bendaki
JF-Expert Member
- Feb 5, 2013
- 952
- 346
CCM huko nyuma ilichukua pesa kutoka serikali kuu na kuanzisha miradi ya kiuchumi. Kulikuwepo na maduka mf super market pale kidongo chekundu, kilimo na kufuga samaki bonde la msimbazi, mahotel, viwanja vya michezo, nk. Hivi vyote hatuvioni kabisa au kama vipo ni magofu. Lile neno SUKITA halitajwi kabisa. Kwa kuwa hii pesa ilitokana na mikopo ya muda mrefu kwa serikali kuu wakati chama kimeshika patamu, sasa miradi iko wapi? CGA anataarifa nayo? Je madeni yake tunaendelea kulipa watz wote? Kuna tunaloweza kujifunza kutokana na yaliyojiri ktk eneo hili?