CHADEMA
JF-Expert Member
- Apr 13, 2013
- 488
- 2,468
TAARIFA KWA UMMA
KILA LA HERI TIMU YA TAIFA, TAIFA STARS
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kupitia kwa Mwenyekiti wa Chama Taifa, Mhe. Freeman Mbowe kimetuma salaam za kuitakia kila la heri Timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu, Taifa Stars na kuwatia ari wachezaji na makocha wao wakiongozwa na Ndugu Emmanuel Amunike, wakati timu hiyo inaelekea kuanza mchezo wake wa kwanza katika Mashindano ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2019) usiku wa leo, jijini Cairo, nchini Misri.
Kupitia ujumbe huo, Mwenyekiti Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na Mbunge wa Jimbo la Hai, ametoa wito kwa Watanzania wote bila kujali tofauti za itikadi zao, kushikamana kwa pamoja katika kuishangilia na kuitakia mafanikio Taifa Stars.
"Timu yetu ya Taifa leo usiku inaanza rasmi mashindano ya AfCON, Cairo, Misri. CHADEMA inawasihi Watanzania wote wa itikadi zote kushikamana katika kuitakia mafanikio timu yetu ya Taifa Stars. Michezo ni uchumi, afya, upendo, heshima, umoja na burudani. Tuitumie AFCON kujirekebisha," amesema Mwenyekiti Mbowe.
Timu ya Taifa Stars ambayo imepangwa Kundi C pamoja na timu za Senegal, Algeria na Kenya, itacheza mechi yake ya kwanza Jumapili, Juni 23, 2019 dhidi ya Timu ya Taifa ya Senegal, katika mchezo utakaopigwa June Stadium, jijini Cairo, nchini Misri, kuanzia saa 2 usiku.
Kila la heri Taifa Stars.
Kila la heri Watanzania.
Imetolewa leo Jumapili, Juni 23, 2019 na;
Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA
KILA LA HERI TIMU YA TAIFA, TAIFA STARS
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kupitia kwa Mwenyekiti wa Chama Taifa, Mhe. Freeman Mbowe kimetuma salaam za kuitakia kila la heri Timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu, Taifa Stars na kuwatia ari wachezaji na makocha wao wakiongozwa na Ndugu Emmanuel Amunike, wakati timu hiyo inaelekea kuanza mchezo wake wa kwanza katika Mashindano ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON 2019) usiku wa leo, jijini Cairo, nchini Misri.
Kupitia ujumbe huo, Mwenyekiti Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni na Mbunge wa Jimbo la Hai, ametoa wito kwa Watanzania wote bila kujali tofauti za itikadi zao, kushikamana kwa pamoja katika kuishangilia na kuitakia mafanikio Taifa Stars.
"Timu yetu ya Taifa leo usiku inaanza rasmi mashindano ya AfCON, Cairo, Misri. CHADEMA inawasihi Watanzania wote wa itikadi zote kushikamana katika kuitakia mafanikio timu yetu ya Taifa Stars. Michezo ni uchumi, afya, upendo, heshima, umoja na burudani. Tuitumie AFCON kujirekebisha," amesema Mwenyekiti Mbowe.
Timu ya Taifa Stars ambayo imepangwa Kundi C pamoja na timu za Senegal, Algeria na Kenya, itacheza mechi yake ya kwanza Jumapili, Juni 23, 2019 dhidi ya Timu ya Taifa ya Senegal, katika mchezo utakaopigwa June Stadium, jijini Cairo, nchini Misri, kuanzia saa 2 usiku.
Kila la heri Taifa Stars.
Kila la heri Watanzania.
Imetolewa leo Jumapili, Juni 23, 2019 na;
Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA