Maoni: Tuunde Jeshi Maalum la Jumuiya ya Afrika Mashariki

comrade igwe

JF-Expert Member
Jan 12, 2015
7,295
3,939
Wana jamvi.

Wana jf
Salaam

Kutokana na maendeleo ya kidunia hasa kiulinzi baadhi ya nchi wanachama duniani wana majeshi ya pamoja mfano NATO kwa utekelezaji wa majukumu ya kimataifa, Hata nchi za Afrika Magharibi wana umoja wa majeshi yao ya ECOWAS ambayo hutekeleza majukumu yao katika nchi wanachama wao tu mfano baada ya uchaguzi wa Gambia na kupelekea Rais alieshindwa kugoma kuondoka madarakani, Majeshi ya ECOWAS yanajiandaa kuivamia kijeshi ili Rais alieshinda Adama Barrow akabidhiwe madaraka kwa amani bila kuvunja katiba.

Hivyo kuna haja jumuiya ya Afrika mashariki tuwe na jeshi maalumu ambalo litakua na utekelezaji wa majukumu maalumu tu, mfano kudhibiti maharamia kwa pamoja, kuingilia kati nchi mwanachama anapochokozwa na kuvamiwa na Majeshi ya nje ya Afrika Mashariki, kuingilia kijeshi nchi mwanachama yoyote anaetishia usalama wa mwenzake, kushauri kiongozi yoyote atakaeonesha nia ya kung'ang'ania madaraka baada ya muda kikatiba kuisha.

Aidha, Pia liwe na jukumu la kutekeleza majukumu ya taasisi za kiraia mfano kutoa msaada wa haraka kwa mwanachama yoyote aliekumbwa na majanga makubwa.
 
Shida tunatofautiana Sana ki philosophy
Wakati wenzetu ni mabepari, sisi ni wajamaa(mabepari uchwara)

Bado udikteta na kuchezea katiba kunakoendelea EAC.....
Wakati Kuna nchi ndani ya EAC hazijawah kubadili raisi toka 1986 Leo uje uwaongezee majeshi?
Ukishangaa ya Burundi utayaona ya Uganda, CCM, Zanzibar Na Rwanda.
 
Bado demokrasia ya kwetu imetushinda Leo tuichanganye na mnyanganyiko mwingine Haiwezekani East Africa
 
Si ingekuwa tumeshavamiwa Bara na Visiwani mpaka muda huu? Na vipi kuhusu Al shabaab si ingekuwa tumeshauvaa mkenge?
 
Tunashirikiana sana upande wa majeshi yetu hasa katika mafunzo na sherehe za kijeshi. Kimsingi majeshi yetu yako kulinda mipaka ya nchi zetu dhidi ya uvamizi kutoka nje, kulinda vizuri uongozi wa nchi uliowekwa madarakani na mamlaka za kiraia, kushiriki kulinda amani katika nchi zenye migogoro, kutoa huduma za dharura katika majanga kama mafuriko, nk. Kuunda jeshi la pamoja ni wazo zuri kwa EAC ila ukakasi utakuwa katika kuligharamia na kulitumia kwa mambo ya kisiara kama mtoa uzi anavyotanabaisha. Viongozi wetu hawana mwelekeo unaofanana na hakuna ambaye amefikia heshima kama ya Nyerere ambaye wenzake waliweza kumsikiliza.
 
Hamna lolote hapa mambo haya alikuwa anayaweza Muammar Gaddafi pekee alitaka kuunganisha Africa yote I we moja na mambo yetu tujitegemee wenyewe pasipo external aid lakini nchi vibaraka za Africa zikasambaza huo mpango, na wazungu walishampima jamaa wakamuwahii kabisaa, haya yote yasingetokeaa ya kuunda jeshi EAC
 
Sababu gani za kufanya tuwe na jeshi la EAC duniani jeshi pekee la jumuiya ambalo ni Active army ni NATO tu kwanza mnapoamua kuanzisha jeshi jambo la kwanza ni kuangalia kuna threat gani nje ya jumuiya yenu lakini kwa EAC hakuna threat yeyote kutoka nje ya jumuiya yetu kuanzia kijeshi au kiusalama so hakuna sababu ya sisi kuwa na jeshi labda ikitokea tuchangie askari tu si kuwa na jeshi

