuku’. Na hata ‘Samura’ waliruhusiwa kufanya ‘Seppuku’ kwa ruhusa tu.
DON FRANCIS
================================
Update: 18/06/2021