Senzo Mthethwa yupo hai

Antony Fereji

Member
Sep 29, 2016
46
63
Kulikuwa na taarifa za muda mrefu kuwa msainii wa reggae wa Afrika kusini, Senzo Mthethwa, ameuawa na marehemu Lucky Dube. Senzo aliyepakua album nne: "Nothing But Prayer", " Irene", "Worshiping Your Love", "Am Sorry", alisimama kuimba tangu mwaka 1999 baada ya kuugua na kupoteza sauti. Senzo aliugua mwaka 1999 alipoenda kufanya 'live show' nchini Malawi. Nilipo ongea na Senzo mwenyewe, mara ya kwanza aliniambia kuwa aliugua malaria kali nakupoteza sauti yake. Lakini baadae, baada ya kuzoeana, alidai kuwa alifanyiwa 'African sciece' na msanii wa reggae wa Malawi atwaye Banda.

Senzo anadai siku alipoingia Malawi alipata mapokezi makubwa ambayo hakuwahi kuyaona ktk maisha yake. Mapokezi hayo yalimfanya Banda akasirike nakuapa kufanya chochote ili kumfifisha Senzo, kwani yeye hakuwahi kuthaminiwa hivyo japo alikuwa msanii mkubwa wa reggae huko Malawi. Senzo alianza kuugua ghafla, akashindwa kufanya onyesho lake. Maisha yake tangu mwaka 1999 yamekuwa ya taabu sana, alipoteza sauti, alikuwa kama mtu asiye jitambua. Lakini Mungu si binadamu, Senzo alianza kupata nafuu tangu mwaka juzi. Anapigana kwa udi na uvumba kurudisha sauti yake, pia anampango wa kutoa album mpya na kuzitolea video nyimbo zake za zamani.

Senzo amekanusha kuwahi kufanya kazi na Lucky Dube. Amedai kuna mtu alikuwepo kwenye bendi ya Lucky Dube alifanana nae tu. Pia amesikitika sana baada ya taarifa kuenea kuwa aliuawa na Lucky Dube. Amedai hakuwahi kuwa na ugomvi na Lucky Dube, wala ugomvi na chuki sio fani yake.

Akiwa na miaka 46, je ataweza kuzitendea haki nyimbo zake za zamani kwa kuzifanyia video? He is a peace soldier.

 
Duh huyu jamaaa si tulisikiaga amededi kitambo???weka picha ntakuamini
 

Attachments

  • senzo.PNG
    senzo.PNG
    150.6 KB · Views: 1,234
Nilipenda sana muziki wa huyu ndugu. Na nilipata shida sana kuupata ukweli wa aidha alishakufa na katika mazingira gani. Majuzi juzi hapa kwenye post ya kutimiza miaka kumi ya kifo cha Lucky Dube,hili la kuuwawa Senzo liliibuka tena ndipo nikapata shauku ya kuutafuta ukweli. Finally nikapata hii documentary yake. Inasikitisha sana, kwa sababu inaonesha maradhi ya cerebral malaria yalimharibia sana, kwa sababu hata kuongea kwake tu si kwa kawaida tena. Si Senzo wa nyimbo zile za Irene, Peace Soldier etc. Kweli hujafa hujaumbika. Video yake hiyo hapo chini.

 
Kulikuwa na taarifa za muda mrefu kuwa msainii wa reggae wa Afrika kusini, Senzo Mthethwa, ameuawa na marehemu Lucky Dube. Senzo aliyepakua album nne: "Nothing But Prayer", " Irene", "Worshiping Your Love", "Am Sorry", alisimama kuimba tangu mwaka 1999 baada ya kuugua na kupoteza sauti. Senzo aliugua mwaka 1999 alipoenda kufanya 'live show' nchini Malawi. Nilipo ongea na Senzo mwenyewe, mara ya kwanza aliniambia kuwa aliugua malaria kali nakupoteza sauti yake. Lakini baadae, baada ya kuzoeana, alidai kuwa alifanyiwa 'African sciece' na msanii wa reggae wa Malawi atwaye Banda.

Senzo anadai siku alipoingia Malawi alipata mapokezi makubwa ambayo hakuwahi kuyaona ktk maisha yake. Mapokezi hayo yalimfanya Banda akasirike nakuapa kufanya chochote ili kumfifisha Senzo, kwani yeye hakuwahi kuthaminiwa hivyo japo alikuwa msanii mkubwa wa reggae huko Malawi. Senzo alianza kuugua ghafla, akashindwa kufanya onyesho lake. Maisha yake tangu mwaka 1999 yamekuwa ya taabu sana, alipoteza sauti, alikuwa kama mtu asiye jitambua. Lakini Mungu si binadamu, Senzo alianza kupata nafuu tangu mwaka juzi. Anapigana kwa udi na uvumba kurudisha sauti yake, pia anampango wa kutoa album mpya na kuzitolea video nyimbo zake za zamani.

Senzo amekanusha kuwahi kufanya kazi na Lucky Dube. Amedai kuna mtu alikuwepo kwenye bendi ya Lucky Dube alifanana nae tu. Pia amesikitika sana baada ya taarifa kuenea kuwa aliuawa na Lucky Dube. Amedai hakuwahi kuwa na ugomvi na Lucky Dube, wala ugomvi na chuki sio fani yake.

Akiwa na miaka 46, je ataweza kuzitendea haki nyimbo zake za zamani kwa kuzifanyia video? He is a peace soldier.
Great News! Niliumia saaaaana Sana. Mungu mkubwa Sana. Rudi Senzo
 
Habari,

Leo nilikuwa naperuzi online nikawa nasikiliza nyimbo za Reggae za mwanamuziki wa miaka ya 90s Senzo Mthethwa.

Cha ajabu kilichonishangaza ni baada ya kupata habari kuwa Jamaa bado ni mzima na anaishi Afrika Kusini hadi sasa.

Ila alisimamisha shughuli za muziki mwanzoni mwa mwaka 1999 baada ya kupata ugonjwa ujulikanao kitaalam kama "Cerebral Maria Infection" uliomsababishia kuweza kuzungumza vyema.

Hii ndiyo ilikuwa sababu ya yeye kukaa kimya miaka yote! Ila watu kila pembe ya dunia wanajua kuwa jamaa alishavuta kitambo.

Jamaa ni mzima na hii ni video yake fupi akikanusha rumours kuwa Alifariki.

 
Back
Top Bottom