Sekretarieti ya Ajira: Tangazo la kuitwa kazini kwa waliofanya usaili Februari 8-15, 2019

Jamii Opportunities

JF-Expert Member
Feb 10, 2014
4,338
1,356
TANGAZO LA KUITWA KAZINI
Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma inapenda kuwataarifu waombaji kazi wa nafasi mbalimbali waliofanya usaili tarehe 08 – 15 Februari, 2019 kuwa majina ya waombaji kazi waliofaulu usaili huo na kupangiwa kituo cha kazi ni kama yalivyoorodheshwa katika tangazo hili.

Orodha ya majina haya pia inajumuisha baadhi ya wasailiwa waliokuwa kwenye kanzidata (Data base) kwa kada mbalimbali ambao wamepangiwa vituo vya kazi baada ya nafasi kupatikana.

Waombaji waliofaulu usaili wanatakiwa kuchukua barua za kupangiwa kituo cha kazi katika Ofisi za Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma zilizopo Barabara ya Kivukoni, Jengo la Utumishi, Masjala ya wazi ndani ya siku saba kutoka tarehe ya tangazo hili na baada ya hapo barua ambazo hazijachukuliwa na wahusika zitatumwa kupitia anuani zao za Posta.

Aidha, waombaji kazi waliofaulu usaili na kupangiwa kituo cha kazi wanatakiwa kuripoti kwa Mwajiri katika muda ambao umeainishwa kwenye barua za kupangiwa kituo cha kazi wakiwa na vyeti halisi (Originals Certificates) za masomo kuanzia kidato cha nne na kuendelea ili vihakikiwe na mwajiri kabla ya kupewa barua ya Ajira.

Kwa wale ambao majina yao hayapo katika tangazo hili watambue kuwa hawakupata nafasi/hawakufaulu usaili, hivyo wasisite kuomba kwa mara nyingine nafasi za kazi zitakapotangazwa.View attachment Tangazo kuitwa Kazini.pdf

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona zile nafasi za TRC hawajaita?
Usaili ulifanyika tarehe hizo hizo
Kuna jamaa nimemuuliza kaniambia hayo mashirika TRC na TPA wanasubiria wafanye vikao vya bodi vya mashirika yao ndio wabariki hizo ajira ndio waitwe changamoto alioniambia jamaa ni kwamba wanaoajiriwa na bodi ni nafasi za ukurugenzi tu hivyo basi hawa wanaotakiwa kuajiriwa Kama wakurugenzi ndio wanawachelewesha wenzao.
Sekretarieti ya ajira imeshamaliza kwa upande wao wanasubiri utaratibu mwingine ukamilike kwenye hayo mashirika na kanidokeza kwamba Kuna uwezekano hayo mashirika yenyewe ndio yakawaaita waliofaulu kazini.
 
Kuna jamaa nimemuuliza kaniambia hayo mashirika TRC na TPA wanasubiria wafanye vikao vya bodi vya mashirika yao ndio wabariki hizo ajira ndio waitwe changamoto alioniambia jamaa ni kwamba wanaoajiriwa na bodi ni nafasi za ukurugenzi tu hivyo basi hawa wanaotakiwa kuajiriwa Kama wakurugenzi ndio wanawachelewesha wenzao.
Sekretarieti ya ajira imeshamaliza kwa upande wao wanasubiri utaratibu mwingine ukamilike kwenye hayo mashirika na kanidokeza kwamba Kuna uwezekano hayo mashirika yenyewe ndio yakawaaita waliofaulu kazini.
That means kuna uwekano utumishi wasihusike tena kwenye kutoa hayo majina kwenye web yao au nimeelewa vibaya.....
 
Kuna jamaa nimemuuliza kaniambia hayo mashirika TRC na TPA wanasubiria wafanye vikao vya bodi vya mashirika yao ndio wabariki hizo ajira ndio waitwe changamoto alioniambia jamaa ni kwamba wanaoajiriwa na bodi ni nafasi za ukurugenzi tu hivyo basi hawa wanaotakiwa kuajiriwa Kama wakurugenzi ndio wanawachelewesha wenzao.
Sekretarieti ya ajira imeshamaliza kwa upande wao wanasubiri utaratibu mwingine ukamilike kwenye hayo mashirika na kanidokeza kwamba Kuna uwezekano hayo mashirika yenyewe ndio yakawaaita waliofaulu kazini.
Kwenye hili naweza kukubaliana na wewe kwa 99%...maana kuna interview za TRC zilifanyika since Dec.2018 za level ya Manager's mpk leo hakuna tangazo lolote lililotolewa la kuitwa kazini.
 
Hii itakuwa ni mbaya, maana kuna uwezekano wakafanya interview watu X, then wakaitwa kazini watu Y....
Sidhani kama kuna possibility hyo maana majina ya watakaoajiriwa mwisho wa siku ni lzm yawasilishwe "Utumishi" for records and all necessary documentations...kwa mantiki hyo ni lzm Utumishi wata-refer kwenye database yao kuangalia majina waliyoletewa kama yana-match na waliyonayo kwa waliosailiwa...in short chance ya kuchomeka jina lolote ni 0.000%
 
Sidhani kama kuna possibility hyo maana majina ya watakaoajiriwa mwisho wa siku ni lzm yawasilishwe "Utumishi" for records and all necessary documentations...kwa mantiki hyo ni lzm Utumishi wata-refer kwenye database yao kuangalia majina waliyoletewa kama yana-match na waliyonayo kwa waliosailiwa...in short chance ya kuchomeka jina lolote ni 0.000%
Yap hata mimi nafahamu hivyo
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom