STRUGGLE MAN
JF-Expert Member
- May 31, 2018
- 8,638
- 16,566
Seneta wa Marekani aituhumu China kuwa ndio imeunda virusi vya Corona
Feb 17, 2020 11:42 UTC
[https://media]
Seneta mmoja wa Marekani amesema kuwa virusi vya Corona ni silaha ya kibaolojia ambayo imeundwa na jeshi la China.
Tom Cotton ameyasema hayo katika mahojiano na kanali ya Fox News na kudai kwamba ripoti kadhaa zinazosema kuwa virusi vya Corona vilianza kuenea katika soko la vyakula nchini China, hazina ukweli wowote na wala virusi hivyo havikuanzia katika soko la wanyama la mji huo wa Wuhan. Cotton ameongeza kwamba haijajulikana virusi vya Corona vilikuja kutokea wapi na kudai kuwa ni lazima chanzo chake kifahamike. Seneta huyo wa Marekani amebainisha kwamba, karibu na soko la vyakula la Wuhan ndiko kuliko na kituo cha uchunguzi wa kisasa cha China ambacho kinajihusisha na uchunguzi wa maradhi ya maambukizi ya binadamu.
[https://media]Tom Cotton, Seneta wa Marekani
Hata hivyo viongozi wa China wametupilia mbali madai ya Tom Cotton na kumtaja kuwa anayesema uongo kuhusiana na chanzo cha virusi vya Corona. Pamoja na hayo Cotton anasisitiza kuwa ni jukumu la serikali ya Beijing kuthibitishe kinyume cha madai kwamba virusi hivyo ni silaha ya kibaolojia. Tangu kulipoibuka virusi vya Corona, vyombo vya habari vinavyomilikiwa na vyama viwili vya Republican na Democrat nchini Marekani vimekuwa vikieneza propaganda dhidi ya China kuhusiana na chanzo cha virusi hivyo na namna ya kuvidhibiti.
Sent using Jamii Forums mobile app
Feb 17, 2020 11:42 UTC
[https://media]
Seneta mmoja wa Marekani amesema kuwa virusi vya Corona ni silaha ya kibaolojia ambayo imeundwa na jeshi la China.
Tom Cotton ameyasema hayo katika mahojiano na kanali ya Fox News na kudai kwamba ripoti kadhaa zinazosema kuwa virusi vya Corona vilianza kuenea katika soko la vyakula nchini China, hazina ukweli wowote na wala virusi hivyo havikuanzia katika soko la wanyama la mji huo wa Wuhan. Cotton ameongeza kwamba haijajulikana virusi vya Corona vilikuja kutokea wapi na kudai kuwa ni lazima chanzo chake kifahamike. Seneta huyo wa Marekani amebainisha kwamba, karibu na soko la vyakula la Wuhan ndiko kuliko na kituo cha uchunguzi wa kisasa cha China ambacho kinajihusisha na uchunguzi wa maradhi ya maambukizi ya binadamu.
[https://media]Tom Cotton, Seneta wa Marekani
Hata hivyo viongozi wa China wametupilia mbali madai ya Tom Cotton na kumtaja kuwa anayesema uongo kuhusiana na chanzo cha virusi vya Corona. Pamoja na hayo Cotton anasisitiza kuwa ni jukumu la serikali ya Beijing kuthibitishe kinyume cha madai kwamba virusi hivyo ni silaha ya kibaolojia. Tangu kulipoibuka virusi vya Corona, vyombo vya habari vinavyomilikiwa na vyama viwili vya Republican na Democrat nchini Marekani vimekuwa vikieneza propaganda dhidi ya China kuhusiana na chanzo cha virusi hivyo na namna ya kuvidhibiti.
Sent using Jamii Forums mobile app