Njowepo
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 9,710
- 2,226
Mawaziri wapigwa 'stop'
Katika hatua nyingine mawaziri wote wamezuiwa kusafiri kikazi nje ya Jiji la Dar es Salaam kutokana na kile ambacho kinaelezwa kuwa ni maandalizi ya kukabidhi ofisi kwa mawaziri wapya ambao wanatarajiwa kutangazwa wakati wowote kuanzia sasa.
Taarifa hizo zimekuja siku moja tu tangu Ikulu kupitia kwa Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue kusema kuwa Watanzania wasubiri Baraza bora la Mawaziri.
Jana, taarifa kutoka vyanzo mbalimbali vya habari serikalini vililidokeza gazeti hili kuwa mawaziri wote sasa wamezuiwa kusafiri nje ya Dar es Salaam kutokana na kusubiri mchakato huo wa kukabidhiana ofisi.
Kwa mujibu wa vyanzo hivyo, karibu mawaziri wote na naibu mawaziri walikuwepo jijini Dar es Salaam jana isipokuwa wachache ambao haikuthibitika mara moja kama walikuwapo au la.
Vyanzo hivyo viliongeza kwamba tayari Rais amekwishamaliza mchakato wa uteuzi na baraza jipya linatarajiwa kukutana na mkuu huyo wa nchi katika semina elekezi Jumanne ya Mei 8, mwaka huu.
Kwa wiki mbili mfulululizo sasa nchi imegubikwa na mjadala kwa watu wa kada tofauti kushinikiza kufanyika mabadiliko ya Baraza la Mawaziri baada ya Bunge kutaka mawaziri wanane waliotajwa kwenye Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh wawajibike au wawajibishwe.
Mawaziri wanaotakiwa kuwajibishwa baada ya kushindwa kuwajibika ni Mustafa Mkulo (Fedha), Omary Nundu (Uchukuzi), Dk Hadji Mponda (Afya na Ustawi wa Jamii), Profesa Jumanne Maghembe (Kilimo, Chakula na Ushirika), Dk Cyril Chami (Viwanda na Biashara), George Mkuchika (Tamisemi), Ezekiel Maige (Maliasili na Utalii), William Ngeleja
(Nishati na Madini).
http://www.mwananchi.co.tz/componen.../22592-jk-apandisha-joto-uteuzi-mawaziri.html
MY TAKE;
So JK ana siku 4 kulitangaza na kuliapisha baraza jipya kabla ya semina elekezi!
Alafu kitengo cha mda wote huo hawa old minister wakiwa kwa transit si wanaweza poteza ushahidi wa kuwapeleka mahakani?Au ni strategy ya mkuu ili jamaa wasiende lupango mwisho wa siku kama dana dana za Yona na Mramba
Katika hatua nyingine mawaziri wote wamezuiwa kusafiri kikazi nje ya Jiji la Dar es Salaam kutokana na kile ambacho kinaelezwa kuwa ni maandalizi ya kukabidhi ofisi kwa mawaziri wapya ambao wanatarajiwa kutangazwa wakati wowote kuanzia sasa.
Taarifa hizo zimekuja siku moja tu tangu Ikulu kupitia kwa Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue kusema kuwa Watanzania wasubiri Baraza bora la Mawaziri.
Jana, taarifa kutoka vyanzo mbalimbali vya habari serikalini vililidokeza gazeti hili kuwa mawaziri wote sasa wamezuiwa kusafiri nje ya Dar es Salaam kutokana na kusubiri mchakato huo wa kukabidhiana ofisi.
Kwa mujibu wa vyanzo hivyo, karibu mawaziri wote na naibu mawaziri walikuwepo jijini Dar es Salaam jana isipokuwa wachache ambao haikuthibitika mara moja kama walikuwapo au la.
Vyanzo hivyo viliongeza kwamba tayari Rais amekwishamaliza mchakato wa uteuzi na baraza jipya linatarajiwa kukutana na mkuu huyo wa nchi katika semina elekezi Jumanne ya Mei 8, mwaka huu.
Kwa wiki mbili mfulululizo sasa nchi imegubikwa na mjadala kwa watu wa kada tofauti kushinikiza kufanyika mabadiliko ya Baraza la Mawaziri baada ya Bunge kutaka mawaziri wanane waliotajwa kwenye Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh wawajibike au wawajibishwe.
Mawaziri wanaotakiwa kuwajibishwa baada ya kushindwa kuwajibika ni Mustafa Mkulo (Fedha), Omary Nundu (Uchukuzi), Dk Hadji Mponda (Afya na Ustawi wa Jamii), Profesa Jumanne Maghembe (Kilimo, Chakula na Ushirika), Dk Cyril Chami (Viwanda na Biashara), George Mkuchika (Tamisemi), Ezekiel Maige (Maliasili na Utalii), William Ngeleja
(Nishati na Madini).
http://www.mwananchi.co.tz/componen.../22592-jk-apandisha-joto-uteuzi-mawaziri.html
MY TAKE;
So JK ana siku 4 kulitangaza na kuliapisha baraza jipya kabla ya semina elekezi!
Alafu kitengo cha mda wote huo hawa old minister wakiwa kwa transit si wanaweza poteza ushahidi wa kuwapeleka mahakani?Au ni strategy ya mkuu ili jamaa wasiende lupango mwisho wa siku kama dana dana za Yona na Mramba