ECOWAS hawana jeshi kama jeshi kwani kuta tofauti ya jeshi na kikosi cha askari jeshi ni taasisi yenye kujitegemea yenye askari na vifaa vyake na bajeti yake kikosi ni kila nchi inatoa wanajeshi na vifaa kuchangia kwa ajili ya mission flani baada ya mission kumalizika kila nchi inachukua wanajeshi wake na vifaa vyake
ECOWAS ina kikosi si jeshi kila nchi inachangia askari yake mfano Gambia nigeria na wenzie wametoa askari kwenda kumuondoa rais wa gambia lakini nataka kukwambia ECOWAS kama ecowas aina hata bunduki hata moja inayomiliki kama jumuiya kila nchi ikichangia wanajeshi wanakuja na vifaa na silaha zao kutoka nchi yao wanagawana tu labda nchi fulani inapigana kutokea angani nyingine majini nyingine nchi kavu sasa ilo uwezi kuliita ni jeshi hvyo ni vikosi tu aiwezekani kila nchi inawalipa wanajeshi wake inakuja na vifaa vyake ukaita ni jeshi

NATO hili ndilo jeshi la jumuiya kwani wana jeshi kama jeshi si kuchangiwa askari bali wanachukua vijana wenyenye kutoka nchi wanachama na kuwafundisha wana vifaa vyao vya kijeshi vyote unavyovijua na usivyovijua wanabajeti yao na wanawalipa mishahara askari yao wenyewe kama jumuiya kila nchi inachangia ada ya jumuiya na jeshi lilitengenezwa na US na EU kwa ajili ya kujihami dhidi ya Russia ndo maana linaitwa jeshi ya kujihami

Kuwa na jeshi ni gharama sana nataka kuwambia kila dola 100 duniani dola 60 inatumika kwa mambo ya ulinzi na usalama kwani vifaa vya kijeshi na ulinzi au usalama ni gharama sana kuliko vifaa vya kiraia mfano ndege moja ya jeshi unaweza kuipata kwa dola 50 milion lakini gharama za matengenezo,instalation, na gharama za uendeshaji ni kubwa sana na itaendelea kuwa kubwa kadili ya ndege inavyotumika mfano NATO US anachangia bajeti ya nato kwa 50% huku UK 10% Germany 10% France 10% na 20% nchi zingine wanachama na kuna nchi zingine hazichangii au kuleta michango kwa wakati

Kutokana na gharama kuwa kubwa sidhani kama kwa kipindi hiki cha Trump NATO itaendelea kuwapo kwani ameshasema aiwezekani US achangie gharama kubwa kuwalinda wengine inatakiwa wachangie wote sawa yani kila mwanachama achangie sawa kitu ambacho aiwezekani aya UK amejitoa ndani ya umoja wa Ulaya na Trump kasema UK kujitoa EU ulikuwa ni uhamuzi sahii sana so sidhani kama ada ya EU ataendelea kutoa pia Mahusiano kati ya US na Russia yanakwenda kuimalika na Trump ameonyesha kuegemea zaid kwa Russia kuliko Ulaya sasa hapo dah lakini tungoje muda utaongea
 
A cha porojo ECOWAS ina kokosi cha kijeshi kinaitwa ecomog mbona unapotosha uma?
Sababu gani za kufanya tuwe na jeshi la EAC duniani jeshi pekee la jumuiya ambalo ni Active army ni NATO tu kwanza mnapoamua kuanzisha jeshi jambo la kwanza ni kuangalia kuna threat gani nje ya jumuiya yenu lakini kwa EAC hakuna threat yeyote kutoka nje ya jumuiya yetu kuanzia kijeshi au kiusalama so hakuna sababu ya sisi kuwa na jeshi labda ikitokea tuchangie askari tu si kuwa na jeshi

