#COVID19 Sekta ya Afya yaanza utafiti ikiwemo kubaini waliochanjwa wamepata Kinga kiasi gani

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,495
9,275
Sekta imeanza kufanya tafiti sita (6) kuhusu tabia za virusi za virusi vya Korona kwa kuangalia 1) askari wa kinga mwili (antibodies); 2) uelewa, mtazamo na utendaji (KAP Study); 3) utafiti wa kimatibabu (Clinical trials); 4) kuchunguza mpangilio wa vinasaba (Gene sequencing); 5) hali ya kimelea kubadili hali/vinasaba vyake vyas awali, na; 6) utafiti wa tiba asili.

Matokeo ya tafiti hizo, ni pamoja na; Kuwezesha Serikali kufahamu aina ya kirusi kilichopo nchini ili kufanya vipimo na kutoa chanjo; Kufahamu sababu za muitikio mdogo wa jamii katika kupata chanjo ya UVIKO - 19 hivyo kuishauri Srikali njia sahihi ya kuongeza muitikio.

Kufahamu ufanisi wa dawa za asili katika kupambana na UVIKO - 19 na kuishauri Serikali; Kufahamu madhara ya UVIKO - 19 kwa wagonjwa wanaopata maambuki; kufahamu viambata vilivyopo kwenye dawa za asili ambavyo vinasababisha utibabu wa korona na kufanya ugunduzi wa chanjo dhidi ya UVIKO-19.
 
"hivi umeshawahi kuona wapi chanjo inafanyiwa utafiti kwa mwaka mmoja" - dkt molell katika kipindi cha ajenda startv.leo hii anakuambia chanjo ni salama.je tumuelewe molel yupi?
 
salakasi zimeanza, wale wazee wa peoples power mnasikia ushauri wa wataalam wa uviko 19, kuna siku tutadungwa masindano ya sumu tuteketee sie wazee wa ''ndiooooo''
 
Kuna hela nyingi za rushwa kwenye hiyo chanjo, kwà hiyo matokeo yatakuwa hivi:

Chanjo ya Covid ni muhimu sana kwa kuwa ndiyo njia pekee ambayo inaweza kutumika kupambana na Covid.
 
Hao wizara ya afya si ndio walijenga kibanda cha kujifukiza hapo Muhimbili?
Ha ha ha! Ule ulikuwa mradi mkubwa kabisa wa hospitali yetu ya referral! Badala ya kufanya tafiti za maana, wanatafiti ni wangapi wamekufa baada ya chanjo!
 
ujenzi wa viwanda unaendelea kwa kasi
Mkoa Wa Pwani Viwanda 650
Hapo Kuna Vidogo, Size Ya Kati, Na Vikubwa
Mwijage Alikuwa Anaupiga Mwingi Mpaka Mzilankende Akamtimua Alipoona Kazidisha Propaganda
 
Mnaacha kufanya utafiti wa dawa ya kuitoa CCM madarakani mnahangaika na magonjwa ya kusadikika ambayo wazungu wanabuni ili wawamalize na ufala wenu.

We ungonjwa gani tishio watu tunapumuliana kama ng'ombe kwenye mwendo kasi, madaladala, basi za mikoani, masokoni humo, mbona tungepukutika kama kitu gani sijui.

Huu ukafiri wenu mnaofanya mtalipia hesabu siku ya kiama kushiriki dhambi ya kuangamiza kizazi cha waafrika wenzenu. Mnakazana kabisa kupambania chanjo chanjo chanjo sisi ni kuku wa nyama hadi mtulazimishie hivyo.....?!
 
Back
Top Bottom