Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,499
- 9,279
Polisi nchini Haiti imesema seneta wa zamani ambaye ni mshukiwa mkuu katika mauaji ya aliyekuwa rais wa nchi hiyo Jovenal Moise ametiwa mbaroni nchini Jamaica.
Msemaji wa jeshi la polisi Gary Desrosiers [Derosieri] ameliambia shirika la habari la Associated Press kwamba John Joel Joseph yuko chini ya ulinzi katika mahabusi. Hakuna taarifa zaidi zilizopatikana kuhusu kukamatwa kwake.
Wakati hayo yakijiri kamanda wa jeshi la polisi nchini Jamaica Stephanne Lindsay ameliambia shirika la habari hilo hilo kwamba watu wengine wamekamatwa pamoja na Joseph na maafisa wanajaribu kubaini ikiwa ni jamaa wa familia.
Kamanda huyo amethibirisha watu hao walikamatwa Jumamosi alfajiri lakini akakataa kutoa taarifa zaidi. Watu waliokuwa na silaha waliyavamia makazi binafsi ya rais Moise katika vilima vya mji wa Port-au-Prince Julai saba mwaka uliopita na kumuuwa kwa risasi.
DW Swahili
Msemaji wa jeshi la polisi Gary Desrosiers [Derosieri] ameliambia shirika la habari la Associated Press kwamba John Joel Joseph yuko chini ya ulinzi katika mahabusi. Hakuna taarifa zaidi zilizopatikana kuhusu kukamatwa kwake.
Wakati hayo yakijiri kamanda wa jeshi la polisi nchini Jamaica Stephanne Lindsay ameliambia shirika la habari hilo hilo kwamba watu wengine wamekamatwa pamoja na Joseph na maafisa wanajaribu kubaini ikiwa ni jamaa wa familia.
Kamanda huyo amethibirisha watu hao walikamatwa Jumamosi alfajiri lakini akakataa kutoa taarifa zaidi. Watu waliokuwa na silaha waliyavamia makazi binafsi ya rais Moise katika vilima vya mji wa Port-au-Prince Julai saba mwaka uliopita na kumuuwa kwa risasi.
DW Swahili