ECOWAS hawana jeshi kama jeshi kwani kuta tofauti ya jeshi na kikosi cha askari jeshi ni taasisi yenye kujitegemea yenye askari na vifaa vyake na bajeti yake kikosi ni kila nchi inatoa wanajeshi na vifaa kuchangia kwa ajili ya mission flani baada ya mission kumalizika kila nchi inachukua wanajeshi wake na vifaa vyake
ECOWAS ina kikosi si jeshi kila nchi inachangia askari yake mfano Gambia nigeria na wenzie wametoa askari kwenda kumuondoa rais wa gambia lakini nataka kukwambia ECOWAS kama ecowas aina hata bunduki hata moja inayomiliki kama jumuiya kila nchi ikichangia wanajeshi wanakuja na vifaa na silaha zao kutoka nchi yao wanagawana tu labda nchi fulani inapigana kutokea angani nyingine majini nyingine nchi kavu sasa ilo uwezi kuliita ni jeshi hvyo ni vikosi tu aiwezekani kila nchi inawalipa wanajeshi wake inakuja na vifaa vyake ukaita ni jeshi

NATO hili ndilo jeshi la jumuiya kwani wana jeshi kama jeshi si kuchangiwa askari bali wanachukua vijana wenyenye kutoka nchi wanachama na kuwafundisha wana vifaa vyao vya kijeshi vyote unavyovijua na usivyovijua wanabajeti yao na wanawalipa mishahara askari yao wenyewe kama jumuiya kila nchi inachangia ada ya jumuiya na jeshi lilitengenezwa na US na EU kwa ajili ya kujihami dhidi ya Russia ndo maana linaitwa jeshi ya kujihami

Kuwa na jeshi ni gharama sana nataka kuwambia kila dola 100 duniani dola 60 inatumika kwa mambo ya ulinzi na usalama kwani vifaa vya kijeshi na ulinzi au usalama ni gharama sana kuliko vifaa vya kiraia mfano ndege moja ya jeshi unaweza kuipata kwa dola 50 milion lakini gharama za matengenezo,instalation, na gharama za uendeshaji ni kubwa sana na itaendelea kuwa kubwa kadili ya ndege inavyotumika mfano NATO US anachangia bajeti ya nato kwa 50% huku UK 10% Germany 10% France 10% na 20% nchi zingine wanachama na kuna nchi zingine hazichangii au kuleta michango kwa wakati

Kutokana na gharama kuwa kubwa sidhani kama kwa kipindi hiki cha Trump NATO itaendelea kuwapo kwani ameshasema aiwezekani US achangie gharama kubwa kuwalinda wengine inatakiwa wachangie wote sawa yani kila mwanachama achangie sawa kitu ambacho aiwezekani aya UK amejitoa ndani ya umoja wa Ulaya na Trump kasema UK kujitoa EU ulikuwa ni uhamuzi sahii sana so sidhani kama ada ya EU ataendelea kutoa pia Mahusiano kati ya US na Russia yanakwenda kuimalika na Trump ameonyesha kuegemea zaid kwa Russia kuliko Ulaya sasa hapo dah lakini tungoje muda utaongea
 
Mkuu threats zinaweza zikawepo kutoka jumuiya nyingine fikiria figisu ya Mkataba wa EAC wa Economic Partnership Agreement ( EPA) ulivyotikiswa na EU yaani economic sabotage kutoka kwa bwana wale, fikiria Al shabab fikiria Geo politics za bwana wale, na mengine meeeeeengiiiiii usioyaona
 
A cha porojo ECOWAS ina kokosi cha kijeshi kinaitwa ecomog mbona unapotosha uma?
Hivi ww unaelewa maana ya jeshi la jumuiya kama jumuiya au kila nchi inachangia wanajeshi kwenye kikosi icho?? duniani jumuiya yenye jeshi kamili ni NATO tu kama kungekuwa na jeshi la jumuiya kwa nini nchi tena zinachangia wanajeshi kwenda kumtoa rais wa Gambia na majeshi yote yametokea kwao yanakutana Senegal ? ok nambie makao makuu ya hayo majeshi ya ecomog yako wapi na bajeti ya ilo jeshi kwa mwaka ni kiasi gani au ni nani anayewalipa mishahara hao wanajeshi wa ecomog kama wanalipwa na nchi zao utasemaje ilo ni jeshi kamili la jumuiya au jeshi la nchi husika ila wanachangia inapotokea mission ?
 
Back
Top Bottom