Sekretarieti ya Maadili kuhakiki Vigogo 658 wakiwemo Mawaziri na Makatibu Wakuu

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,365
8,097
Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma nchini Tanzania imewataka viongozi 658 waliochaguliwa kwa ajili ya uhakiki, kufanya maandalizi ya uhakiki huo.

Hayo yamesemwa leo Jumatano Novemba 2, 2022 na Kamishna wa Maadili Jaji Mstaafu Sivangilwa Mwangesi wakati akizungumzia kuhusiana na shughuli hiyo.

“Viongozi watakaohakikiwa ni baadhi ya mawaziri, naibu mawaziri, makatibu wakuu na wengine wa kada mbalimbali,” Amesema viongozi hao wataohakikiwa ni kutoka katika mikoa ya Kilimanjaro, Dar es Salaam, Lindi, Njombe, Dodoma, Tanga, Geita, Mwanza, Tabora na Iringa.

Amesema wananchi wenye taarifa muhimu kuhusiana na raslimali na madeni ya viongozi pia wanaombwa kutoa ushirikiano ili kufanikisha jukumu hili.

Aidha, amesema sektarieti inatoa rai kwa wakuu wa mikoa, makamanda wa polisi na mamlaka nyingine katika maeneo mbalimbali kutoa ushirikiano.
 
Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma nchini Tanzania imewataka viongozi 658 waliochaguliwa kwa ajili ya uhakiki, kufanya maandalizi ya uhakiki huo. Hayo yamesemwa leo Jumatano Novemba 2, 2022 na Kamishna wa Maadili Jaji Mstaafu Sivangilwa Mwangesi wakati akizungumzia kuhusiana na shughuli hiyo.

“Viongozi watakaohakikiwa ni baadhi ya mawaziri, naibu mawaziri, makatibu wakuu na wengine wa kada mbalimbali,” Amesema viongozi hao wataohakikiwa ni kutoka katika mikoa ya Kilimanjaro, Dar es Salaam, Lindi, Njombe, Dodoma, Tanga, Geita, Mwanza, Tabora na Iringa.

Amesema wananchi wenye taarifa muhimu kuhusiana na raslimali na madeni ya viongozi pia wanaombwa kutoa ushirikiano ili kufanikisha jukumu hili. Aidha, amesema sektarieti inatoa rai kwa wakuu wa mikoa, makamanda wa polisi na mamlaka nyingine katika maeneo mbalimbali kutoa ushirikiano.
SIASA TU INGEKUWA BAADA YA UHAKIKI TAARIFA ZAO ZINATANGAZWA ILI WANANCHI WAZIJUE NA KAMA WAMEDANGANYA WANANCHI WAJUE KAMA WENZETU WA NCHI YA KENYA LAKINI SISI INAKUWA SIRI
 
Kila Mtu akifanya kazi yake inapendeza Sana. Tume iendelee na kazi yake ya mapambio na kuficha maovu ya viongozi, Usanii wa maigizo kama huu waachiwe kina JB na Joti.
 
Na zile zinazoagiza yutong na scania na zenyewe zinahakikiwa vipi, maana huenda ukakutana na wamiliki feki........bongolala sanaa sana.
 
Back
Top Bottom