maramia
JF-Expert Member
- Jul 17, 2015
- 2,030
- 1,344
Sikutegemea kama haya ninayoyaona katika shule ya Ngudu high school ningeweza kuyaona yakifanywa katika awamu hii ya Rais Magufuli.
Ya waalimu walioko mazoezi (field) kutumia muda wa kuanzia saa 11 jioni hadi saa 2 usiku na wakati mwingine muda wa kazi na katika majengo ya shule kufundisha tyusheni ya topic muhimu za kidato cha 5 na 6 na kisha kutoa majaribio na kutunga mitihani kutoka kwenye topic zile tu wanazofundisha tusheni ili kuwalazimisha wale wasio lipia walipie kusoma masomo hayo ya ziada.
Kwa kweli hata wale tulio na kauwezo kidogo tunaolipia tunaumia sana, hali hii haitupendezi kwa sababu inatuumiza kiuchumi na inatujengea matabaka ya makusudi na ya kijinga.
Cha ajabu kauli ya waalimu hawa ambao wameungana na waalimu wa ajira wa shule hii ni "Ukitaka vya bure rudi O level"
Kwa kweli huku ni kutunyanyasa tyusheni ya mwanafunzi kulipia mpaka laki moja watoto wa wakulima maskini wataitoa wapi?
Mheshimiwa Ndalichako tafadhali waokoe watoto hawa walioko shule hii kabla hawajafelishwa elimu na maisha na hawa waalimu wenye tamaa za kijinga.
Sent using Jamii Forums mobile app
Ya waalimu walioko mazoezi (field) kutumia muda wa kuanzia saa 11 jioni hadi saa 2 usiku na wakati mwingine muda wa kazi na katika majengo ya shule kufundisha tyusheni ya topic muhimu za kidato cha 5 na 6 na kisha kutoa majaribio na kutunga mitihani kutoka kwenye topic zile tu wanazofundisha tusheni ili kuwalazimisha wale wasio lipia walipie kusoma masomo hayo ya ziada.
Kwa kweli hata wale tulio na kauwezo kidogo tunaolipia tunaumia sana, hali hii haitupendezi kwa sababu inatuumiza kiuchumi na inatujengea matabaka ya makusudi na ya kijinga.
Cha ajabu kauli ya waalimu hawa ambao wameungana na waalimu wa ajira wa shule hii ni "Ukitaka vya bure rudi O level"
Kwa kweli huku ni kutunyanyasa tyusheni ya mwanafunzi kulipia mpaka laki moja watoto wa wakulima maskini wataitoa wapi?
Mheshimiwa Ndalichako tafadhali waokoe watoto hawa walioko shule hii kabla hawajafelishwa elimu na maisha na hawa waalimu wenye tamaa za kijinga.
Sent using Jamii Forums mobile app