Sekta binafsi isije kuwa mzigo kwa umma kutokana na mtazamo wa Rais Samia

kmbwembwe

JF-Expert Member
Aug 16, 2012
10,416
7,199
Kila nikimsikiliza rais Samia kuhusu mtazamo wake kushirikisha sekta binsfsi kutoa huduma kwa umma nakua na mashaka.

Sekta binafsi ni watafutaji wa faida. Dhana ya kusema serikali ishirikiane na sekta binafsi kutoa huduma kama afya elimu etc lazima itafsiriwe vyema isiweze kutumika vibaya ambapo vigogo Serikali wanaweza kushirikiana na watu binafsi kufanya ubadhirifu na wizi wa fedha za umma huku wananchi wakinyonywa na kupata huduma duni au watu binafsi wakitoa huduma hewa huku fedha ya serikali inaliwa.

Kinachotakiwa ni kampuni binafsi zenye uwezo kupewa fursa kutoa huduma ziada huku serikali ikifanya udhibiti kuona kuna bei wananchi wanazimudu kutokana na sekta binafsi kuendeshwa kwa tija.

Huko nyuma kuna mifano mingi ya ubabaishaji wa sekta binafsi kwa kufanya uhuni. Tunakumbuka richmond, iptl na ziko kampuni binafsi kibao za kujenga miradi ya maji iliyojenga miradi feki bila hata kutoa maji huku wakilipwa mabilioni ya fedha.

Kinachotakiwa ni serikali kufanya kazi kwa tija na kutimiza wajibu wake na sio kujidai kushirikiana na sekta binafsi ili kuwapa fursa wapigaji kuibia umma.

Tunataka sekta binafsi yenye tija uwezo wa mtaji na ujuzi kushirikiana na serikali sio wababaishaji na wahuni.
 
Ni mtazamo finyu kudhani Serikali inaporusu kitu inatakiwa ilale bila ku regulate.

Ni mtazamo finyu pia kudhani Nchi inaweza kuendelea bila sekta binafsi.

Nchi zenye maendeleo duniani zina sekta binafsi imara.
 
Umenikumbusha kuna KM na msaidizi wake mmoja 2016 walisambaza photocopy machine kwenye taasisi 35 za umma nchi nzima na hazikupiga hata copy moja kisa zililetwa bila wino zikabaki maonyesho mpaka leo
Mfumo wa CCM ni hatari sn
 
Hujui lolote kuhusu sekta binafsi. Inaonekana ni muajiliwa na Wala hujui kujishughulisha bila kuajiliwa ni sehemu ya sekta binafsi
 
Ni mtazamo finyu kudhani Serikali inaporusu kitu inatakiwa ilale bila ku regulate.

Ni mtazamo finyu pia kudhani Nchi inaweza kuendelea bila sekta binafsi.

Nchi zenye maendeleo duniani zina sekta binafsi imara.
Ni Kweli ila Kwa nchi hii au level ya nchi za kiafrika bado Sana... Sawa lengo ni faida ila hizi za Huku afrika na hapa Tanzania ni ufisadi mtupu na mambo ya hovyo
 
Nakumbuka miaka hiyo nilifanyaga research ya PPP (Public and Private Patnership). Bt nishayasahau yote. Ya mwilini yanachosha sana, nimeamua nizame rohoni totally. Nidili na ya milele. Nchi za ulimwengu wa tatu, ni tabu sana. Umasikini umeawapiga watu kiasi kwamba akipata nafasi anawaza kuiba tu.


YESU NI KRISTO
 
Tatizo watendaji wa serikali zetu ndio kikwazo sio sekta binafsi liweke hili sawa kwanza
 
Back
Top Bottom