VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,800
Katika kile kinachoonekana kama kujiosha kwa wananchi,Sekretarieti mpya ya CCM sasa imevuka mipaka.Imepewa kazi za Mawaziri ili izifanye. Kati ya kazi hizo ambazo hata Katibu wa Uenezi,Nape Nnauye amezikiri ni kumaliza tatizo la soko la korosho katika mkoa wa Mtwara(ambayo ni kazi ya Mawaziri wa Kilimo na Ushirika pamoja wa Viwanda na Biashara).Pia,kurejesha maeneo yaliyovamiwa katika mkoa wa Arusha(ambayo ni kazi ya Waziri wa Ardhi).
Hiyo itafanywa katika ziara zitakazoanza mikoani ambazo zitaihusisha Sekretarieti hiyo mpya chini ya Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana. Ziara hizo zimetafsiriwa na Wachambuzi wa mambo kama kuiga M4C ya CHADEMA ili kupunguza kasi ya chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania.
Ama kweli chama changu kinatapatapa.Kingeanza kwanza kwanza na kumalizia kujivua gamba halafu ndipo mambo hayo yafuate. Kweli tumeishiwa mbinu na malengo!
Hiyo itafanywa katika ziara zitakazoanza mikoani ambazo zitaihusisha Sekretarieti hiyo mpya chini ya Kanali Mstaafu Abdulrahman Kinana. Ziara hizo zimetafsiriwa na Wachambuzi wa mambo kama kuiga M4C ya CHADEMA ili kupunguza kasi ya chama hicho kikuu cha upinzani nchini Tanzania.
Ama kweli chama changu kinatapatapa.Kingeanza kwanza kwanza na kumalizia kujivua gamba halafu ndipo mambo hayo yafuate. Kweli tumeishiwa mbinu na malengo!